Zakumi
JF-Expert Member
- Sep 24, 2008
- 5,063
- 2,471
Mkuu Zakumi,
Ningependelea utoe hiyo proof kama ulivyoainisha.
Pili, sikubaliani na hoja kuwa Nyerere alijenga chuo kimoja kilichotoa watu chini ya 500. Sentensi ilivyo ni kweli lakini maudhui yake yana walakini.
Hatuwezi kuongelea chuo kikuu kimoja au wasomi chini ya 500 bila kuiangalia historia na ukweli unaoambatana na huo.
Wakati anakabidhiwa nchi alikuwa na watu wa kiwango cha chuo kikuu wasiozidi 10. Kwa maneno mengine hata angewachagua wote wawe katika baraza la mawaziri bado alikuwa na upungufu.
Wakati hayo yakitokea alichukua nchi ikiwa haina chuo kikuu, vyuo vya elimu ya kati n.k. Hapo hujaongelea uwepo wa maprofesa wakufundisha vyuo hivyo.
Changamoto alizo kuwa nazo ni nyingi kuliko kiongozi yoyote aliyefuata. Illiteracy ilikuwa juu sana, hali ya afya ilikuwa mbaya, miundo mbinu hafifu, nishati mgogoro na wakati huo huo tukiishi katika dunia hii ya mafuta kutoka arabuni.
Majanga kama njaa, mafuriko hayakusita kumsubiri afanye kazi aliyotarajia.
Wapi aanzie katika hali dhaifu kama hiyo?
Kwanza ilikuwa kujenga vyuo vya elimu ya kati katika kila sekta ili kutoa wataalam wa kupunguza tatizo wakati nchi ikijenga uwezo. Tukaona kila tupliposafiri vyuo vya elimu, kilimo, medical assistant, technical college n.k.
Lengo halikuwa kupata madokta 100 kwa wakati mmoja watakaoishia katika hospitali za rufaa, lengo lilikuwa kupata wataalam wa akti kuzui yale yaliyokuwa katika uwezo wao.
Pengine ukiacha chuo kikuu cha UDOM nitajie chuo kingine cha elimu ya juu au ya kati kilichojengwa na marais waliofuata.
Wote walichofanya ni ku-upgrade vyuo vilivyokuwa tayari katika kada ya kati.
Pengine unitajie katika Hospitali za serikali zilizopo zipi zimejengwa nje ya utawala wa Nyerere.
Tafadhali nitajie vituo vya afya 20 kati ya 100 unavyojua vilijengwa baada ya mwalimu.
Katika nishati, tuliwahi kujadili kuwa hakuna rais aliyefuata aliyewekeza katika nishati kuliko Nyerere.
Kuwekeza sina maana ya kutumbukiza mabilioni kwa mtu mmoja na kumlipa milioni 167 kwa siku, nina maanisha kitu tunachoweza kusema huu ni uwekezaji kama Nyumba ya mungu, Kidatu n.k.
Nyerere aliwekeza katika viwanda vidogo ili kuinua thamani ya bidhaa za wakulima kama Pamba. Hakuna kiongozi aliyefuata ambaye amewekeza katika viwanda zaidi ya Mwalimu. Waliofuata wameaua vyote na kuacha tuagize mitumba na zile za china.
Miundombinu inayojengwa sasa ni kazi ya uwekezaji wa Nyerere.
Sikumbuki kiongozi aliyeanza kwa kuvunja pori ili kujenga bara bara, achilia mbali ujenzi wa reli zn.k.
Ni katika kipindi chake nchi iliingia vitani pamoja na kufa kwa EAC.
Katika kipindi cha miaka 23 ambayo ni michache kuliko pale alipoachia hadi sasa bado alifanya mambo mengi kuliko viongozi wote watatu kwa pamoja.
Ninachotaka kukueleza hapa siyo nini Mwalimu alifanya, nataka uiangalie picha nzima kutoka kila angle kabla ya kutoa takwimu za wahitimu 500. Uwezekano wa kutoa wahitimu 5,000 ulikuwepo, je hicho ndicho kilikuwa kipaumbele kwa wakati na changamoto zilizomkabili?
Kwanini tuangalie watu 500 au pungufu bila kuangalia ilikuaje na ingefanyikaje.
Nyerere kama mwanadamu ana mapungufu sasa ni wajibu wetu tuonyeshe mapungufu yako wapi na angefanya nini kwa wakati ule. Kuibuka na takwimu zachuo kikuu kimoja, wahitimu 500 bado hakujaweza kutueleza kosa lilikuwa wapi na kwamba takwimu hizo kwa kuangalia social-economic factors zinatoa ukweli.
Nguruvi,
I took great pains to compile historical data from Unesco. Please refer the attached files. In those files, which cover the period between 1970 and 1997, you will clearly see the efforts the country took to educate the nation.
There were was a surge of primary school net enrollment in late 70s which reached its peak in 1980. Afterward there was a downward spiral of the process which reached 57% in 1985, 51% in 1990, 49% in 1997.
With regard to secondary school education, the number is pathetic. In 1970, the country enrolled 3,762 secondary school students and 9,847 in 1985.
The entrance for tertiary education was even worse. In 1970, the country enrolled 2,027 students. In 1985 the country recorded 4863 new students.
Remember, tertiary education includes all post secondary school institutions of learning.
The number of students enrolled in various levels of education was under the auspices of government policies.