Mkongwe Mzoefu
JF-Expert Member
- Aug 10, 2018
- 842
- 2,467
Mimi na wenzangu raia wa Mkoa wa Manyara hakika mmetuaibisha sana sisi wakazi wa Kateshi kwa kutumia shida na machungu yetu kama mtaji wenu CCM katika harakati zenu za siasa kuelekea uchaguzi wa mitaa 2024 na ule mkuu 2025.
Nini hasa kimepelekea nyie mjivishe jukumu la nani aje atupe pole na misaada na nani asikanyage Kateshi?
Msiba ni wetu, nyie ni nani mnataka kutufanya sie ni mbumbumbu kiasi mnafikia kumzuia Mwenyekiti wa Chadema na ujumbe wake mdogo kuja kutusabahi? Mlichofanya ni kama mnatuchulia na misiba itajirudia kama sie hatutafanya zindiko la kuondoa hilo balaa mlilotuangushia bila nyie kujua.
Kikwetu kwenye msiba ukimbagua mtu yeyote basi elewa utazika mfululizo hadi umuombe radhi uliyembagua wakati kaja kwako kwa moyo mmoja.
Tafadhali sana muombeni msamaha Mbowe na watu wake, msibani hakuna mgeni mashuhuri kuliko mwingine, vinginevyo tutawachukia kama mlivyochukiwa na kabila fulani ambalo mlikula hadi rambirambi zao kwa kashfa na kejeli nyingi.
Tunajua hata tusipo wapa kura kama huko mtaiba tuu, lakini bora mjue mnaiba kura kwa vile tumewachukia kwa mliyotenda.
Wazee wetu watakaa na kulishughulikia hili kama mtadharau kutuomba radhi na kumuomba radhi mgeni wetu aliyekuja kwa moyo mwema.
Pia soma> Manyara UPDATE: Waliofariki kwa Mafuriko Wilayani Hanang wafikia 63
Nini hasa kimepelekea nyie mjivishe jukumu la nani aje atupe pole na misaada na nani asikanyage Kateshi?
Msiba ni wetu, nyie ni nani mnataka kutufanya sie ni mbumbumbu kiasi mnafikia kumzuia Mwenyekiti wa Chadema na ujumbe wake mdogo kuja kutusabahi? Mlichofanya ni kama mnatuchulia na misiba itajirudia kama sie hatutafanya zindiko la kuondoa hilo balaa mlilotuangushia bila nyie kujua.
Kikwetu kwenye msiba ukimbagua mtu yeyote basi elewa utazika mfululizo hadi umuombe radhi uliyembagua wakati kaja kwako kwa moyo mmoja.
Tafadhali sana muombeni msamaha Mbowe na watu wake, msibani hakuna mgeni mashuhuri kuliko mwingine, vinginevyo tutawachukia kama mlivyochukiwa na kabila fulani ambalo mlikula hadi rambirambi zao kwa kashfa na kejeli nyingi.
Tunajua hata tusipo wapa kura kama huko mtaiba tuu, lakini bora mjue mnaiba kura kwa vile tumewachukia kwa mliyotenda.
Wazee wetu watakaa na kulishughulikia hili kama mtadharau kutuomba radhi na kumuomba radhi mgeni wetu aliyekuja kwa moyo mwema.
Pia soma> Manyara UPDATE: Waliofariki kwa Mafuriko Wilayani Hanang wafikia 63