CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

Kwa tuliosoma zamani na tuliopenda namba (hesabu), twajaribu kutafuta uwiano kati ya kitendo cha CCM kuvua gamba, je walitumia HCF (Highest Common Factor) au LCM (Lowest Common Multiple) ? Samahani wana JF kiswahili chake sikijui, nimesoma zamani.

Nadhani hizi picha mbili zitatusaida kujibu hiki kitendawili, Kazi kwenu !


kikwete_rostam1.jpg wtcoj.jpg

Tangu hawa watu wawili wanadiwe na kupewa Ubunge hata mwaka bado. Cha ajabu walionadiwa eti wanatoswa kwa kuhusishwa na ufisadi lakini aliyewanadi na kusimamia uchakachuaji wa kura anaenziwa kama shujaa na asiye na na doa - CCM ni killer poke ?
 
Kwa tuliosoma zamani na tuliopenda namba (hesabu), twajaribu kutafuta uwiano kati ya kitendo cha CCM kuvua gamba, je walitumia HCF (Highest Common Factor) au LCD (Lowest Common Denominator) ? Samahani wana JF kiswahili chake sikijui, nimesoma zamani.

Nadhani hizi picha mbili zitatusaida kujibu hiki kitendawili, Kazi kwenu !



Tangu hawa watu wawili wanadiwe na kupewa Ubunge hata mwaka bado. Cha ajabu walionadiwa eti wanatoswa kwa kuhusishwa na ufisadi lakini aliyewanadi na kusimamia uchakachuaji wa kura anaenziwa kama shujaa na asiye na na doa - CCM ni killer poke ?
Kigawo Kikubwa cha Shirika (KKS), Kigawo Kidogo cha Shirika (KDS)
 
Kigawo Kikubwa cha Shirika (KKS), Kigawo Kidogo cha Shirika (KDS)
Asante Mkuu Mnyinusura, si unajua tena kisomo chetu cha miaka ileee ambapo wazito wa kuelewa waliketishwa karibu na Mwalimu huku vipanga wakilinda benchi za nyuma.

Hata hivyo kwa hizo picha mbili una maoni gani ? Naona kama vile mkuu anakula kivulini marugaruga juani huku wazalendo pamoja na njaa yao makofi kama kawa.
 
Asante Mkuu Mnyinusura, si unajua tena kisomo chetu cha miaka ileee ambapo wazito wa kuelewa waliketishwa karibu na Mwalimu huku vipanga wakilinda benchi za nyuma.

Hata hivyo kwa hizo picha mbili una maoni gani ? Naona kama vile mkuu anakula kivulini marugaruga juani huku wazalendo pamoja na njaa yao makofi kama kawa.

As usual wametumia LCF - Mwenyekiti. Hahaha ahahaha ahaha!
 
Jana nimemsikia Msekwa akisema viongozi wapya wa CCM watazunguka nchi nzima kujitambulisha kwa wananchi kuwa wamejivua gamba na sasa ni wapya na pia kuwa chama chao kimezaliwa upya. Tunatofautiana uwezo wa kuelewa na kutambua mambo, CCM wanaposema wamejivua gamba wanamaanisha nini hasa na ni ujumbe gani wanajaribu kuwapa wananchi hasa wa vijijini wasioelewa siasa za mafumbo kama hizi isije kuwa ujumbe wao unapokelewa ndivyo sivyo, kuna mwenye kunielewesha tafadhali. Niko serious maana kuna watu wengi akiwepo mke wangu wananisumbua kuhusu swala hili la operation vua gamba wakati mwingine naona aibu kuwajibu kwa maana sina jibu sahihi. Msaada please.
 
sio siri chadema ndio chama kikuu cha upinzani kwasasa lakini kimekuwa kina kashfa nyingi sana kama vile swala la udini,ingawa walijaribu kumuita kundini prof safari ili kufuta dhana ya udini lakini bado swala la udini halijafutika mioyoni mwa watu,pia liko swala la kupewa fedha na mataifa ya nje,liko swala la ukabila,pia liko swala la vurugu,mfano hai ni pale mbunge machachari Godbless Lema alipotamka live bungeni kuwa milango ifungwe watu wapigane!(mwananchi ya leo) hivi kweli mtu aliyepewa dhamana na wananchi anaweza kutamka maneno kama hayo katika chombo kikuu cha maamuzi nchini?? sasa je chadema kuvua gamba na kuwa na sura mpya katika macho ya watu?
Suluba zikizidi hata punda anaweza kusema. CCM wamejaribu kuwaonea CDM katika kila nyanja wakitumia vibaya vyombo vya dola kama Usalama wa Taifa, Polisi, Mahakama hadi Bungeni. Kama mbunge huyo alitamka hivyo ni kutokana na hasira za kugandamizwa kulikopindukia kwa haki na Chama cha wezi na Mafisadi CCM. CCM kwa kutumia vyombo vinavyogharimiwa na wananchi wote (Wakiwemo wana CDM pia) kuwanyanyasa, kuwajeruhi, kuwaua na hata kuwaibia, sentensi yake hiyo inawakilisha si hasira zake tu, bali za watanzania wote waliochoka kugandamizwa na wababe hawa wanaoamini kuwa ni miungu ya Tanzania. Siyo siri kwamba badio tuna uchungu wa ndugu zetu waliofanywa vilema na polisi washabiki wa CCM kule Arusha na na unyanyasaji wa wawakilishi wetu na hizo Mahakama zenu zilizogeuka wakala wa CCM tunasubiri "Kichaa" yeyote kutuhamasisha tuingie mitaani mtuue kabisa kama si kuukomesha udhalimu wenu.
CCM lazima wajue lolote wanalowafanya wapinzani leo kesho itakuwa zamu yao na sheria na kanuni wanazotunga leo kuwagandamiza wapinzani zinaweza kutumiwa na hao hao watakapoingia madarakani.
Wamehangaika kuzuia uhuru wa maoni kuanzia nje mpaka ndani ya Bunge, ni lipi basi litakalobaki kama si kukamatana mashati na kudai haki kwa nguvu? Maandamano hawayataki ati yanahatarisha amani, mikutano hadi kwa kibali toka kwa makada wao "Wakuu wa wilaya, mikoa na polisi, Bungeni wameweka Spika mgandamizaji wa upinzani kada wa CCM. Ni lipi litakalobaki? Najua Mh. Lema alisema hivyo kwa kutania tu, lakini mawazo yetu wengi tulioko nje ya mjengo na kuhisi kuhujumiwa ni kwamba CCM wasipojirekebisha tutaidai haki kwa nguvu kama walivyofanyawenzetu Tunisia, Misri, na sasa Syria, Yemeni na kwingineko.
 
chadema ni mtoto wa nyoka wajua mtoto wa nyoka ni nani……..
Wala msijidanganye chadema itatuokoa wabunge wake wenyewe wapo kwa ulaji tu wa nafasi zao sasa mnaona jinsi vichwani hakuna kitu bado mnawatetea. Eti tu pigane hii mpya kwa siasa za bongo
 
sio siri chadema ndio chama kikuu cha upinzani kwasasa lakini kimekuwa kina kashfa nyingi sana kama vile swala la udini,ingawa walijaribu kumuita kundini prof safari ili kufuta dhana ya udini lakini bado swala la udini halijafutika mioyoni mwa watu,pia liko swala la kupewa fedha na mataifa ya nje,liko swala la ukabila,pia liko swala la vurugu,mfano hai ni pale mbunge machachari Godbless Lema alipotamka live bungeni kuwa milango ifungwe watu wapigane!(mwananchi ya leo) hivi kweli mtu aliyepewa dhamana na wananchi anaweza kutamka maneno kama hayo katika chombo kikuu cha maamuzi nchini?? sasa je chadema kuvua gamba na kuwa na sura mpya katika macho ya watu?
Kabla ya kuwaambia CDM wajivue gamba tuhakikishie kama wewe hauna gamba.
 
Mag3.. nadhani ni kwamba hawakufuata kile ambacho kinajulikana kama "the order of operation" ambayo enzi zile sisi tuliita MAGAZIJUTO. Yaani, ukipewa hesabu zenye masharti mbalimbali ya kuzifanya basi kuna mtiririko unatakiwa ufuate ili upate majibu. Hivyo, hesabu ambayo iko 34+45x23(34/10)-70 kwa mtu ambaye hajua Order of Operation ataanza kujumlisha!! Atafanya kile anachokiona lakini atafikia jibu lisilo sahihi kwani kanunu ya MAGAZIJUTO inatoa mwongozo wa kipi kifanyike kwanza kuanzia kushoto kwenda kulia.

Kwa hiyo naamini hawa jamaa pamoja na kuangalia HCF vile vile hawakufuata kanuni za MAGAZIJUTO matokeo yake wamepata majibu; tatizo ni majibu yasiyo sahihi.
 
Tukijiuliza kama nyoka anapojivua gamba anabadilika tabia basi na ccm kujivua gamba itakuwa mpya lakini kama nyoka habadiliki tabia au aina CCm inatakiwa kufanya zaidi ya kujivua gamba.
 
Kuna mtu mmoja alikuwa na tabia mbaya sana mbele ya jamii lakini huwezi kuamini alivyobadilika baadaye na sasa ni mfano mzuri katika jamii (na visevesa hutokea pia) na ni hivyo baadhi wakiishafanikiwa kutokana na dhambi zao wanabadilika kuwa wacha Mungu na hata wahubiri wa dini. To be objective tuwape muda angalau miezi sita kuwasoma mwelekeo na ndipo tuweze ku-project based on relevant updated data.

Lakini pia tuliosoma zamani tulikuwa na HCF na LCM.
 
Joka litaendelea kuwa joka hata likatwe mkia. Hakuna jipya hata hivyo vijoka vidogo vina sumu. Solution ni kuwauwa majoka wote kusafisha kichaka.
 
Kwani Joka likijivua Gamba uwa linahama pori?

BTW: Huwezi kuona msitu wakati upo msituni - Utaona MITI
 
Kwa tuliosoma zamani na tuliopenda namba (hesabu), twajaribu kutafuta uwiano kati ya kitendo cha CCM kuvua gamba, je walitumia HCF (Highest Common Factor) au LCD (Lowest Common Denominator) ? Samahani wana JF kiswahili chake sikijui, nimesoma zamani.

Nadhani hizi picha mbili zitatusaida kujibu hiki kitendawili, Kazi kwenu !



Tangu hawa watu wawili wanadiwe na kupewa Ubunge hata mwaka bado. Cha ajabu walionadiwa eti wanatoswa kwa kuhusishwa na ufisadi lakini aliyewanadi na kusimamia uchakachuaji wa kura anaenziwa kama shujaa na asiye na na doa - CCM ni killer poke ?


...mkuu, swali lako zuri kwani limegusa maeneo mawili muhimu ninayependayo maishani: Maths na Politics! Tuendelee kupata majibu toka kwa wataalamu wengine. Ila kitu kimoja kidogo sijakielewa kama nilivyo-highlight hapo juu, sijawahi kuona LCD (Lowest Common Denominator) bali LCM (Lowest Common Multiple). I nevertheless stand to be corrected.
 
Duuuuu! Hata wewe pia??? Mi nilidhani kashanga peke yake ndo ana mawazo mafupi, kumbe mko wengi hivi??? Ila tutafika tu.
chadema ni mtoto wa nyoka wajua mtoto wa nyoka ni nani..
Wala msijidanganye chadema itatuokoa wabunge wake wenyewe wapo kwa ulaji tu wa nafasi zao sasa mnaona jinsi vichwani hakuna kitu bado mnawatetea. Eti tu pigane hii mpya kwa siasa za bongo
 
yes KWA MTINDO WA ZOMEA-ZOMEA INAYOENDESHWA NA HAO GENDER-BALANCE WA CCM,KUNA HAJA YA SIKU MOJA KUFUNGA MLANGO ILI ANGALAU WALE KICHAPO KIDOGO.ILI WAELEWE KUJIHESHIMU NDANI YA BUNGE TOFAUTI NA WALIVYOZOEA MIPASHO YA TOT.
 
Jinsi ulivyoandika unaonekana kabisha wewe ni mgeni humu jamvini na si ajabu hii ni post yako ya kwanza. Unajitahidi karibu nawe utakuwa expert wa jf. Ila jaribu kuwa mbunifu sio unjweka mada ambazo watu wamezoea kuzisikia tangu mwaka jana. Be a great thinker!"!

Duh, ww waonyeshwa jua mchana , waulizwa nn hicho wasema huo ni mwezi, acha kukataa kila kitu huo ndio ukweli kijana
 
Back
Top Bottom