Rev. Kishoka,
Mkuu wangu pengine umesahau au huelewi kwamba vita ya Chadema ni kuwaondoa CCM madarakani. Dhamira hii haijabadilika kwani hii ni Vita baridi ya kisiasa..Na kutokana na kutoelewa huku ndiko kumewafanya wengi wenu msijiunge na Chadema ktk vita hii toka awali. Chadema will use all means hata iwe vifaa vya CCM wenyewe kupata ushindi kama Nyerere alivyompiga Idd amin na mizinga yake mwenyewe kushinda vita.
Kwa hiyo mnashindwa kuelewa kwamba hapa sii swala la demokrasia at it's best, ila ni kuitumia demokrasia hiyo hiyo inapowezekana kutumika kwani Mungu katukataza kuua lakini ukiwa vitani huwezi kuweka silaha chini ukisema ati Mungu alikataza kuua na haitakuwa haki kkuua ili upande kumshinda adui yako..
Strategy ya Chadema ni ya Ushindi by all means hayo ya Demokrasia na Itikadi huu sio wakati wake na ndio maana hadi sasa hivi mnashindwa kuwaelewa Chadema kwani kama ingebidi kuchukua silaha ingekuwa hatuzungumzii tena demokrasia wala usalama wa Taifa isipokuwa kwa uzito wa hatua walizochukua.
Alichofanya Zitto ni kuchekecha hao mizoga ili kupata kinachoweza kulika. Zitto baada ya kutopa taarifa za hao waliojiunga wale wenye woga na kujificha wamekimbilia kukana kujitoa CCM. na kama nilivyowahi kusema siku za nyuma kutoka CCM na kujiunga Chadema haitakuwa kazi ndogo kwao. Watatangazwa magazetini na hakuna Usiri, watavikwa majezi na penbgine hata kupewa wajibu ambao hawatapenda kuufanya ili mradi wanapimwa Uaminifu wao kwa chama na hasa vita hii.
Kwa Chadema hili swala lipo beyond maslahi ya Chama au matakwa ya demokrasia - ni swala la Mustakabali wa Taifa letu ambao uko hatarini. Uhatari ambao pengine nyie mnashindwa kuusoma au kukifikiria isipokuwa mnaona tu sheria na taratibu za demokrasia ambayo haipo nchini to begin with..Tukishindwa sasa hivi, they will be no 2015...Take my word for that!
WEWE jamaa una akili !