CCM tusiende tena kwenye Midahalo

CCM tusiende tena kwenye Midahalo

kwa sasa Bunge halali lipo "mtaani" huko umebaki mkutano mkuu wa nec tena husio na mwenyekiti maalum. ngoja upepo uendelee kuvuma tu kitaa, tuone ka "bwana mkubwa" hajawaita wayamalize....!!!

UKAWA wana uwezo gani wa kuhimili gharama za midahalo na mikutano kwa miezi mitatu mfululizo? unless wawe funded na vikundi vya nje visivyoitakia mema Tanzania na hizo funds ndizo zikazowatenganisha.

Kitendo cha UKAWA ilitakiwa iwe ni protest ya siku moja tu na siku ya pili warudi bungeni. Na si kulisusia bunge kabisa, hawana vyanzo vya mapato na hapo ndipo watakapoanza kutumika. Tena kwa kukujuza tu, licha ya kutumiwa na makundi ya nje, CCM yenyewe wanaweza kuwatumia kwa fedha kiaina ili iwasambaratishe.

Kitendo cha UKAWA mimi nnakiona ni kama pweza kujipalilia mkaa mwenyewe anapochomwa.

Utanambia.
 
Leo nilikuwepo Serena Hotel kuhudhuria Mdahalo ulioandaliwa na Taasisi moja binafsi nchini (jina limenitoka). Nimesahau hadi jina la Taasisi kwa yaliyotokea pale. Mdahalo huo ulikuwa ukiongozwa na Bi.Rosemary Mwakitwange na kurushwa moja kwa moja na ITV na Radio One. Pamoja na washiriki wengine,meza kuu iliwajumuisha watu 'wazito'.

Mdahalo ulijikita katika Mada: Tanzania Tuitakayo.Lakini hasa ilizungumzwa sana Rasimu ya Katiba mpya.Meza kuu ilikuwa na Wageni kama Ndugu Juma Duni Haji (Waziri wa Afya wa Zanzibar-CUF),Ndugu Vuai Ali Vuai (Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Zanzibar) na Humprey Polepole (Mjumbe wa zamani wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba).

Kiufupi,CCM tumedhalilishwa,tumezomewa,tumejichanganya,tumepoteana,tumejiharibia na kukosea kuhudhhuria pale. Vuai hakutusaidia. Alibaki kutetema kwa hasira na kushikwa na tashwishwi zisizo na maana. Eti alidai watu 9000 ni asilimia 5 ya watu wote wa Zanzibar.Kweli?! Hivi hata kama Zanzibar ina watu milioni moja kamili,asilimia 5 ni watu 9000?

Duni na Polepole walitamba walivyoweza.Walishangiliwa.Walifunika.Walimpotezea mbali Vuai. Walishinda kirahisi kutokana na mwakilishi wa CCM kukosa hoja za haja na kubaki kubwabwaja. Sikuamini macho yangu.Watanzania watatuonaje kiuongozi kama watu waliopo ni watu aina ya Vuai? Tusiende tena kwenye Midahalo

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

may be ua right,ila sasa kwa mchakato wa katiba tusisimamie vyama,hapa ndo mambo yanapoharibika,na wale wapuuz wa dodoma ndio wanaofanya hayahaya ya kutanguliza bendera za vyama
 
UKAWA wana uwezo gani wa kuhimili gharama za midahalo na mikutano kwa miezi mitatu mfululizo? unless wawe funded na vikundi vya nje visivyoitakia mema Tanzania na hizo funds ndizo zikazowatenganisha.

Kitendo cha UKAWA ilitakiwa iwe ni protest ya siku moja tu na siku ya pili warudi bungeni. Na si kulisusia bunge kabisa, hawana vyanzo vya mapato na hapo ndipo watakapoanza kutumika. Tena kwa kukujuza tu, licha ya kutumiwa na makundi ya nje, CCM yenyewe wanaweza kuwatumia kwa fedhakiaina ili iwasambaratishe.

Kitendo cha UKAWA mimi nnakiona ni kama pweza kujipalilia mkaa mwenyewe anapochomwa.

Utanambia.

Unaposema vikundi vya nje visivyotakia mema Tanzania una maanisha nini???!!!
Tumekuwa tukipokea pesa kwa bajeti kutoka nje pia hivi huwa wana nia njema kwa mujibu wa nani???!!!!

Una maana hata kama wanachofanya kingekuwa sahihi inabidi waache sababu hawana fedha????!!!!
 
UKAWA wana uwezo gani wa kuhimili gharama za midahalo na mikutano kwa miezi mitatu mfululizo? unless wawe funded na vikundi vya nje visivyoitakia mema Tanzania na hizo funds ndizo zikazowatenganisha.

Kitendo cha UKAWA ilitakiwa iwe ni protest ya siku moja tu na siku ya pili warudi bungeni. Na si kulisusia bunge kabisa, hawana vyanzo vya mapato na hapo ndipo watakapoanza kutumika. Tena kwa kukujuza tu, licha ya kutumiwa na makundi ya nje, CCM yenyewe wanaweza kuwatumia kwa fedhakiaina ili iwasambaratishe.

Kitendo cha UKAWA mimi nnakiona ni kama pweza kujipalilia mkaa mwenyewe anapochomwa.

Utanambia.

ila ufadhili hata serikali inapewa ufadhili,kuna baadh ya vifaa vinavyotumiwa na vyombo vya dola huwa ni misaada na watanzania wanauliwa na vifaa hivyohivyo,hapa logic ni kuacha ndoto na akili za kivyama kujenga katiba,,,,ulimlalamikia Look-v kwa upuuz wake,yule alienda mbali si tu uchama mpaka udini aliuweka kwa sababu ya katiba hii hii,na hili ndo aliloliibua Lipumba na ndo hao UKAWA wakatoka,
Assalam aleykum
 
CCM bwana kwa kujitoa ufahamu, kwahiyo uushatutabiria kama tutakosa pesa kwani nyie hela mnayo? Acc zenu zote ziko na figure 3 au ndo mnatambia hela za STRABAG? Kuna mwisho wake mtatafuta mpk dirisha la kutokea mtakosa labda mkaungane na Wasira msituni
 
Nape alijua mvua ingemnyeshea, asingeweza kwenda
 
Unaposema vikundi vya nje visivyotakia mema Tanzania una maanisha nini???!!!
Tumekuwa tukipokea pesa kwa bajeti kutoka nje pia hivi huwa wana nia njema kwa mujibu wa nani???!!!!

Una maana hata kama wanachofanya kingekuwa sahihi inabidi waache sababu hawana fedha????!!!!

Nimeuliza hivi, huu mdahalo wa Serena kautayarisha nani na fedha za kukodisha ukumbi wamezitoa wapi? na hicho kikundi kilichotayarisha huo mdahalo wana faida ipi? naomba majibu kwa hilo.

Nikisema "vikundi vya nje visivyotakia mema Tanzania" nnamaanisha "vikundi vya nje visivyoitakia mema Tanzania".
 
Leo nilikuwepo Serena Hotel kuhudhuria Mdahalo ulioandaliwa na Taasisi moja binafsi nchini (jina limenitoka). Nimesahau hadi jina la Taasisi kwa yaliyotokea pale. Mdahalo huo ulikuwa ukiongozwa na Bi.Rosemary Mwakitwange na kurushwa moja kwa moja na ITV na Radio One. Pamoja na washiriki wengine,meza kuu iliwajumuisha watu 'wazito'.

Mdahalo ulijikita katika Mada: Tanzania Tuitakayo.Lakini hasa ilizungumzwa sana Rasimu ya Katiba mpya.Meza kuu ilikuwa na Wageni kama Ndugu Juma Duni Haji (Waziri wa Afya wa Zanzibar-CUF),Ndugu Vuai Ali Vuai (Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Zanzibar) na Humprey Polepole (Mjumbe wa zamani wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba).

Kiufupi,CCM tumedhalilishwa,tumezomewa,tumejichanganya,tumepoteana,tumejiharibia na kukosea kuhudhhuria pale. Vuai hakutusaidia. Alibaki kutetema kwa hasira na kushikwa na tashwishwi zisizo na maana. Eti alidai watu 9000 ni asilimia 5 ya watu wote wa Zanzibar.Kweli?! Hivi hata kama Zanzibar ina watu milioni moja kamili,asilimia 5 ni watu 9000?

Duni na Polepole walitamba walivyoweza.Walishangiliwa.Walifunika.Walimpotezea mbali Vuai. Walishinda kirahisi kutokana na mwakilishi wa CCM kukosa hoja za haja na kubaki kubwabwaja. Sikuamini macho yangu.Watanzania watatuonaje kiuongozi kama watu waliopo ni watu aina ya Vuai? Tusiende tena kwenye Midahalo

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Ndio maana hata bungeni hamjadili rasimu iliyo wakilishwa, na badala yake nnajadili rasimu yenu. Hivi mmeitoa wapi??
 
Nimeuliza hivi, huu mdahalo wa Serena kautayarisha nani na fedha za kukodisha ukumbi wamezitoa wapi na hicho kikundi kilichotayarisha huo mdahalo wan faida ipi? naomba majibu kwa hilo.

Nikisema "vikundi vya nje visivyotakia mema Tanzania" nnamaanisha "vikundi vya nje visivyoitakia mema Tanzania".

Kama ni misaada na ufadhili basi vyama na serikali wote wanapata! !!!!
Nani anakuwepo kuhakiki nia ya misaada na ufadhili wa aina hiyo??!!!!
Hatari ndio unaanza kuiona leo kwa mkutano wa serena????!!!
Haya yote yanafanyika kwa faida gani ya wanaotoa ufadhili na misaada?????!!!

Ingekuwa vema kuwa makini pia na vikundi vya ndani na watu binafsi wasiyoitakia mema Tanzania!!!!!

Unapowasha taa ukubali kuona unachotafuta na usichokitafuta pia!!!!!
 
Kama ni misaada na ufadhili basi vyama na serikali wote wanapata! !!!!
Nani anakuwepo kuhakiki nia ya misaada na ufadhili wa aina hiyo??!!!!
Hatari ndio unaanza kuiona leo kwa mkutano wa serena????!!!
Haya yote yanafanyika kwa faida gani ya wanaotoa ufadhili na misaada?????!!!

Ingekuwa vema kuwa makini pia na vikundi vya ndani na watu binafsi wasiyoitakia mema Tanzania!!!!!

Unapowasha taa ukubali kuona unachotafuta na usichokitafuta pia!!!!!

Bado hujajibu maswali yangu, unajaribu kuyakwepa na kuyajengea hoja muflis. Wafadhili wa Serikali wanajulikana na sio siri. Na hakuna anae ifadhili Serikali bila kuwa na faida na ufadhili wake.

Sasa unapowafadhili UKAWA una faida ipi?

Tafadhali jibu maswali yangu kama hauna jibu. Kaa kimya tu kuliko kujaribu kuyajengea hoja muflis.
 
Bado hujajibu maswali yangu, unajaribu kuyakwepa na kuyajengea hoja muflis. Wafadhili wa Serikali wanajulikana na sio siri. Na hakuna anae ifadhili Serikali bila kuwa na faida na ufadhili wake.

Sasa unapowafadhili UKAWA una faida ipi?

Tafadhali jibu maswali yangu kama hauna jibu. Kaa kimya tu kuliko kujaribu kuyajengea hoja muflis.

Kama ungekuwa huna akili ningejibu ila sijibu utakavyo sababu unajua kwenye maswali yangu kuna majibu yako na unajua kuwa yamo na nasema sijibu hapa kama utakavyo ila vile naona inafaa!!!!

Hakuna atajaye ifadhili UKAWA bila ya kuwa na faida nayo, same goes!!!!!
Sasa suala ni faida inamlenga nani na nani inamuacha nje ya muktadha?????!!!!
Misaada haiwezi kuwa na faida kwa wote hata kama imeainishwa hivyo kwa maandishi,sasa hoja yako ni ipi haswa????!!!!!

Misaada ya afya imeanza kitambo lakini mpaka sasa kina mama wanalala na kujifungulia chini????!!!Faida ya misaada unaipimaje kwa kundi lipi kwa mujibu wa nani?????!!!

By the way huo muunganiko ni matokeo ya vyama ambavyo vina ruzuku na vina wafadhili umewahi kuhoji hayo????!!!!
So either jointly au singularly cha muhimu ni hoja wanayobeba na sio ufadhili,sababu ufadhili ni syndrome!!!!!
 
Niliangalia mdahalo wote, msimlaumu Vuai mada aliyokuwa anaitetea haikuwa na facts za kuweza kumpa mwanya wa kuweza kuonekana hoja zake zina msingi. Yeyote atayeamua kutetea serikali mbili hatopata hoja za kuweza kutetea msimamo wake ukilinganisha na anayetetea serikali tatu.Kwa ufupi ni kuwa mtaji wa hoja uko katika serikali 3 zaidi kuliko kwenye serikali mbili, kama ingetokea TL apewe nafasi ya kutetea msimamo wa S3 na Vuai atetee S2 basi hata hilo garasa Vuai angeibuka mshindi - sababu ni kuwa hoja za kutaka S3 ni nyingi kuliko zile za kutaka S2.
 
Hapo nilikusudia kumaanisha TL atetee serikali 2 na Vuai atetee serikali 3 basi Vuai angeibuka mshindi.
 
Kama ungekuwa huna akili ningejibu ila sijibu utakavyo sababu unajua kwenye maswali yangu kuna majibu yako na unajua kuwa yamo na nasema sijibu hapa kama utakavyo ila vile naona inafaa!!!!

Hakuna atajaye ifadhili UKAWA bila ya kuwa na faida nayo, same goes!!!!!
Sasa suala ni faida inamlenga nani na nani inamuacha nje ya muktadha?????!!!!
Misaada haiwezi kuwa na faida kwa wote hata kama imeainishwa hivyo kwa maandishi,sasa hoja yako ni ipi haswa????!!!!!

Misaada ya afya imeanza kitambo lakini mpaka sasa kina mama wanalala na kujifungulia chini????!!!Faida ya misaada unaipimaje kwa kundi lipi kwa mujibu wa nani?????!!!

By the way huo muunganiko ni matokeo ya vyama ambavyo vina ruzuku na vina wafadhili umewahi kuhoji hayo????!!!!
So either jointly au singularly cha muhimu ni hoja wanayobeba na sio ufadhili,sababu ufadhili ni syndrome!!!!!

Nimeuliza hivi, huu mdahalo wa Serena kautayarisha nani na fedha za kukodisha ukumbi wamezitoa wapi? na hicho kikundi kilichotayarisha huo mdahalo wana faida ipi? naomba majibu kwa hilo.

Unaleta mambo ya akina mama wakati nyinyi wenyewe ndio mnawazalisha kama kuku. Hao kina mama mimba wanajijaza wenyewe? usianze viroja. Hebu anzeni kuwacha kuwaingilia bila kinga uone kama hospitali zitajaa. It takes two to tango.
 
Back
Top Bottom