Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 364,912
- 842,384
- Thread starter
- #201
UTEKAJI UNAUMIZA WANANCHI.
Rhoda Kunchela Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Katavi amewatembelea wazazi wa Juma Kaswahili ambaye ameripotiwa kupotea katika mazingira yasiyojulikana tangu Mei 18, 2025 huku familia yake ikiendelea kuiomba Serikali kusaidia kupatikana kwake.
Akizungumza baada ya kutembelewa na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), baba mzazi wa Juma Kaswahili, Gerevasi Makwani amesema familia imekuwa katika majonzi makubwa tangu kutoweka kwa kijana huyo.
“Mimi ni mzazi wa Juma Kaswahili, kijana aliyepotea katika mazingira yasiyojulikana. Tarehe 18 Mei 2025 kijana wangu alipotea mpaka leo hajulikani alipo. Nimehangaika mitandaoni na vituoni lakini hapatikani mpaka leo,” amesema Makwani.
Amesema kutoweka kwa mwanawe kumeiathiri familia kiuchumi na kijamii kwa kuwa alikuwa msaada mkubwa kwa wazazi wake na familia kwa ujumla.
“Naiomba Serikali kusaidia, huyo kijana alikuwa ni msaada wetu kwa sababu tumemsomesha ili aisaidie familia lakini mpaka sasa tuna majonzi makubwa sana. Kiuchumi tumeteteleka, kwa msaada na maneno alikuwa anatusaidia sana yule kijana,” amesema.
Aidha, amewashukuru viongozi wa CHADEMA pamoja na wanachama wa chama hicho kwa namna wanavyofuatilia suala hilo.
“Tunawashukuru viongozi wa chama chetu cha CHADEMA kama John Heche na wanachama wengine kwa namna ambavyo wanalishughulikia sana jambo hili,” ameongeza.
Kwa upande wake, mama mzazi wa Juma Kaswahili, Teleza Rukasi amesema bado ana maumivu makubwa kutokana na kutofahamu alipo mwanawe wala hali yake.
“Hili linanisikitisha sana mwanangu kupotea hivi hivi sijui alipo, sijui amekufa au yupo hai. Naiomba Serikali ilifanyie kazi kabisa hili jambo ili mwanangu arudi, alikuwa ananisaidia,” amesema kwa huzuni.
Mpaka sasa, hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu mahali alipo Juma Kaswahili huku familia na viongozi wa CHADEMA wakiendelea kuitaka Serikali na vyombo vya usalama kuongeza juhudi za kumtafuta.
Rhoda Kunchela Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Katavi amewatembelea wazazi wa Juma Kaswahili ambaye ameripotiwa kupotea katika mazingira yasiyojulikana tangu Mei 18, 2025 huku familia yake ikiendelea kuiomba Serikali kusaidia kupatikana kwake.
Akizungumza baada ya kutembelewa na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), baba mzazi wa Juma Kaswahili, Gerevasi Makwani amesema familia imekuwa katika majonzi makubwa tangu kutoweka kwa kijana huyo.
“Mimi ni mzazi wa Juma Kaswahili, kijana aliyepotea katika mazingira yasiyojulikana. Tarehe 18 Mei 2025 kijana wangu alipotea mpaka leo hajulikani alipo. Nimehangaika mitandaoni na vituoni lakini hapatikani mpaka leo,” amesema Makwani.
Amesema kutoweka kwa mwanawe kumeiathiri familia kiuchumi na kijamii kwa kuwa alikuwa msaada mkubwa kwa wazazi wake na familia kwa ujumla.
“Naiomba Serikali kusaidia, huyo kijana alikuwa ni msaada wetu kwa sababu tumemsomesha ili aisaidie familia lakini mpaka sasa tuna majonzi makubwa sana. Kiuchumi tumeteteleka, kwa msaada na maneno alikuwa anatusaidia sana yule kijana,” amesema.
Aidha, amewashukuru viongozi wa CHADEMA pamoja na wanachama wa chama hicho kwa namna wanavyofuatilia suala hilo.
“Tunawashukuru viongozi wa chama chetu cha CHADEMA kama John Heche na wanachama wengine kwa namna ambavyo wanalishughulikia sana jambo hili,” ameongeza.
Kwa upande wake, mama mzazi wa Juma Kaswahili, Teleza Rukasi amesema bado ana maumivu makubwa kutokana na kutofahamu alipo mwanawe wala hali yake.
“Hili linanisikitisha sana mwanangu kupotea hivi hivi sijui alipo, sijui amekufa au yupo hai. Naiomba Serikali ilifanyie kazi kabisa hili jambo ili mwanangu arudi, alikuwa ananisaidia,” amesema kwa huzuni.
Mpaka sasa, hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusu mahali alipo Juma Kaswahili huku familia na viongozi wa CHADEMA wakiendelea kuitaka Serikali na vyombo vya usalama kuongeza juhudi za kumtafuta.