CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, amepokelewa kwa shangwe kubwa katika Kata ya Mlowo, Jimbo la Mbozi mkoani Songwe, wakati akiendelea na ziara yake ya kisiasa katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Taarifa mbalimbali za chama zilionesha maandalizi ya mapokezi hayo yaliyofanyika mchana wa Juni 24, 2026.

Wafuasi na wanachama wa CHADEMA walijitokeza kwa wingi kumpokea kiongozi huyo, hali inayotafsiriwa na baadhi ya wachambuzi kama ishara ya mwamko wa kisiasa kuelekea mikutano ya chama hicho.

Baada ya mapokezi ya Mlowo, macho na masikio ya wengi sasa yanaelekezwa Tunduma ambako shughuli za jioni zinatarajiwa kuvuta umati mkubwa zaidi.
1782308717590.jpg
1782308714627.jpg
 
CCM CHAMA CHANGU TUKUBALI MSIGWA AMETUPIGA 3–0!

📝 Naandika haya kama mwanachama mwaminifu wa Chama Cha Mapinduzi anayependa kuona chama chetu kinaendelea kushinda kwa hoja, sera na utekelezaji wake. Lengo langu si kukikosoa chama changu kwa kukidhoofisha, bali kukikosoa ili kijirekebishe.

🤔 Kwa mtazamo wangu, katika ziara hii tumepoteza mwelekeo wa kisiasa. Tumetumia nguvu nyingi kumjibu mtu mmoja badala ya kujibu hoja zinazowasilishwa kwa wananchi.

Chama changu kinashindwa kujibu hoja za Heche? 📢

👥 Kadri mikutano ya John Heche inavyoendelea, ndivyo anavyozidi kupata uungwaji mkono. Ukiwasikiliza wananchi na kuangalia namna wanavyopokea hoja zake, utaona wazi kuwa anazungumza mambo yanayowafanya wafikiri.

❓ Lakini sisi tunafanya nini?

📊 Badala ya kujibu hoja zake kwa sera, takwimu na mafanikio ya serikali yetu, tunaonekana kushambulia watu binafsi. Serikali yetu imefanya mambo mengi mazuri. Kwa nini tunashindwa kuyasema kwa nguvu na kwa lugha inayowafikia wananchi?

📌 Kwa mfano:

1️⃣ Kwanza, Heche anasema serikali ya CCM imeshindwa kutumia rasilimali za Taifa kuwakomboa Watanzania kiuchumi kwa zaidi ya miaka 60 ya Uhuru. Hata hoja hii hatuijibu kwa nguvu na takwimu.

2️⃣ Pili, anaendelea kudai kuwa serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan haina uhalali wa kisiasa kwa sababu, kwa mtazamo wake, haikuchaguliwa moja kwa moja na wananchi. Badala ya kutoa majibu ya kikatiba na kisiasa, tunaonekana kukwepa hoja, jambo linalowafanya baadhi ya wananchi kuendelea kuamini simulizi hizo.

Halafu tunampa Msigwa umuhimu usiohitajika 🎯

🗣️ Wakati viongozi wangu wa Chama Cha Mapinduzi, wakiongozwa na Comrade Kihongosi pamoja na Comrade Ally Hapi, wakijitahidi kumshughulikia Peter Simon Msigwa kwa hoja kwamba ameondoka baada ya kukosa cheo, Msigwa mwenyewe anaendelea kusisitiza kuwa aliondoka CCM kutokana na matukio ya mauaji ya Oktoba 29.

💔 Anasema hawezi kuendelea kuishi akiwa sehemu ya dhambi ya damu za watu wasio na hatia.

❓ Swali langu ni moja tu:

⚖️ Ni kiongozi gani wa chama changu aliyesimama kujibu hoja hiyo moja kwa moja?

🥅 Chama changu tunapiga penalti nje ya goli. Teknolojia haidanganyi. Je, kweli tunaweza kutumia nguvu na rasilimali nyingi kiasi hiki kwa sababu ya mwanachama mmoja aliyeamua kuondoka? Hii inatuma ujumbe gani kwa wananchi?

📍 Mifano ipo wazi:

1️⃣ Tunatafuta na kukodisha screen kubwa ili wanachama watazame mkutano wa CHADEMA na kumsikiliza mwanachama aliyetuacha. Je, chama chetu hakina ajenda zake tena? Tunamsubiri Heche aseme ndipo tujibu?

2️⃣ Nilikuwepo kwenye maandalizi ya kuwapokea viongozi wetu hapa Iringa. Kulikuwa na uratibu wa bodaboda, mafuta na posho kwa vijana ili kupamba ujio wa viongozi. Je, nguvu zote zile zilikuwa kwa ajili ya kumjibu Msigwa pekee? Mbona utekelezaji wa Ilani ya CCM haukuwa ajenda kuu?

3️⃣ Tumetumia karibu robo tatu ya muda wa mikutano yetu kumzungumzia mtu aliyeamua kuondoka mwenyewe. Hivi leo kina David Silinde, Mwita Waitara, Dkt. Kitila Mkumbo, Patrobas Katambi, Pauline Gekul, Joshua Nassari, Peter Lijualikali, Dkt. Vincent Mashinji, Caristus Lazaro, Bananga na wengine wengi, kama wangeachwa walipokuwa, leo wangekuwa wanachama wa CCM?

🚶 Msigwa kuondoka ni haki yake ya kisiasa. Tulimpata mchezaji mzuri lakini hatukujua kumtumia ipasavyo. Sasa kwa nini gharama zote hizi?

📩 Nimekuwa nikipeleka maoni yangu ndani ya chama mara kwa mara, lakini mara nyingi hayasikilizwi. Leo nimeamua kuyaandika hapa kwenye kundi letu la WhatsApp ili tuyatafakari kwa pamoja.

🏛️ Chama kikubwa kama CCM hakipaswi kuonekana kinamfuata mtu mmoja. Kinapaswa kuongoza mjadala wa kitaifa kwa sera, hoja na mafanikio ya serikali yake.

📢 Tukubali ukweli. Katika mapambano ya hoja, hisia hazitoshi. Tunahitaji majibu ya kisera, takwimu, mawasiliano bora na uwezo wa kuwashawishi wananchi. Tukitumia muda mwingi kushambulia watu badala ya kujibu hoja zao, tunawapa nafasi ya kuonekana wanashinda mbele ya umma.

⚽ Kwa mtazamo wangu, katika awamu hii ya ziara tumepigwa 3–0. Lakini mechi bado haijaisha.

💡 Tujitathmini, turekebishe mkakati wetu, tutoke kwenye vikao vyetu tukiwa na hoja zenye nguvu, na tuwaeleze wananchi kwa ufasaha utekelezaji wa Ilani ya CCM na kazi zinazofanywa na serikali yetu.

🌿 Kidumu Chama Cha Mapinduzi. Kidumu chama tawala.

Comrade Ally Ismail Kombo
1782326450239.jpg
 
Mhe. John Heche akiwa njiani kuelekea Mkoa wa Katavi kuendelea na Operesheni #KatibaMpya #FreeTunduLissu amefanya zoezi la kupandisha bendera katika vizimba vya Chama mjini Sumbawanga.
1782390817001.jpg
1782390814099.jpg
 
‼️HABARI MBAYA‼️

Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mwanza Adam Chagulani amekamatwa na Polisi jioni hii, kapelekwa kituo cha Polisi Central Mwanza.

Polisi wamembambika kesi wanadai kaleta Vijana kutoka nchini Kenya ili waje kuandamana.

Maandamano ya 7/7 yamewapanikisha mpaka wamedata wanakamata kila mtu ambae wanadhan anaushawishi kwenye eneo lake.

Jambo moja ambalo wanapaswa kujua ni kwamba kukamata watu hakuwezi kuwasaidia kuzuia Maandamano ya Wananchi sana sana kunazidi kutuongezea morali. #77Tunatoka 💪
1782793381315.jpg
 
Dua na sala mapema leo, Jumanne, tarehe 30 Juni 2026, kabla ya kuanza kwa kikao cha kawaida cha Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kinachofanyika mjini Kigoma, Kanda ya Magharibi.
1782872364855.jpg
1782872361847.jpg
 
KANDA YA VICTORIA.

TISHIO LA UHAI.

Tumepokea taarifa za kupotea/kutooneka kwa Neema Chozaile ambaye ni Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Geita.

Neema Chozaile alitoka nyumbani kwake kwenda kuhemea mahitaji ya familia tarehe 29.6.2026 majira ya saa 4:00 asubuhi.

Hadi muda huu tunatoa taarifa hajarudi nyumbani na simu zake hazipatikani.

Tunatoa wito kwa wanaomshikiria kwa sababu yoyote ile wamwachie huru akiwa mzima.

Tunalitaka Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita lichukue hatua za dharura kuhakikisha Neema Chozaile anapatikana akiwa hai na bila majeraha.

Tunatoa wito kwa watanzania wote kusimama na kukomesha tabia hii ya kishenzi ya kuteka na kupoteza watu. Tabia ya kuteka na kupoteza watu haikubaliki mbinguni na hata hapa duniani. Sasa ni wakati wa kutumia gharama yoyote ile kukomesha tabia hii ya kishetani.

Free Neema Chozaile

Zacharia Obad
Katibu wa CHADEMA Kanda ya Victoria.
1782872613743.jpg
 
Jana baada ya kikao cha Kamati Kuu, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, Mhe. John Heche, akiwa ameambatana na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar pamoja na viongozi wengine wa chama, walitembelea Makaburi ya Rubengera ambako walitoa heshima zao kwa kutembelea kaburi la marehemu Bi. Hajjat Shida Salum Mohamed, aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama.

Aidha, viongozi hao walifika katika eneo la Mji Mwema nyumbani kwa marehemu Ndugu Ally Kisara, aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Kigoma, ambaye alifariki dunia hivi karibuni. Wakiwa pamoja na familia ya marehemu, viongozi hao waliungana nao katika dua, wakimuombea marehemu apumzike kwa amani na kuiombea familia nguvu, faraja na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.
1782891710217.jpg
1782891707136.jpg
1782891704541.jpg
1782891701919.jpg
1782891698979.jpg
1782891696049.jpg
1782891692805.jpg
1782891689915.jpg
 
 
KINACHOENDELEA KIGOMA KUHUSU KIFO CHA DEREVA WA MHE. HECHE.

Anaandika Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa Deogratius Mahinyila

Ni muhimu pia taarifa zikawa zinasemwa zote.

1. Marehemu pia alikutwa na pesa Cash na nilikabidhiwa mimi kiasi cha Shilingi laki 4 na elfu 28.

2. Alikuwa ametokwa na damu mdomoni.

3. Pathologist ambao ndo wanatakiwa kufanya postmortem walifika usiku wa kumkia leo wametoka Mkoani Mwanza na Geita hadi muda huu majira ya saa nane mchana na dakika bado Postmortem haijaanza.

4. Tumejulishwa kwamba kuna Pathologist mwingine anakuja kuungana na waliopo yeye anatokea Dodoma ni wa Serikali.

5. Tumejulishwa kwamba wataalam wote hao baada ya kufika Kigoma, leo asubuhi walipelekwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Simon Sirro, Hatujui walienda kufanya kikao cha nini na kwa ajili ya nini. Je huo ndio utaratibu wa kazi yao?

6. Hapo hapo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma amenukuliwa na Clouds TV alisema kwamba kwa uzoefu wa Polisi (Yeye alikuwa IGP) kifo cha Maradufu ni cha kawaida tu. Je majibu ya uchunguzi yakija tofauti na maoni ya Polisi mtasemaje? Je majibu ya uchunguzi yakija kufanana na maoni ya Polisi mtakataaje kuwa ni matokeo ya mjadala uliofanyika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa leo asubuhi??

6. Muda ni Mwalimu mzuri. Ukweli una tabia ya kuchelewa kidogo kibinadamu lakini lazima utajidhihirisha ndani ya wakati wake sahihi, tuupe muda nafasi.

7. Sisi tutaendelea kuwepo hapa Mochwari hadi hapo Wataalamu watakapofika na Uchunguzi kufanyika. Matokeo yoyote ya Uchunguzi yatatusaidia kuweka sawa kumbukumbu ya kila jambo.

Mahinyila.
02/07/2026.
Maweni, Kigoma.
1783004652019.jpg
 
Jioni hii, ibada fupi ya kumwombea marehemu Suez Dani Maradufu imefanyika katika Hospitali ya Mkoa wa Kigoma, Maweni, kabla ya mwili wake kuondoka na kuanza safari kuelekea Tarime, mkoani Mara, kwa ajili ya maandalizi ya mazishi.
1783106498265.jpg
1783106494701.jpg
1783106491093.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom