CECAFA Kagame Cup 2012 - Live updates

CECAFA Kagame Cup 2012 - Live updates

Mimi huyu kocha amenishangaza sana,amelalamikia goli walilofungwa akidai kuwa wachezaji walikuwa wakigombana nje alafu refa akaruhusu mpira urushwe na hatimae Yanga kujipatia goli la kuongoza dakika ya 100. Pili,huyu kocha amelalamikia kitendo cha mchezaji kutibiwa kwa dakika 6 uwanjani,nadhani alitafsiri kuwa ulikuwa ni upotezaji wa muda. Sasa hapa cha ajabu ni kwamba,kwa nini alilalamika kwa msisitizo kuwa "THIS IS AFRICA...",je,alimaanisha Africa hakuna waamuzi wenye akili au wachezaji pia hawana uwezo wa kutosha na ndio sababu ya wao kujidai wameumia mara kwa mara ili kupoteza muda?
Pia nikajiuliza,kama huyu kocha amefikia kuidharau Afrika,sasa anafanya nini huku,si aende Ulaya au mabara mengine akafundishe soka?
Ndo hayo tu niliya-note leo baada ya mecì kati ya APR FC VS YANGA FC.
Yule mzungu ni kama mfa maji,haishi kutapatapa. Kwani wao APR kwanini walishindwa kutumia fursa ya red card waliyopata Yanga wakashinda?
 
Yule mzungu ni kama mfa maji,haishi kutapatapa. Kwani wao APR kwanini walishindwa kutumia fursa ya red card waliyopata Yanga wakashinda?

Habari za kuaminika zilizopatikana kupitia Wanyarwanda waliokuwa wakisafiri kutoka Dar kwenda Kigali kwa kutumia magari ya 'IT' asubuhi siku ya mechi hii zinaeleza kuwa Mhe. Kagame aliwaagiza APR warudi na kombe la CECAFA kwa vile amekuwa akitoa fedha nyingi huku akinufaisha timu ngeni, alitishia kusitisha ufadhili kwa APR endapo wangeshindwa kuchukua kombe hili.

Sasa wametolewa katika kinyang'anyiro cha ubingwa, hali itakuwaje? Pengine huyu mzungu alipotafakari yote haya alifahamu fika kuwa kibarua kimefikia ukomo.
 
Simba.jpg

Mmoja wa viongozi wa juu wa nchi hii alitoa hotuba ifuatayo:

'UKIMWI ni janga la kitaifa, kila mtu anajua jinsi ugonjwa huu unavyoambukizwa. Watu hupanga siku, muda na mahali pakufanya vitendo vinavyosababisha UKIMWI ..., wapo watu ambao umri wao hauwaruhusu kujihusisha na vitendo hivyo mfano wasichana wadogo na ambao ni wanafunzi, hawa kujihusisha kwao na vitendo hivi ni KIHEREHERE tu ...'

Kabinti kama ka Ms. Azam, FC (Kuzaliwa 2007) kutembea na mibabu kama Mny. Simba, SC (Kuzaliwa 1936) na Bw. Yanga, SC (Kuzaliwa 1935) sio KIHEREHERE?

Hata hivyo kabinti kenyewe kanaonekana kuwa na mkosi maana Mny. Simba, SC kamamemwangusha, hakika asiyejua kufa atazame kaburi, bila shaka Mny. Simba, SC alikutana na 'Brain concurssion' (Tazama picha hapo juu).

Haijafahamika leo itakuwaje kwa Bw. Yanga, SC.
 
wakuu naona mechi ya APR imewai sasa dak. Ya 88 APR 1-2 Vita club. Je na ya Yanga itawai.?
 
wakuu naona mechi ya APR imewai sasa dak. Ya 88 APR 1-2 Vita club. Je na ya Yanga itawai.?
Ni muda ule ule saa 10, walifikiri APR na VITA wataenda dk.30 zaidi na baadae Penalt ndo maana mechi imeanza mapema.
 
Yule mzungu ni kama mfa maji,haishi kutapatapa. Kwani wao APR kwanini walishindwa kutumia fursa ya red card waliyopata Yanga wakashinda?

Sijui Mzungu wa wapi yule,eti ooh goli lilifungwa katika mazingira tatanishi,kwanini team yake na yenyewe haikufunga goli katika mazingira tatanishi basi iwe 1-1,tuingie kwenye penalt?
 
Waleteni waleteni hao Azam,koo linaniwasha kushangilia ile mbaya
 
Sijui Mzungu wa wapi yule,eti ooh goli lilifungwa katika mazingira tatanishi,kwanini team yake na yenyewe haikufunga goli katika mazingira tatanishi basi iwe 1-1,tuingie kwenye penalt?

Penalt na kipa mwenyewe Baltez??? ingekuwa mwisho wa safari
 
Waleteni waleteni hao Azam,koo linaniwasha kushangilia ile mbaya
Dahhhhh!natamani nami ningekua japo nachungulia kwenye kioo,anyway najua jf ni zaidi ya kideo,so sisi tulio mbali tutayapata matokeo hapa ndani!
 
Penalt na kipa mwenyewe Baltez??? ingekuwa mwisho wa safari

Ahaa PrN kumbe upo enh....very nice,umeniona leo nawakilisha from the begining....ni dalili za uhakika kwamba baada ya dk 90+5/120 au maguu kumi na mawili ya mtu mzima ni kicheko tu
 
PrN,Bemg na Skype najua mtaishia kimyakimya humu ndani hata kuaga hamtaaga
 
Back
Top Bottom