figganigga
Platinum Member
- Oct 17, 2010
- 26,691
- 59,193
mwanaume akiguna jua amekili kosa. Kumbe kweli kang'atuka!. Asante nape. mia
Nape,
Kinana anaweza kutumia maneno yoyote yale kuhakikisha kuwa haeleweki vibaya. Nia yake moyoni haiwezi kuwa reflected na maneno, ni yeye mwenyewe anafahamu kwanini ameng'atuka.
Kama ilikuwa ni kupokezana vijiti basi angetoa kijiti hicho kati ya 10-15, lakini anaposubiri robo ya karne inatia shaka sana.
Kwa kuliangalia jambo hili kisiasa, ukweli ni kuwa Kinana ameamua kuungana na wazee wengine kukaa pembeni ili kulinda legacy yao. Ni wazi kuwa chama kipo katika hali na wakati mgumu sana kisiasa na watu waliojenga heshima zao wasingependa kuwa sehemu ya 'kamati' za kuandaa maziko ya chama. Huu ni ukweli usiohitaji fikra nawe unaufahamu.
Kwa upande wa pili, inaweza kuwa amejiuzulu kugombea akijua kuwa kuna mahali patamrudisha katika kamati hiyo.
Mathalani, akipewa ukatibu mkuu basi anaingia kwa kofia hiyo. Kuna mchezo unachezwa hapa, guess what, Tanzania ya leo si ya jana. Time will tell!
Mbona hili mmefanya mapema hivi kuja kukanusha?! I can sense the sign of RED FLAG! Nafahamu wazi kwamba udhaifu mkubwa wa CCM ni ama kupuuza moja kwa moja au kuchelewa kuchukua hatua za kujibu tuhuma mbalimbali dhidi ya chama hususani zinazotolewa hapa JF! Au ndo tuseme Idara ya Uenezi imezaliwa upya na kwa kasi mpya?! Hata hivyo msisahau kwamba, mashahidi wa tuhuma za Richmond, including Dr. Msabaha ndani ya kiapo alisema vingine na nje ya kiapo "akawang'ata sikio" kwamba mzigo ni wa bwana mkubwa na yeye anatolewa kafara tu....so, inawezekana kabisa Kinana kwenye barua ameandika kwamba anang'atuka kupisha damu changa na nje ya barua akawang'ata watu sikio kwamba hawezi kuendelea na siasa uchwara!
Mkuu Mwita Maranya ishu iliyoko ubaoni ni kujiuzulu kwa Kinana. Wewe kama una yako na Ndungulile fungulia thread tutachangia....dr f.ndungulile ni mapema sana kumshukuru Nnauye Jr kwa madai ya kuweka kumbukumbu sawa kwani hajaainisha chanzo cha hayo maneno anayodai ni ya Kinana.
Hata hivyo Kinana atakuwa amewahi kusoma alama za nyakati hataki jumba bovu lianguke nae akiwemo. Wewe tu ndio bado umeshindwa kufanya maamuzi magumu pamoja na kuzibwa mdomo na chama chako cha ccm, mbunge uliyechaguliwa na wananchi unazuiwa kufanya mikutano na wewe umeridhika kama vile mambo yako shwari!
Kama kumbukumbu zangu zipo sawa ni kwamba Kinana alikuwa anawachana akina Lowassa live ndani ya vikao.....hilo la ufisadi wa Kinana nafahamu limeshwahi kuibuka hapa JF!Mkuu NasDaz you cant be seriou my friend. Kinana huyu huyu tunayemfahamu anapambana na ufisadi/mafisadi? Mara hii umeshasahau lundo la tuhuma zake za rushwa, ufisadi na uharamia wake? Zipo thread nyingi tu hapa ukizitafuta utazipata zimeweka wazi kila kitu.
Mbona kanusho limetoka haraka hivi? hiyo moja; Pili wapi barua kamili ya kung'atuka? Tatu mbona ile thread hadi sasa iko hewani?.................najaribu kuunganisha mambo
dr f.ndungulile ni mapema sana kumshukuru Nnauye Jr kwa madai ya kuweka kumbukumbu sawa kwani hajaainisha chanzo cha hayo maneno anayodai ni ya Kinana.
Hata hivyo Kinana atakuwa amewahi kusoma alama za nyakati hataki jumba bovu lianguke nae akiwemo. Wewe tu ndio bado umeshindwa kufanya maamuzi magumu pamoja na kuzibwa mdomo na chama chako cha ccm, mbunge uliyechaguliwa na wananchi unazuiwa kufanya mikutano na wewe umeridhika kama vile mambo yako shwari!
Kuhusu kujiudhuru sijui kungatuka kwa kinana bila kufata la nape wala la wanaosema siasa uchwara.
Kama wewe ni greatthinker utajiuliza hivi
Ni juzi tu alikuwa manager wa kampeni, alifungua tawi USA huko, alikuwepo kwenye team ya usuluhishi kwa makundi yasiyopatana CCM, na bado ana umri mzuri tuu kuendesha siasa ukilinganisha historia ya viongozi wengi wa CCM...sasa jiulize why yeye???? na kwanini kwa muda huu? then utapata jibu na kujua mchele ni upi kati ya nape na wanaodai ni siasa uchwara.