CHADEMA kina wanachama wangapi?

Tukitaka kufanya Fair Judgement, Mwanakijiji hana Credibility yoyote ya kuiongelea Chadema hasa ukizingatia wakati Chadema ndio kinakubalika kwa Watanzania yeye akawa yuko bize kugawanya watu ili wajiunge CCJ.

Ndio maana nimemuuliza hapa haya unayoyasema hapa mbona ukushauri yafanyike CCJ mpaka chama chao kikafutwa kwa kushindwa kuleta Wanachama Live ili wahakikiwe? au anadhani yeye angehakikiwa kwa kupitia Sype kutokea Detroit?

Tupunguze unafki, pamoja na udhaifu mkubwa uliounesha Mwanakijiji bado unaheshimika na hata mimi nakuheshimu, usitake tena kupoteza hawa trust.

No Matola hapo nitamtetea nauhakika anania nzuri sana..Ila anaonyesha concern ya jambo ambalo wengi hawatalielewa....Anahitaji mabadiliko haraka kuliko wengi tunavyo amini..Anataka kula matunda ya kazi ya mikono yake..Lakini mi namwambia achanganye na sacrifice kidogo aone utamu wake..Maana hata Yesu alikubali kubeba dhambi za watu lakini baba yake alipomwacha kwa madakika machache tu akataka kukacha ila kwavile alikuwa na uhakika wa matokeo alifunga macho nakuangalia utukufu ule mkubwa zaidi kuliko ile aibu na maumivu ya wakati aliyokuwepo..Ndicho kinachomsumbua ndugu yangu huyu....Vinginevyo anamapenzi mazito na mahaba juu na CDM kuliko mimi wa kuchonga...lol!
 
Nyie endeleeni kuwapamba kwa mashada ya majani na kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa mkidhani mnawasaidia. Watengenezeeni udhuru wa kila namna ya kwanini hawakufanya vizuri sasa na kwanini hawakufanya vizuri 2010 au kwenye zile chaguzi za diwani zilizopita. Mjiandae kuwatengenezea udhuru mwingine wakikosa kufanya vizuri 2015.. na 2020. Mtakuja kushtuka sote tunawajukuu na vitukuu huku CCM kizazi cha nne kikiwa kimeshika hatamu ya madaraka.

Lazima tuwapambe MMM tunataka kuoa hayo mambo mengine tutaelekezana chumbani..Wewe sasa unaonekana unalako jambo na wengine ambao wana lao jambo basi wanapanda juu ya mgongo wako..Shauri lako aise utageuka nguzo ya chumvi we tamani tu uzuri wa sodoma na gomora..Acha viteketee tutajenga upya.
 
Si lazima haya tunayoyapigania leo mafanikio yake tuje kuyashuhudia kwa macho, tunaweka Foundation ya nchi Historia itajiandika yenyewe kwamba watoto zetu wakati wanakula matunda tunayopigania leo watajuwa kwamba Baba zao tulikataa katakata kutiwa vidole vya makalioni na Watawala.

Wewe kama ni Political analyst mzuri hivi unashindwa kujuwa nafasi ya wanawake kwenye siasa zetu? nilitegemea angalau ushauri new reform of Bawacha maana Wanawake ndio wapiga kura wakuu, huwa hawaganduki vituoni mpaka amepiga kura yake, na hawa majority bado ni royal kwa CCM.

Hilo ndilo tatizo la MMM.....Well said kamanda afadhali umweleze labda atakuelewa wewe!
 
Tukitaka kufanya Fair Judgement, Mwanakijiji hana Credibility yoyote ya kuiongelea Chadema hasa ukizingatia wakati Chadema ndio kinakubalika kwa Watanzania yeye akawa yuko bize kugawanya watu ili wajiunge

oh boy; sawa wewe ni more credible than I; kwa hiyo wewe pekee ndio unatakiwa uzungumzie CDM na wengine wote hawastahili.
 
Wewe kama ni Political analyst mzuri hivi unashindwa kujuwa nafasi ya wanawake kwenye siasa zetu? nilitegemea angalau ushauri new reform of Bawacha maana Wanawake ndio wapiga kura wakuu, huwa hawaganduki vituoni mpaka amepiga kura yake, na hawa majority bado ni royal kwa CCM.

Na hili huoni kuwa linahusiana na idadi ya wanachama? au hujasoma hapo juu nilichosema juu ya "demographics". Sasa hivi unajuaje kama wanachama wengi siyo wanawake?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
No Matola hapo nitamtetea nauhakika anania nzuri sana..Ila anaonyesha concern ya jambo ambalo wengi hawatalielewa....Anahitaji mabadiliko haraka kuliko wengi tunavyo amini..Anataka kula matunda ya kazi ya mikono yake..Lakini mi namwambia achanganye na sacrifice kidogo aone utamu wake..Maana hata Yesu alikubali kubeba dhambi za watu lakini baba yake alipomwacha kwa madakika machache tu akataka kukacha ila kwavile alikuwa na uhakika wa matokeo alifunga macho nakuangalia utukufu ule mkubwa zaidi kuliko ile aibu na maumivu ya wakati aliyokuwepo..Ndicho kinachomsumbua ndugu yangu huyu....Vinginevyo anamapenzi mazito na mahaba juu na CDM kuliko mimi wa kuchonga...lol!
Mimi namuelewa sana Mwanakijiji na ni mmoja wa followers wake wakubwa na amefanya kazi kubwa sana kwa nchi yetu, kwa wale wafuatiliaji wa mambo wanalijuwa hili vyema.

Labda na yeye nimkumbushe kama Mtanzania hii vita tunayopigana ni do or die, wote tunatamani kuona na kuyashuhudia wenyewe mabadiliko yakitokea, lakini vile vile namshauri MM na yeye aplay part yake ili Diasporas nao waruhusiwe kupiga kura huko walipo.

Kinachonisikitisha ni kuona Watanzania wenzetu ambao wanaishi Ughaibuni badala ya kuwa na Jumuiya za Kitanzania zenye nguvu na wawe wameangukia kwenye ulevi wa kufunguwa matawi ya vyama, ndio maana sijawahi kuona ajenda ya Watanzania inayoongea kwa sauti moja kwamba tunataka hiki na serikali inapaswa kuwasikiliza.

All in all sasa ni wakati wa kila mtu kutimiza wajibu, mimi naanza kwa kuishauri Chadema waivunje Bawacha haraka na kufanyike New Reform na watafutwe na kushawishiwa kina mama majasiri wajiune na Chama kuendesha taasisi hizo, nazijuwa vyema fitina za siasa Tanzania bila kuwakamata kina mama bado kazi ngumu sana. sina tatizo na wasichana wengi wao ni waelewa sana hasa wenye elimu ya vyuo ndio hawana shida kabisa.
 
Tukitaka kufanya Fair Judgement, Mwanakijiji hana Credibility yoyote ya kuiongelea Chadema hasa ukizingatia wakati Chadema ndio kinakubalika kwa Watanzania yeye akawa yuko bize kugawanya watu ili wajiunge CCJ.

Ndio maana nimemuuliza hapa haya unayoyasema hapa mbona ukushauri yafanyike CCJ mpaka chama chao kikafutwa kwa kushindwa kuleta Wanachama Live ili wahakikiwe? au anadhani yeye angehakikiwa kwa kupitia Sype kutokea Detroit?

Tupunguze unafki, pamoja na udhaifu mkubwa uliounesha Mwanakijiji bado unaheshimika na hata mimi nakuheshimu, usitake tena kupoteza hawa trust.

CCJ hata mimi MMM aliniingiza mjini kwa mara ya kwanza..Ila baadaye alinieleza ukweli nisiazime akili yangu kwake niwe nafikiria independent..Ndiyo nika pick myself from the sand na ku-arise ni shine bila kutegemea mtu....Nia yake ilikuwa njema ndiyo maana aliweza kuwarudisha aliowapotosha!
 
All in all sasa ni wakati wa kila mtu kutimiza wajibu, mimi naanza kwa kuishauri Chadema waivunje Bawacha haraka na kufanyike New Reform na watafutwe na kushawishiwa kina mama majasiri wajiune na Chama kuendesha taasisi hizo, nazijuwa vyema fitina za siasa Tanzania bila kuwakamata kina mama bado kazi ngumu sana. sina tatizo na wasichana wengi wao ni waelewa sana hasa wenye elimu ya vyuo ndio hawana shida kabisa.

Matola.. ushauri wakko wa kutaka BAWACHA ivunjwe kwa watu wengine wataona huitakii mema CDM; watakuhoji una msingi wa kutaka ivunjwe wakati wapo kina mama ndani ya CDM na wengine ni wabunge. Wapo watakaosema kuwa pendekezo lako lina lengo la kudhoofisha CDM na kuweka hadharani kuwa BAWACHA ivunjwe ni kumpa nguvu adui.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Mimi namuelewa sana Mwanakijiji na ni mmoja wa followers wake wakubwa na amefanya kazi kubwa sana kwa nchi yetu, kwa wale wafuatiliaji wa mambo wanalijuwa hili vyema.

Labda na yeye nimkumbushe kama Mtanzania hii vita tunayopigana ni do or die, wote tunatamani kuona na kuyashuhudia wenyewe mabadiliko yakitokea, lakini vile vile namshauri MM na yeye aplay part yake ili Diasporas nao waruhusiwe kupiga kura huko walipo.

Kinachonisikitisha ni kuona Watanzania wenzetu ambao wanaishi Ughaibuni badala ya kuwa na Jumuiya za Kitanzania zenye nguvu na wawe wameangukia kwenye ulevi wa kufunguwa matawi ya vyama, ndio maana sijawahi kuona ajenda ya Watanzania inayoongea kwa sauti moja kwamba tunataka hiki na serikali inapaswa kuwasikiliza.

All in all sasa ni wakati wa kila mtu kutimiza wajibu, mimi naanza kwa kuishauri Chadema waivunje Bawacha haraka na kufanyike New Reform na watafutwe na kushawishiwa kina mama majasiri wajiune na Chama kuendesha taasisi hizo, nazijuwa vyema fitina za siasa Tanzania bila kuwakamata kina mama bado kazi ngumu sana. sina tatizo na wasichana wengi wao ni waelewa sana hasa wenye elimu ya vyuo ndio hawana shida kabisa.

We umembembeleza sana hapo kwanini na yeye asirudi nyumbani na kuungana na makamanda kulala barabarani waking'atwa na mbu ili aje alalamike vizuri tusipo enda kwa speed anayoitaka? Nini kinamfanya abakie huko nyuma ya key board yake? Mzee wa kijijini rudi kazipige tuone na wewe utadondosha wangapi...Just think hao watu wengine hawana hata ajira za uhakika na maisha yao yako hatarini then you think wanafanya michezo tu kupoteza ushindi? They are trying hard na wana limit zao kama individuals so kwa kidogo wanachotupatie turidhike na tuseme asante unless na ss tujitoelee kama wao tuone inavyo kuwa nzuri kulaumiwa huku umejitoa 100%
 
We umembembeleza sana hapo kwanini na yeye asirudi nyumbani na kuungana na makamanda kulala barabarani waking'atwa na mbu ili aje alalamike vizuri tusipo enda kwa speed anayoitaka? Nini kinamfanya abakie huko nyuma ya key board yake? Mzee wa kijijini rudi kazipige tuone na wewe utadondosha wangapi...Just think hao watu wengine hawana hata ajira za uhakika na maisha yao yako hatarini then you think wanafanya michezo tu kupoteza ushindi? They are trying hard na wana limit zao kama individuals so kwa kidogo wanachotupatie turidhike na tuseme asante unless na ss tujitoelee kama wao tuone inavyo kuwa nzuri kulaumiwa huku umejitoa 100%

imeandikwa kuwa hata kama mtu akitoka ahera na kuja kuwaambia hawatomwamini; wanao Musa na Manabii!!! Hao walio on the ground waendelee sisi wengine tutaendelea kubwabwaja tu kutoka nje. Lakini ukweli wa hoja hautegemei anayesima yuko wapi. Kichaa akisema nyumba yako inaungua haijalishi kama anasema hivyo akiwa kwenye shimo la takataka.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Matola.. ushauri wakko wa kutaka BAWACHA ivunjwe kwa watu wengine wataona huitakii mema CDM; watakuhoji una msingi wa kutaka ivunjwe wakati wapo kina mama ndani ya CDM na wengine ni wabunge. Wapo watakaosema kuwa pendekezo lako lina lengo la kudhoofisha CDM na kuweka hadharani kuwa BAWACHA ivunjwe ni kumpa nguvu adui.
Hakuna Ubishi kwamba Chadema uwepo wa Bavicha unaonekana dhahiri na wanapiga kazi ya ukweli na hapa Wasichana na hasa Wasichana wasomi wote wapo humu.

Bawacha inahitaji Mindset mpya, kamati kuu ya Chadema inapaswa kuanza mazungumzo nz wanaharakati wenye nguvu mfano wa Ananilea Nkya ili waje kukabidhiwa jukumu la kuiongoza Bawacha, hii siyo taasisi ya Wabunge wa Viti Maalum ambao wameshaiuwa na haipo, huo ndio ukweli.

Wanaharakati wanaruhusiwa kujiunga na vyama vya kisiasa ni kwa nini wasitafutwe wale ambao wako strong na wakashawishiwa kuijenga jumuiya hii? au ni kwa nini basi baadhi ya wabunge kama kweli wanayosifa hii ya kuwa viongozi wa Bawacha basi wajiandae kufanya kazi hii na ubunge uwe ni part time kwao na 2015 wasigombee kabisa ili kujenga The heart of Chadema. Sijui kama naeleweka hapa.....
 
Personally sijawahi wala sina mpango wa kuwa na kadi ya chama chochote cha siasa unless for personal benefits only. Mara yangu ya kwanza kupiga kura ni mwaka 2000 nilipofikisha umri wa kupiga kura. Mara zote hizo nimekua napigia kura Chadema wagombea wote ispokuwa 2000 ambapo hakuwepo mgombea urais tu. Napiga kura kwa dhamira yangu binafsi si kwa vile tu ni mwanachama. Kwetu sisi wote ni wapiga kura wa Chadema ambao hatujawahi kuwa na kadi ya uanachama. Kuwa na kadi siyo kipimo tosha, cha msingi ambacho Chadema inahitaji kwangu siyo just kuwa mwanachama bali ni kura yangu.
 
imeandikwa kuwa hata kama mtu akitoka ahera na kuja kuwaambia hawatomwamini; wanao Musa na Manabii!!! Hao walio on the ground waendelee sisi wengine tutaendelea kubwabwaja tu kutoka nje. Lakini ukweli wa hoja hautegemei anayesima yuko wapi. Kichaa akisema nyumba yako inaungua haijalishi kama anasema hivyo akiwa kwenye shimo la takataka.

Salute!
 
Tatizo kubwa ni kwamba Chadema huwa wana-copy na ku-paste wanachofanya CCM. Kadi zinagawiwa kama pipi na ktupwa kama maganda ya pipi.

kuhama+chama1.JPG


kuhama+chama+4.jpg


kuhama+chama+5.JPG


Kuweka agenda ya kupokea wanachama wapya katika mikutano ya hadhara ni matumizi mabaya ya muda na ruzuku. Bora kadi zingerejeshwa na kutolewa kwenye matawi ya vyama. Ni ufinyu wa uelewa wa demokrasia na kushindwa kuthubutu. Matokeo yake vyama vinaishia kuwa na mamluki.
 
Sikubaliani na wewe kwenye hoja hii, CCM huwa wanaprint kadi za Chadema na kuwagawia watu wao ili kuuhadaa umma kwamba kuna watu huwa wanarudisha kadi, swali la kujiuliza mbona hakuna wanachama wa Tadea wanaorudisha kadi zao na kujiunga na CCM? Hizi ni propaganda nyepesi na zinafikia ukingoni.
Tatizo kubwa ni kwamba Chadema huwa wana-copy na ku-paste wanachofanya CCM. Kadi zinagawiwa kama pipi na ktupwa kama maganda ya pipi.

Kuweka agenda ya kupokea wanachama wapya katika mikutano ya hadhara ni matumizi mabaya ya muda na ruzuku. Bora kadi zingerejeshwa na kutolewa kwenye matawi ya vyama. Ni ufinyu wa uelewa wa demokrasia na kushindwa kuthubutu. Matokeo yake vyama vinaishia kuwa na mamluki.
 
Wanaharakati wanaruhusiwa kujiunga na vyama vya kisiasa ni kwa nini wasitafutwe wale ambao wako strong na wakashawishiwa kuijenga jumuiya hii? au ni kwa nini basi baadhi ya wabunge kama kweli wanayosifa hii ya kuwa viongozi wa Bawacha basi wajiandae kufanya kazi hii na ubunge uwe ni part time kwao na 2015 wasigombee kabisa ili kujenga The heart of Chadema. Sijui kama naeleweka hapa.....

nani aanzishe mpango huu? wewe ndugu yangu kuwashauri hili ni kujaribu kuwafanya waonekane wao hawana mawazo kama haya na kwa kweli inakuwa ni sawana kuisaidia CCM. Watu wengine hawawezi kuona hili unalopendekeza ni jema kwa sababu kalitoa Matola hata kama lina mantiki.
 
Sikubaliani na wewe kwenye hoja hii, CCM huwa wanaprint kadi za Chadema na kuwagawia watu wao ili kuuhadaa umma kwamba kuna watu huwa wanarudisha kadi, swali la kujiuliza mbona hakuna wanachama wa Tadea wanaorudisha kadi zao na kujiunga na CCM? Hizi ni propaganda nyepesi na zinafikia ukingoni.

Na Chadema inalijua hili? Chadema wamechukua hatua gani? Kama kadi zao zinafekiwa na wao wanakaa kimya si keundeleza ufeki wenyewe?

CCM wanajua utaratibu wa Chadema kutoa kadi kwa wanachama wapya na kumonitor existing members siyo mzuri kwa hiyo wanaweza ku-print kadi feki na wanachama wapya feki pia.

Chadema haina robust system ya kuhakiki wanachama wake, let alone watu ambao watawapigia kura zaidi ya kugeneralise kwenye majukwaa tuu.

Siku hizi kuna mpaka teknologia ya ku-computerize hizo kadi badala kutengeneza kama kadi za harusi vile. Hata mie naweza kufeki hizo kadi za chadema na kuziuza mtaani na pesa nikatia ndani.

Ni bora kuwa kuwa wanachama 10 lakini ni wa ukweli kuliko wanachama 100 ambao huna uhakika nao.
 
Na Chadema inalijua hili? Chadema wamechukua hatua gani? Kama kadi zao zinafekiwa na wao wanakaa kimya si keundeleza ufeki wenyewe?

CCM wanajua utaratibu wa Chadema kutoa kadi kwa wanachama wapya na kumonitor existing members siyo mzuri kwa hiyo wanaweza ku-print kadi feki na wanachama wapya feki pia.

Chadema haina robust system ya kuhakiki wanachama wake, let alone watu ambao watawapigia kura zaidi ya kugeneralise kwenye majukwaa tuu.


hii hoja nayo haina mashiko; kama CCM wananunua kadi kuna namna nyingi za kuweza kucounter hili. Mara nyingi tunaambiwa CDM inawasomi wengi; ni kweli wasomi wetu walioko CDM wameshindwa kufikiria namna ya kushughulikia hili? Lakini inakuwaje kama ni kweli wapo wanaCDM wanaorudisha kadi zao kirahisi hivyo? Ni kitu gani kinawafanya watu warudishe kadi? Kama wapo mamia ya wana CCM wanahamia CDM na kuleta kadi zao kwa CDM haiwezekani kweli kuwa wapo pia wana CDM kwa mamia ambao na wanarudisha kadi zao kwa CCM? Kwanini iwe kweli kwa CCM lakini isiwe kweli kwa CDM?

Hatari ya hili ni kuwa vyama havikui idadi kwa sababu namba zao zina cancel each other each time
 
  • Thanks
Reactions: EMT
hii hoja nayo haina mashiko; kama CCM wananunua kadi kuna namna nyingi za kuweza kucounter hili. Mara nyingi tunaambiwa CDM inawasomi wengi; ni kweli wasomi wetu walioko CDM wameshindwa kufikiria namna ya kushughulikia hili? Lakini inakuwaje kama ni kweli wapo wanaCDM wanaorudisha kadi zao kirahisi hivyo? Ni kitu gani kinawafanya watu warudishe kadi? Kama wapo mamia ya wana CCM wanahamia CDM na kuleta kadi zao kwa CDM haiwezekani kweli kuwa wapo pia wana CDM kwa mamia ambao na wanarudisha kadi zao kwa CCM? Kwanini iwe kweli kwa CCM lakini isiwe kweli kwa CDM?

Hatari ya hili ni kuwa vyama havikui idadi kwa sababu namba zao zina cancel each other each time

Hoja yangu au ya Matola haina mshiko? Kama mdau mmoja alivyowahi kuuliza haya maswali:

Kwa nini kadi hizo zisirudishwe kwa vyama husika katika matawi yao ili waweze kuhakiki wananchama wao?

Vyama vya siasa vinahakiki vipi wanachama wake?

Kwa nini mikutano mingi ya hadhara ya vyama vya siasa agenda kubwa ni kuwapokea wanachama wapya?

Kazi ya idara ya uenezi ya chama ni nini? Idara hii kichama kwa jinsi vyama vinavyofanya kazi hivi sasa ina mapungufu gani?

Viongozi ambao walikuwa na dhamana wanapohamia vyama vingine tunajifunza nini? Wanakuwa wamekosa nini? Kuhamia chama kingine ni suluhisho?

Ni vigumu kuelewa pamoja na vyama vya siasa kumiliki wataalamu wa uchambuzi wa mambo ya siasa na uchumi, bado wameshindwa kutumia taaluma yao kuwashauri vyama vyao kuweka agenda ya kuwapokea na wanachama wapya katika mikutano yao ya siasa ni matumizi mabaya ya muda na fedha.

Kubwa zaidi ni kutafuta umaarufu wa kichama tuu. Kuna uhakika gani kama wanachama hao siyo wanachama wa chama hicho hicho? Je hao wanaorudisha hizo kadi sio mamluki wa kisiasa ambao kwa upeo na uelewa wa ukuaji wa demokrasia ndani ya vyama wanasiasa wanafikiri kuwa matukio kama haya yanawaongeza wananchama kumbe wanongeza kero ndani ya vyama vyao kwa kuwapata wananchama wa msimu ambao wengi wao huishia kuwa mamluki wa kisiasa wanaohama tuko chama kimoja kwenda kingine?

Kesho wakisikia CUF wako Jangwani watarudisha hizo kadi na kuingia CUF. Keshokutwa ikirudi CDM watarudisha za CUF na CCM na kuingia CDM. Na CCM wakirudi tena kufanya mkutano watarudisha hizo kadi na kuchukua za CCM.

Vyama vya siasa hata CCM wana tatizo la kutojua idadi ya wanachama wao ambao ni hai na ambao wanaweza kukisaidia chama katika kukiletea maendeleo na kukipigia kura wakati wa uchaguzi. vyama vinapumbazwa na halaiki ya watu wakati wa mikutano yao ya wazi.

Siasa ni zaidi ya ushabiki wa mpira. Siasa safi na zenye tija ndizo zitakazowezesha taifa hili kusonga mbele.
 
Back
Top Bottom