CCM tusiende tena kwenye Midahalo

CCM tusiende tena kwenye Midahalo

Leo nilikuwepo Serena Hotel kuhudhuria Mdahalo ulioandaliwa na Taasisi moja binafsi nchini (jina limenitoka). Nimesahau hadi jina la Taasisi kwa yaliyotokea pale. Mdahalo huo ulikuwa ukiongozwa na Bi.Rosemary Mwakitwange na kurushwa moja kwa moja na ITV na Radio One. Pamoja na washiriki wengine,meza kuu iliwajumuisha watu 'wazito'.

Mdahalo ulijikita katika Mada: Tanzania Tuitakayo.Lakini hasa ilizungumzwa sana Rasimu ya Katiba mpya.Meza kuu ilikuwa na Wageni kama Ndugu Juma Duni Haji (Waziri wa Afya wa Zanzibar-CUF),Ndugu Vuai Ali Vuai (Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Zanzibar) na Humprey Polepole (Mjumbe wa zamani wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba).

Kiufupi,CCM tumedhalilishwa,tumezomewa,tumejichanganya,tumepoteana,tumejiharibia na kukosea kuhudhhuria pale. Vuai hakutusaidia. Alibaki kutetema kwa hasira na kushikwa na tashwishwi zisizo na maana. Eti alidai watu 9000 ni asilimia 5 ya watu wote wa Zanzibar.Kweli?! Hivi hata kama Zanzibar ina watu milioni moja kamili,asilimia 5 ni watu 9000?

Duni na Polepole walitamba walivyoweza.Walishangiliwa.Walifunika.Walimpotezea mbali Vuai. Walishinda kirahisi kutokana na mwakilishi wa CCM kukosa hoja za haja na kubaki kubwabwaja. Sikuamini macho yangu.Watanzania watatuonaje kiuongozi kama watu waliopo ni watu aina ya Vuai? Tusiende tena kwenye Midahalo

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Alisema watu laki 9
 
Mleta mada amevurugwa

waambie wenzako wa lumumba project kuwa wakati wote kupinga ukweli unatakiwa umakini wa hali ya juu na umahiri wa kupangua hoja na kujenga hoja zitakazopelekea ushawishi kwa wananchi.mara zote mmebaki kuattack personality na hoja nyepesi hivi kinana pemba aliongea nini cha maana kudilute hoja za ukawa?zaidi ya kumzungumzia maalim self!
 
Mleta mada amevurugwa

Hujajibu hoja au ndio kama kawaida yenu wana ccm kubwabwaja bila hoja. mmeaibika sana serena leo vuai anateyemeka tuuu! Anajing'ata tuu hajui kujenga hoja aibu tu ilimjaa.
 
Sasa kwanini wamekimbia bunge maalum la katiba? Hizo hoja zao mitaani zinawasaidia nini?
 
Sio kweli dada angu, hebu tuanzie kwenye chopa 3, kata 3. Kalenga na chalinze ndio tuseme hayo,

Ni aibu kujivinia ushindi haram tena kwa watu ambao hata kusoma hawajui.chalinze mnawanyima elimu makusudi ili muendelee ku,kanyaga ,haya na huko kwingine mananunua shahada mnatumia rushwa na mnajivuna mmeshinda hata aibu huoni?? Kati ya wapiga kura wote walio jiandikisha ni robo tu ndio walio piga kura halafu mnajitutumua, hata ushindi wa vyama vya upinzani pia sio wa kushangilia sababu ya idadi ya wapiga kura, lakin kwa vile upinzani wakishinda wanashinda kwa haki hawatoi rushwa wa hawahongi wali na maharage na vijikanga na viji tshirt wana haki ya kuushangilia ushind wao lakini sio ccm.
 
Sasa kwanini wamekimbia bunge maalum la katiba? Hizo hoja zao mitaani zinawasaidia nini?

Bunge unalijua wewe na walio kuwa kwenye mdahalo sio wabunge ni wananchi,,sasa ukitaka kuona ccm wanavyo tokea kwenye madirisha wananchi waende bungen kujenga hoja na wana ccm ndio utajua kuwa ccm hawana hoja hata chembe.
 
Vuai alinifurahisha limoja tu. Akasema mjengoni hawakubaki ccm wenyewe bali walibaki na wale kundi la 102 waliobaki yaani 175. Nikamwona wa maana sana. Yaani aliamua kuusema ukweli kuwa, JK aliwalundika humo mabuda 175 ya ccm ili kuhakikisha kuwa kelele zao ziwazime UKAWA. Kazi kweli kweli. Mh. Vuai, lazima aelewe kuwa hao waliobaki wasingalithubutu kutoka nje kwani Boss hakuwatuma kuipinga ccm. Alisema UKAWA warudi au wasirudi mambo yataendelea kama kawa. Safi sana lakini aelewe kuwa kitakacho zaliwa hapo ni cha ccm sio cha wananchi. Tumeshaerevuka na kuelewa kuwa kinachojadiliwa sio ile rasimu iliyopelekwa kisheria bali nyingine ya vichochoroni. Msipoteze kodi zetu jamani ccm. Mwogopeni Mungu.
 
Watamkumbuka mzee Makamba alishawakataza ccm kutohudhuria midahalo maana lazima wavuliwe nguo.CCM INANUKA DHAMBI
 
CCM siku zote hawajawahi kufanya vizuri kwenye midahalo tangu ule wa urais wa 1995 wakiwakirishwa na mzee mkapa ulioongozwa na mzee Simbeye.
lakini pia hiyo ndo taawira halisi ya viongozi wanao liongoza taifa hili ndo maana hata katika bunge hoja zao ni hafifu sana na mwisho kuishia kulazimisha maswala.
hata hivo Vuai asingekuwa na hoja yoyote kwa kuwa siku zote kuutetea uongo ni ngumu sana, maana ukweli anaujua.
 
Leo nilikuwepo Serena Hotel kuhudhuria Mdahalo ulioandaliwa na Taasisi moja binafsi nchini (jina limenitoka). Nimesahau hadi jina la Taasisi kwa yaliyotokea pale. Mdahalo huo ulikuwa ukiongozwa na Bi.Rosemary Mwakitwange na kurushwa moja kwa moja na ITV na Radio One. Pamoja na washiriki wengine,meza kuu iliwajumuisha watu 'wazito'.

Mdahalo ulijikita katika Mada: Tanzania Tuitakayo.Lakini hasa ilizungumzwa sana Rasimu ya Katiba mpya.Meza kuu ilikuwa na Wageni kama Ndugu Juma Duni Haji (Waziri wa Afya wa Zanzibar-CUF),Ndugu Vuai Ali Vuai (Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Zanzibar) na Humprey Polepole (Mjumbe wa zamani wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba).

Kiufupi,CCM tumedhalilishwa,tumezomewa,tumejichanganya,tumepoteana,tumejiharibia na kukosea kuhudhhuria pale. Vuai hakutusaidia. Alibaki kutetema kwa hasira na kushikwa na tashwishwi zisizo na maana. Eti alidai watu 9000 ni asilimia 5 ya watu wote wa Zanzibar.Kweli?! Hivi hata kama Zanzibar ina watu milioni moja kamili,asilimia 5 ni watu 9000?

Duni na Polepole walitamba walivyoweza.Walishangiliwa.Walifunika.Walimpotezea mbali Vuai. Walishinda kirahisi kutokana na mwakilishi wa CCM kukosa hoja za haja na kubaki kubwabwaja. Sikuamini macho yangu.Watanzania watatuonaje kiuongozi kama watu waliopo ni watu aina ya Vuai? Tusiende tena kwenye Midahalo

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Naibu katibu mkuu wa ccm yupo vizuri sana nimeshuhudia ule mdahalo ,kilichoshuhudiwa kama kawaida ya upande wa pili kuwa na jazba na alijitahidi kueleza kuwa wawe tayari kusikiliza wanayoyapenda na wasiyoyapenda,huo ndiyo ustaarabu wa mdahalo,kadhalika duni haji naye alisisitiza vivyo hivyo.tupo kwenye mjadala jamani tuwe tayari kusikiliza na yale ambayo hatuyapendi,hatuhitaji kutukana wala kuzomea ama kupiga kelele hoja kwa hoja
 
Bunge unalijua wewe na walio kuwa kwenye mdahalo sio wabunge ni wananchi,,sasa ukitaka kuona ccm wanavyo tokea kwenye madirisha wananchi waende bungen kujenga hoja na wana ccm ndio utajua kuwa ccm hawana hoja hata chembe.

Duh! Duni siyo mbunge? usianzishe vichekesho hapa, kuna jukwaa lake.
 
Nape ndio boya angeharibu kabisaa, na mleta mada0hajavurugwa kwa kuwa kila mtu alishuhudia.
 
Ushauri wako ni mzuri sn kwa mtu mwenye akili lazima aufuate lkn haya majamaa hayasikii,,,hija hawana kabisa ht bmk wamebaki wenyewe lakni hawasemi hoja zao za kutaka serikali mbili wamebakia kutukana tu
 
Sio kweli dada angu, hebu tuanzie kwenye chopa 3, kata 3. Kalenga na chalinze ndio tuseme hayo,

tatizo sio chopa 3 au kata 3, c c yao inatumia msuli mkubwa kulazimisha mambo ila taratibu watu wataelewa tuu watajua mbivu na mbichi.
 
Nape alisoma alama za nyakati mapema akaingia mitini sasa nahodha yeye hakuelewa pale anakuja kuongea na wananchi na siyo kwenye lile bunge lao wanalodanganyana pale.
Kila akianza uwongo anazomewa baadae anapata hasira kisha anatulizwa na moderator kwa kuambiwa tuvumiliane inabidi awe mpole. Kwa kweli sijaona swali alilojibu Vuai zaidi ya kuongea siasa za CCM+Uwongo uwongo waliozoea.
Hii mihadala hawaiwezi, Chama kimekufa na wao wenyewe ndiyo wazidi kukizika.
 
Kutetea uongo kunahitaji uwe na moyo wajiwe. Moyo huo wanao wakina wasira, lukuvi, nape, kinana nk
 
Wenye akili wanaelewa tu kwa nini juma duni, au polepole akiongea walikuwa wanashangiliwa saaana, kusoma hujuwi hata picha huoni.
 
Back
Top Bottom