Kikarara78
JF-Expert Member
- Nov 18, 2010
- 1,495
- 904
Natumaini Ushauri wako wahusika wataufanyia kazi,
Mada aka Status zako nazikubali sana, Haufungamani na Upande wowote ule.
Majuzi ulikuja na Uzi kuwa CCM kujibu mapigo ya UKAWA, na kweli tukaona.
Zidi kutufungua macho kwa nondo zenye mashiko.
Welcome back Mkuu Vuta - Nkuvute
Mada aka Status zako nazikubali sana, Haufungamani na Upande wowote ule.
Majuzi ulikuja na Uzi kuwa CCM kujibu mapigo ya UKAWA, na kweli tukaona.
Zidi kutufungua macho kwa nondo zenye mashiko.
Welcome back Mkuu Vuta - Nkuvute
Leo nilikuwepo Serena Hotel kuhudhuria Mdahalo ulioandaliwa na Taasisi moja binafsi nchini (jina limenitoka). Nimesahau hadi jina la Taasisi kwa yaliyotokea pale. Mdahalo huo ulikuwa ukiongozwa na Bi.Rosemary Mwakitwange na kurushwa moja kwa moja na ITV na Radio One. Pamoja na washiriki wengine,meza kuu iliwajumuisha watu 'wazito'.
Mdahalo ulijikita katika Mada: Tanzania Tuitakayo.Lakini hasa ilizungumzwa sana Rasimu ya Katiba mpya.Meza kuu ilikuwa na Wageni kama Ndugu Juma Duni Haji (Waziri wa Afya wa Zanzibar-CUF),Ndugu Vuai Ali Vuai (Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Zanzibar) na Humprey Polepole (Mjumbe wa zamani wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba).
Kiufupi,CCM tumedhalilishwa,tumezomewa,tumejichanganya,tumepoteana,tumejiharibia na kukosea kuhudhhuria pale. Vuai hakutusaidia. Alibaki kutetema kwa hasira na kushikwa na tashwishwi zisizo na maana. Eti alidai watu 9000 ni asilimia 5 ya watu wote wa Zanzibar.Kweli?! Hivi hata kama Zanzibar ina watu milioni moja kamili,asilimia 5 ni watu 9000?
Duni na Polepole walitamba walivyoweza.Walishangiliwa.Walifunika.Walimpotezea mbali Vuai. Walishinda kirahisi kutokana na mwakilishi wa CCM kukosa hoja za haja na kubaki kubwabwaja. Sikuamini macho yangu.Watanzania watatuonaje kiuongozi kama watu waliopo ni watu aina ya Vuai? Tusiende tena kwenye Midahalo
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam