CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

JESHI LA POLISI LIMEVAMIA NYUMBANI KWA MBYELLA (ANAYEUZA NGUO NA VIFAA VYA CHADEMA NA KUONDOKA NA TSHIRT, KOFIA, NGUO NA BENDERA ZA CHADEMA.

Nimepata taarifa kwamba usiku wa kuamkia leo mida ya saa nane, Jeshi la Polisi limevamia nyumbani kwa Yoromu Mbyella, mfanyabiashaa ambae huwa anauza sare za CHADEMA wakidai wanamtafuta kwa kosa la kutengeneza Tshirt zenye maandishi “FREE TUNDU LISSU”

Kwa mujibu wa mtoa taarifa, Mbyella mwenyewe hakuwepo nyumbani so Polisi walifanya upekuzi na baada ya kumkosa waliondoka kwa muda.

Baadaye walirejea wakiwa na Gari aina ya Fuso kisha wakabeba nguo zote na vifaa vyenye nembo ya chadema ikiwemo Bendera za Chadema ambazo huwa anauza kisha wakaondoka na mali hizo bila kutoa sababu zaidi.

Kwa mujibu wa mke wa Mbyella (anayeuza nguo na vifaa vya chama) nyumbani kwao kuna duka la kuuza vifaa hivyo ambavyo Polisi wameondoka navyo vyote.

Tunafuatilia kufahamu sababu hasa ya kuvamia nyumbani hapo na kuleta taharuki kwa mtu ambaye hata kama wangemhitaji Polisi, wangempatia wito na angefika kituoni kama Polisi walikuwa na jambo na Mbyella.

Kuuza vifaa vya chama kama nguo, kofia, Bendera siyo kosa kisheria.
1780222898591.jpg
 
Back
Top Bottom