CCM yanguruma Busanda; Wapinzani chali!

That is the sprit, lakini isiwe ni kwenye media kuwa kuna makosa madogo yatalekebishwa, kwani kama hamkurekebisha you will never get majombo mengine zaidi ya haya mliyonayo, naogopa mtawekewa mamruki na kusambaratisha chama chenu kabla hamjafikia kiwango kinachotakiwa cha ushindi.

Hii inanikumbusha watu kama Lamwai now in CCM who was a real threat to CCM na sio kama kina Marando walivyosambaratishwa na kuamua kurudi CCM wenyewe bila kupenda.

Hii inanitia mashaka kama kweli watanzania wako serious wanataka kuondoa umasikini au wanataka uendelee, suala la msingi hapa ni kuongeza idadi ya wabunge mjengoni ili walete changamoto kwa wabunge wa CCM waongee mambo ya msingi badala ya blah blah kila siku.
 
Busara na elimu bado i nahitajika, heri ya busanda japo makao makuu wameibuka na upinzani, japo sijawa updated, inakuwaje Dar, jijini majimbo yote yalienda CCM?
 
Duh!!!
Kama dola imeshikwa kihivyo. je tunapata ujumbe gani hapo????

Nilisema tangu awali kwamba kama ikishindikana kupata katiba mpya inayokwenda na wakati basi kazi kubwa ielekezwe kuelimisha jamii kuhusu haki za kimsingi. hata polisi nao ni jamii ni budi waelimishwe wajue wapo ktk mstari upi wasije wakajilaumu huko mbeleni.
 
Kujaza watu katika kampeni si kipimo cha ushindi.
Wengine walikuwa ni mashabiki tu ambao wala hawakujiandikisha, wengine ambao hawakupiga kura ni wale waliouza shahada zao au wanawake waliozuiliwa na waume zao kama tulivyojuzwa. Upinzani bado haujakomaa vijijini na wala wasitafute mchawi.
 

hapo tupo ukurasa mmoja Mkuu
 

Acha Porojo Ndugu yangu na ni kosa kubwa sana kuwadharau watu zaidi ya 22,000 waliopigia kura na kuwaita ni vijana wa Kijiweni wewe wa ofisini unafanya umefanya nini , nyinyi ndio wale ambao huwa mnaogopa hata kuhudhuria mikutano ya vyama vya upinzani eti kuogopa vibarua vyenu ( Shame on you) CHADEMA, 2005 CHADEMA got only 4% sasa wakuu wamepata zaidi ya 40% bado huoni kama kuna Juhudi? CHADEMA should stand as CHADEMA suala la kuunda Ushirika na vyama Muflisi ni Kujimaliza
 
Busara na elimu bado i nahitajika, heri ya busanda japo makao makuu wameibuka na upinzani, japo sijawa updated, inakuwaje Dar, jijini majimbo yote yalienda CCM?

Mjini bwana pako tofauti sana,wananchi wengi hasa wa DAr wanataka DAR iendelee hivyo ilivyo ile waedelee kula shushu..Hivyo ndiyo maana CCM inaendele kushinda!

Wananchi wengi ni zao la mafisadi hasa mijini ..sasa lazima walinde chakula cha wajomba zao na mababa zao."Mabuzi" yao yaweze kushinda si unajua siasa ya Tanzania ...hauwezi kuwa mwanasiasa bongo mpaka uwe mtu wa totoz na kilaji..Nyani Ngabu unasemaje hapo?Hata mawaziri na viongozi wengine hulipwa fadhila baada ya kuunganishiana wanawake..!
 

Sababu kama hizi huwa tunazipata pindi timu zetu za mpira zikienda kucheza nje na kufungwa, watanzania hatujambo kwa kutafuta maelezo ya kuhalalisha failure. Jamani tukubali ushindi huu na mwingine wowote wa CCM unapangwa na hao wapinzani, tena wananchi wanapoonesha nia ya kuin'goa CCM wao wanatafuta njia zote za kuibakisha (ushahidi tumeuona Busanda).
 

CUF ndio walipata kura wa pili baada ya CCM kwenye uchaguzi wa 2005. Ila nahisi strategy ya Chadema ni kuwa chama kikuu cha upinzani kwa CCM, ndio maana haikutaka kuwaacha watu wake kaunge mkono yule wa CUF, labda angepata angewakilisha vizuri hivyo Chadema wangelipoteza jumla. It's not fine, but it's understandable.
Kwa mtindo huo tusishangae huko Biharamulo wote Chadema, CUF, TLP na hata UDP wakaweka wagombea, na jimbo likarudi CCM.
 

Hizi namba za matokeo zinanifurahisha jinsi zinavyoishia na 49 na 27.

Hapa kwenye idadi ya waliojitokeza ni fundisho kwa wote walioshiriki uchaguzi kuwa voter turn out katika chaguzi zetu ndio determining factor ya nani atashinda kati ya wale wanaochuana kwa karibu. Ina maana hapo iwapo CHADEMA ingeweza kuwahamasisha wapiga kura wengine elfu 9 kati ya 80,280 wasiojitokeza wangeibuka washindi. Kuna sayansi ya uchaguzi ambayo inabidi vyama vya upinzani wajifunze.vitu vidogovidogo sana wanashindwa kufigure out.
 
Hamtaamini lakini ndiyo ukweli, poleni sana. Ni vizuri tu wakawa waungwana kama yule jamaa wa Magogoni kwa kukubali ukweli. Haina maana kuleta zogo na kutunga uongo. Hata mkinuna UKWELI NDIYO HUO !!!!!!!
 
Hakuna kulala vyama vya upinzani visikate tamaa kwa matokea haya kwani bado wananchi wanaitaji muda kuweza kuelewa nini kinaendelea na ukichukulia watu wengi waliopiga kura shule yao ni ndogo hivyo wanaitaji kuendelea kutembelewa kwa kufanya mikutano ya mara kwa mara uko mikoani.Hiyo inaweza kusaidia. Pia inabidi hivi vyama viwe na matawi vijijini though yapo lakini ni machache.

MAPAMBANO YAENDELEE HAKUNA KURUDI NYUMA
 
CHAMA CHA MAFISADI NI MAFIA SANA. WANAOIBA KURA HUWEZI KUWAZANIA kama hao mawaziri wamekutwa na hizo shahada ni uthibitisho tosha kabisa
 

I salute you SIR!!! Naomba nikupongeze kwa juhudi zenu za kui chalenge CCM. Hata bila kuwin kiti bado impact yenu kwa maisha ya wana Busanda ni kubwa. Mtaji wenu mwakani utakuwa utekelezaji mbovu wa ahadi za CCM na hapo hiyo difference za kura elfu saba ni ndogo mno kuzi win compared na muda uliobaki wa CCM kutekeleza walichokiahidi. Usife moyo shujaa wa kweli ni yule mwenye makovu mengi mgogoni na reward yake ni ile facial expression after winning the battle. So keep it up na hongera kwa kukubali kushindwa.
 
CHADEMA should stand in Biharamulo, Achaneni na Hizi Porojo za akina Mrema na wenzake! Kwa nini mara zote linapokuja sula la Ushirika Chadema ndio anaonekana yuko Obliged kupanda jukwaani kupigia kampeni chama kingine!
 

Good Observation mkuu, Bila Chadema hata hizo Nguzo za Umeme zisingepelekwa huko Busanda.
 
Lazima tufike sehemu tukubali kuwa uwanja siyo even kwa vyama kwani ccm imechukua raslimali za wananchi na kuzifanya zao. Hivyo inatakiwa wanyang'anywe. Harafu kuwepo na utaratibu wa kuonyesha hela za kampeni zinatoka wapi kwani tumeona wakina obama walikuwa wanasema wazi na matumizi yao yanafuatiliwa. Then from there tutakuwa tumepata pa kuanzia. Lakini kwa muendelezo huu tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu itachukua muda sana mabadiliko kutokea.
 
I fully agree with you Ndege ya uchumi...CHADEMA should stand on its own and prove to be the main opposition party to CCM.
 

Ndugu yangu hapo ndipo huwa nafikia maamuzi kuwa hawa watu tuliowapa jukumu la ukumbozi wa wanyonge wa nchi hii wanatuhujumu. Suala la voters turn out limekuwa likijitokeza kila mara kwenye hizi chaguzi(wasituambie wamesahau) lakini hakuna anayeonesha kujali. Na matokeo kama haya wanawavunja nguvu hata hao wachache wa hapo Busanda na wengine nchi nzima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…