Parabolic
JF-Expert Member
- Dec 3, 2013
- 2,743
- 2,601
Kitendo cha CCM kuwaita waandishi wa habari katika press conference iliyotarajiwa kufanyika jijini Dodoma Julai 28, kuanzia saa 11 jioni hadi saa 6 usiku si cha kiungwana.
Ilitarajiwa kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla angetoa taarifa ya watia nia ya ubunge na udiwani, lakini waanjijini humo, lakini waandishi wa habari walisubiri katika ukumbi wa White House bila mafanikio hadi saa 6 usiku, a,bapo ndipo kikao cha Kamati Kuu ya CCM ndio kilimaliza muda wake.
Waandishi waliendelea kusubiri wakidhani Makalla atazungumza usiku huo, lakini pia hakutokea.
Ilitakiwa CCM watoe taarifa kwamba ama kikao kimeahirishwa au kimesogezwa mbele na waombe radhi usiku ule ule. Lakini kukaa kwao kimya, kinatoa tafsiri ya dharau kwa waandishi na hata wananchi waliokuwa wakisuiri kwa hamu taarifa hiyo.
Tabia hii ya wanasiasa au watoa taarifa kupoteza muda wa waandishi wa habari imekita mizizi kwa sababu ya ama ni dharau tu kwa tasnia ya uandishi wa habari au kuonyesha kwamba hata wanahabari wenyewe wameamua tu kudharaulika, kwa sababu hatuoni viongozi wao wakitoa taarifa za kukemea.
Ifike wakati sasa dharau hii kwa waandishi wa habari ikemewe na iachwe mara moja.