Mwanamageuko
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 8,602
- 5,569
Kumuombea mgonjwa ama mtu yeyote aliyepatwa na kadhia yoyote ni jambo la kiungwana na linalofanywa na binadamu wenye utu kinyume na wafanyavyo baadhi ya wanadamu wenye roho za fisi kama sio nguruwe.Tunamuimbea Lissu apone aje aendelee na majukumu yake kama kawaida. Hakuna kitu cha thamani zaidi kwa binadamu zaidi ya uhai, hata kama ni adui yako, muombee njaa, usimuombee kifo.
Natumai huyo jamaa atapona na atakuja kuendelea na majukumu yake na kuungana na familia yake.
Kurudi kwa mh. TL Kutazidi kupeperusha na kutapanya manyoa ya kuku yaliyokwishafunuliwa na upepo kwa hakika tutaona zaidi ya nyeti za kuku.