OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,199
- 103,733
Katibu Mkuu wa BAVICHA Nusrat Hanje na mratibu wa uhamasishaji taifa Twaha Mwaipaya wapo gerezani yapata mwezi sasa kwa kile kinachodaiwa kuuharibu wimbo wa taifa kwa kusema "Mungu ibariki Chadema, wabariki viongozi wake". Msajili wa vyama vya siasa Jaji Mutungi nae kakipa onyo Chadema kwamba jana wakati wa ufunguzi wa Baraza kuu, wanachama waliongeza ubeti wa 3 kwenye wimbo wa taifa kwa kusema "Mungu ibariki Chadema, wabariki viongozi wake"
_
Wafuasi wa CCM wakashangilia kauli ya Mtungi na wakafurahia akina Nusrat kusota jela kwa madai eti wameharibu wimbo wa taifa. Sasa nawauliza hawa wafuasi wa CCM wenye vichwa kama "Mtungi" je hiki kilichofanywa na vijana wa CCM Temeke ni sawa? Pia muulizeni huyo mwenye "Mtungi" wake hiki ni nini? Je CCM hapa hawajaharibu wimbo wa taifa? Hizi double standard ndio zinafanya Mtungi aonekane Mtungi kweli. Mtungi bhana.!
Credit: Malisa Godlisten