Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 369,077
- 853,940
- Thread starter
- #281
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, amehoji sababu za kuahirishwa kwa kesi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, akitaka uwazi zaidi kuhusu mwenendo wa shauri hilo.
Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Mwembetogwa June 13, 2026mkoani Iringa, Heche amesema kuna maswali ambayo yanahitaji majibu kuhusu hatua za kuahirishwa kwa kesi hiyo.
"Mnaficha nini?" amehoji Heche mbele ya umati wa wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Kiongozi huyo wa CHADEMA pia amezungumzia suala la amani na usalama nchini, akisisitiza kuwa jukumu la kulinda amani ni la wananchi wote na si la vyombo vya usalama pekee.
"Polisi hawawezi kulinda amani peke yao, amani inalindwa na raia," amesema.
Heche ameeleza kuwa baadhi ya viongozi na wanachama wa chama hicho wameamua kuendelea kusimamia wanachokiamini kuwa ni haki zao za kikatiba bila kuongozwa na hofu.
"Sisi wengine tumekataa kuogopa, hatutakubali," amesema huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Kauli hizo zimetolewa wakati CHADEMA ikiendelea na kampeni zake za kisiasa na mikutano ya hadhara katika maeneo mbalimbali nchini, ambapo viongozi wake wamekuwa wakizungumzia masuala ya demokrasia, haki za kiraia na utawala wa sheria.
Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Mwembetogwa June 13, 2026mkoani Iringa, Heche amesema kuna maswali ambayo yanahitaji majibu kuhusu hatua za kuahirishwa kwa kesi hiyo.
"Mnaficha nini?" amehoji Heche mbele ya umati wa wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Kiongozi huyo wa CHADEMA pia amezungumzia suala la amani na usalama nchini, akisisitiza kuwa jukumu la kulinda amani ni la wananchi wote na si la vyombo vya usalama pekee.
"Polisi hawawezi kulinda amani peke yao, amani inalindwa na raia," amesema.
Heche ameeleza kuwa baadhi ya viongozi na wanachama wa chama hicho wameamua kuendelea kusimamia wanachokiamini kuwa ni haki zao za kikatiba bila kuongozwa na hofu.
"Sisi wengine tumekataa kuogopa, hatutakubali," amesema huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Kauli hizo zimetolewa wakati CHADEMA ikiendelea na kampeni zake za kisiasa na mikutano ya hadhara katika maeneo mbalimbali nchini, ambapo viongozi wake wamekuwa wakizungumzia masuala ya demokrasia, haki za kiraia na utawala wa sheria.