CHADEMA Special Thread

CHADEMA Special Thread

Tazama Picha zikionyesha Msaidizi wa TUNDU LISSU akiwa ameumizwa vibaya na watekaji usiku wa kuamkia leo.

David Djumbe alitekwa siku ya Jana Maeneo ya Bunju akiwa na rafiki yake wakati wa kutekwa alipiga kelele sana bodaboda wakafukuzia GARI kwa nyuma

Walipofika umbali wa kilometa kama 3 watekaji walipoona bodaboda bado wanafuatilia GARI, watekaji walishuka na kuanza kupiga RISASI wakati huo Djumbe wakiwa wamemuacha ndani ya GARI.

Ndio David Djumbe akapata upenyo na kukimbia akiwa na Pingu mkononi na ameporwa damu kama anavyoonekana.
.
1779358102425.jpg
 
Jeshi la Polisi Oysterbay limemfungua pingu David Jumbe, ambazo zilikuwa zimembana kisiasi cha kusababisha mikono kuvimba.

Djumbe alitekwa usiku wa kuamkia leo akafanikiwa kuwakimbia watekaji.

Maumivu haya Mpaka lini, sasa Djumbe apelekewe hospitalini.
Imeandikwa na Twaha Mwaipaya
1779358778339.jpg
1779358775743.jpg
1779358772120.jpg
 
Katibu Mkuu wa CHADEMA Mhe. JOHN MNYIKA ameongoza zoezi la upandishaji wa bendera katika vizimba mbalimbali Arusha Mjini. Zoezi hilo limefanyika leo tarehe 22 Mei 2026 ambapo hapo baadae mchana Chama kinatarijia kufanya uzinduzi wa Operesheni #KatibaMpya #FreeLissu Kanda ya Kaskazini.
1779477738758.jpg
1779477735586.jpg
1779477738758.jpg
 
Back
Top Bottom