Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,811
- 6,506
Wanachama wa Chadema ukitaka kuwaona subiri mikutano ya Chadema Chopa akitua utawaona, Chopa ikiondoka na wao wanaondoka.
Maswali ya MMK yamelenga kama ulivyobainisha. Kwa nini chama kinashindwa wakati kinapenda kuwaaminisha umma kama kina wanachama, wapenzi na washabiki wengi zaidi ya vyama vingine nchini.
Unakumbuka pale walipokuja na jina lao pale uwanja wa jangwani eti kwa vile kulikuwa na nyomi ambayo haijawahi kutokea.
Wana CDM Hawapendi kuambiwa ukweli. Halafu nafikiri wengi wanapumbazwa na hii mitandao wakati uwanja hasa wa mapambano uko vijijini ambako Watanzania wengi wanaishi. Viongozi wao huwa wanaenda vijijini na chopa kama watalii.
Nafikiri hawa makamanda wanapambana na adui ambaye siye. Hawawezi kumpata na kumuua adui kupitia mitandao ya 'kijamii'.