Bongolander
JF-Expert Member
- Jul 10, 2007
- 5,067
- 2,197
That is the point Mchambuzi.Vile vile Marehemu Edward Sokoine; Kuna kitabu kimoja nimekisoma na kugundua jinsi gani kiongozi huyu asivyopewa heshima (hasa na viongozi uchwara waliomfuata baadae) anayostahili kwa mchango wake mkubwa sana kwa taifa letu (Tanzania); huyu mtu alikuwa anaelekea urais after nyerere on merit kabisa; wengi wetu tulimjua kwa suala la vita dhidi ya mafisadi (wahujumu uchumi tu), lakini kumbe mtu huyu alifanya mambo makubwa sana kwenye kilimo n.k; nikipata muda nita-share taarifa hii.
Mbali ya Nyerere, hakuna kiongozi mwingine wa ngazi za juu (mawaziri wakuu, makamo wa rais na marais) aliyelifanyia taifa hili mambo ya maana in terms of legacy kama Sokoine (ukimtoa mkapa ambae alijaribu kidogo) pamoja na elimu yake ya Form Four (i.e. Sokoine); bottom line is, you have a point kuhusu Mrema;
Wasomi wanaofaa na wale wasio wasomi wanaofaa wote hawatakiwi na CCM. Ukiangalia watu wanaouawa hapa Tanzania unaweza kuona kuwa ni wasomi, au kama sio wasomi ni wale ambao wanajua mafisadi wanaitafuna vipi Tanzania. Kiaina naweza kusema kuwa kuna elements za jinsi wasomi walivyokuwa treated katika serikali tatu au nne zilizozpita Uganda.
Watu wote wenye elimu na wasio na elimu, lakini wanaoweza kulifanyia taifa mambo ya maana, hawana political future katika mazingira ya sasa ya Tanzania.