wasaidizi wa Rais akiwemo Ridhiwani Kikwete na January Makamba sio! Hii nchi imekwisha iko siku watampelekea Kikwete list ya kunyonga toka mahakamani halafu wadai amedanganganywa!Katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi (CCM) Yusuph Makamba ,amesema kama aliyeenguliwa kugombea ubunge jimbo la Nzega na chama hicho Hussein Bashe,ni raia halali wa Tanzania basi anayestahili kubebeshwa lawama ni wasaidizi wa JK na si chama hicho
Akizungumza na Nipashe jijini dar es salaam jana,Makamba alisema chama chake kilipata Vielelezo kwamba Bashe si raia kutoka kwa wasaidizi wa Rais hivyo CCM haistahili lawama
'' Wasaidizi wa Rais ndiyo walituambia sisi kuwa Bashe si Raia sasa kama wizara ya mambo inasema ni raia basi ituambie ,lakini leo tunaendelea kuamini tulichoambiwa na wasaidizi wa rais''
Source Nipashe
Katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi (CCM) Yusuph Makamba ,amesema kama aliyeenguliwa kugombea ubunge jimbo la Nzega na chama hicho Hussein Bashe,ni raia halali wa Tanzania basi anayestahili kubebeshwa lawama ni wasaidizi wa JK na si chama hicho
Akizungumza na Nipashe jijini dar es salaam jana,Makamba alisema chama chake kilipata Vielelezo kwamba Bashe si raia kutoka kwa wasaidizi wa Rais hivyo CCM haistahili lawama
'' Wasaidizi wa Rais ndiyo walituambia sisi kuwa Bashe si Raia sasa kama wizara ya mambo inasema ni raia basi ituambie ,lakini leo tunaendelea kuamini tulichoambiwa na wasaidizi wa rais''
Source Nipashe
Pumbavu walishindwa cross check na jamaa wa uhamiaji instantly?
Nijuavyo kufanya uamuzi waitaji atleast 3 sources sasa wakarely on one source.
Ngoja niishie apo nsije tukana bure
atokee chizi mmoja awapige risasi hawa viongozi wabovu''top'' tuanze upya la sivyo hakuna mabadiliko Tz.
Mzee Makamba majibu yake yanaonyesha msuguano mkali kati ya Ikulu na wizara husika.Raisi ni kiogonzi wa serikali na chama tawala CCM.Kwa maana wasaidizi wake wa Ikulu,Wizara ya Mambo ya Ndani,CCM,wako kwenye anga yake.Alishidwa vipi kutenganisha pumba na mchele wakati ndio ameshika usukani?Hiyo sintojua itawaghalimu CCM kwenye uchanguzi mkuu.
Jamani jamani jamani, maigizo maigizo maigizo!Hamna lolote walishapanga kumkandamiza Bashe siku zote hizo hawakujua kuwa Bashe hakuwa na URAIA mpaka ashinde kura za maoni..?
Hii yote inatokana na MAJUNGU na VISASI vya Ridhwan, Ridhwan na Bashe walipisha maneno sasa Ridhwan kushirikiana na SAWAHIBA wake wakaa mua kumuandalia ZENGWE la URAIa Bashe wakapeleka majungu kwa Baba ambae ni Rais na Mwenyekiti wa Chama tawala CCM na Rais bila kufuatilia na kupata uhaki anaamua kuwa Bashe sio RAIA, sasa wanakujaje na kusema kuwa ni RAIA..? CCM ni kijiwe cha MAJUNGU na FITINA ni ukiwaambia ukweli wanakuambia kuwa sio RAIS, mfani Jenerali Ulimwengu aliambiwa kuwa sio rai, juzo Mhe Mstapha Mkullo nae aliambiwa kuwa sio rai sasa miaka mitano yote mtu anakuwa wziri tena kwenye wizara nyeti ya Fedha na Uchumi leo unakuja kusema sio raia.
Mimi nataka kumpa USHAURI wa Bure kijana Ridhwan wewe ni WAKILI aende akawe WAKILI na ndicho alichosomea na ujiweekee mazingira mazuri ya kuishi baada ya 2015 na wala sio mabali amebakiasha MIAKA 5 ya kupika majungu baada ya hapo ataiona CCM ni chungu maana Baba atakuwa Msoga anapumzika na Makamba nae Bumbuli anapumzika hakuwa wa kumtetea na tabia MAJUNGU haimfai unashindwa kumalizana na mwanaume mwenzi unaenda kupika majungu na kumpelekea Baba ili iweje sasa FAIDA gani sasa ameipata?? Aibu tupu
mkuu natofautiana na wewe maana albam mpya ndio inavuma. kwa hiyo kingwangala a.k.a saidi bagaile alitakiwa kuvuma kama santuri mpyaJethro,
Hilo la Makamba kali sana, bora afumbe kinywa chake.
Kuhusu kuchukua mtu wa tatu nafikiri maelezo ya CCM yana make sense. Wewe ulikuwa mbunge miaka mingi, wananchi wako wamekukataa
kwa kura nyingi sana, hii ni ishara hukubaliki, hivyo bora kuchukua mtu mpya. Walifanya hivyo hivyo hata Njombe kule kwa Nyimbo.
Ila nimeshangaa kwanini hawakufanya hivyo kule Iringa? Yule mama naye wangemtema.