Mkuu Tumaini Makene, asante kwa taarifa hii kuhusu Chadema na viongozi wake katika suala zima la kupokea ushauri, ushauri siku zote huwa ni ushauri tuu, mshauriwa ana hiyari aupokee au kuupuuza.
Kwa vile sote tuko humu jf, sisi wengine hatuna vyama, mazuri tutapongeza, madudu tutakemea, na kwenye ushauri tutatao, its up to Chadema to take it or leave it, ila kuna sisi wengine hatupendagi makelele ya watu kuja kutulilia humu kila baada ya miaka mitano!, ndio maana sisi wengine tunashauri, na tukiisha puuzwa, wakati wa kuleta vilio humu vya November, 2015, sio tuu tutawakumbusha tuliwashauri nini, bali badala ya kuwapa pole kwa vilio, tutawazomea tukiamini hayo ndio mliyoyataka!.
Asante.
Pasco.