CECAFA Senior Challenge: Kutoka Uganda

CECAFA Senior Challenge: Kutoka Uganda

Hakuna kosa alichofanya Juma K Juma Mabeki nao wanacheza Foul za mchangani wanaona kurusha miguu ya kifua ndio mpira na Rebound hakuna hata mchezaji mmoja wa Kilimanjaro aliyewavamia Cranes japo najaribu kumtetea Juma Kasseja naye ni muda kuweka Gloves chini awapishe wengine.
Mkuu.......Siku zote kwenye football kipa akitema mpira na mshambuliaji wa timu pinzani akifunga huwa ni kosa la KIPA.....Kaseja amefanya kosa alilofanya Jean Claude Ndoli wa Rwanda juzi walivyocheza na Stars.......

Yondani kacheza fou
l nje kabisa ya 18 na aicheza wakati yeye na Chuji wakijaribu kumzuia Ssentongo asiete madhara na wangemuacha ingekuwa ni madhara......

Tukuba
li tu kwamba timu nzima imeteleza leo
 
Tanzania Bara ndomana hatufiki mbali tunapenda kulalamikiana na kuuweka lawama kutoka timu ya Taifa kuziingiza vilabu havihusu vilabu hapa na ikirudi timu ya Taifa ya Tanzania tukumbuke kuweka timu sio kwa Vilabu vya Dar-es-salaam tu waweke Vilabu vya Mikoa mengine na Wachezaji wa Visiwani wengi wazuri tu. Kaseja lile sio kosa lake ila ni muda aweke Gloves chini na tuache kuingiza vilabu hapa ndomana wengine wanaishia hawashangilii vilabu tena vya Tanzania na kubakia kutizama timu ya Taifa japo Kilimanjaro wanafanya uozo Zanzibar walicheza vizuri. Pia tukumbuke hili fundisho tutajifunza.
 
tusubiri tu mechi ya keshokutwa tucheze huku tukijadili katiba mpya
 
... Namkumbuka mbrazil Maxmo. "TUTAJIPANGA UPYA" Tanzania kila mwaka tunajipanga tunajipanga upya!
 
rafu ya kizembe sana imechezwa na Tanzania, Kaseja kadaka na kuutema mpira, waganda wanashambulia hapa kama watatu hivo,,,,ni goli!!Ssentongo tena!!-UG 3 vs TZ O
TZ tuna mpira wa magazetini once again live pumba zetu zinaonekana. Sijawahi kuiamini bongo ktk mpira wa miguu. Wanacheza ovyo tu msisubiri kushinda kikombe na timu hii ovyo. RIP TZ wanajisemea waganda
 
Dakika ya 85

Tanzania 0-3 Uganda

Ngassa anakabwa na watu wanne

Umeme umekatika uwanjani
 
Taa zina zima uwanjani...naona Tanesco wameenda hadi Uganda ili walau tufanye juju kidogo magoli yarudi...
 
Back
Top Bottom