CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

Kwa kuvua gamba walikuwa wakimaanisha nyoka...Hivyo wananchi wanapasa kujua CCM ni joka inabidi wajihadhari nalo liwe la kibisa ama la porini yote ni hatari tu.
 
Source: Magazeti ya Rai, Alhamisi Aprili 14-20,2011;na Mtanzania Jumatano APRILI 13,2011;
kATIKA Rai nimevutiwa mno na nukuu za viongozi wapya hawa wawili, Nape Nnauye, Katibu wa Itikadi na Uenezi; na Katibu wake Mkuu Wilson Mukama:-
Nape: Uk wa 2 "Kuna mapinduzi makubwa yanakuja. Maadili kwa wengi wao yamepotea. Kwa hiyo basi nawaomba wajipange upya kama kuna mtu anajiona ni mchafu na hataki kubadiklika basi ajiondoe kabla ya kuondolewa,"
Wilson: "Ni lazima tukijenge upya chama chetu, watu wenye kashfa watalazimika kujiondoa wenyewe kabla hatujawafukuza."

Katika Mtanzania nimevutiwa na taarifa hii ya kipekee:-
Kichwa cha habari iliyopewa uzito wa kwanza kwamba "CHILIGATI, NAPE WAMCHIMBA JK" Kichwa hiki kiliambatana na habari iliyosheni utamu kwamba Chiligati na Nape saa chache baada ya kushika nyadhifa hizo wameanza kumchimba Mwenyekiti wao, Rais Jakaya Kikwete; , ambaye kwa mujibu wa habari hizo ni kwamba ni mtuhumiwa wa 11 kwenye orodha ya watu wanaotuhumiwa kuwa mafisadi kwa mujibu wa orodha ya LIST OF SHAME ya iliyosomwa na CDM DSM Mwembeyanga miaka kadhaa iliyopita nakurudiwa katika viwanja vya Jangwani mwaka jana 2011; na mpaka leo ushahidi wa dhahiri umethibitisha kulingana na kashfa za EPA, KAGODA, RICHMOND, DOWANS, IPTL, nk.

Bila shaka matamko ya aina hii yanazidi tu kujenga maswali mengi zaidi ndani ya waTz wanaofuatilia utekelezaji wa dhana ya Kujivua Gamba yenye Kaulimbiu "Towards New CCM"

Wakati nikitafakari kama kweli kuvua gamba kwa staili hii kutazaa CCM Mpya, nilikumbuka maneno ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CDM kwamba CCM inaumwa kansa kwenye damu, na siyo kwenye gamba; tena nikajuiliza kwamba hawa jamaa Nape na Chiligati ni wazao wa hawa wazee wanaotuhumiwa??? Je wana ubavu wa kutikisa hili dude CCM bila support ya waasis wa ufisadi walioenguliwa katika CC ya CCM na kupewa eti siku 90 kujitoa wenyewe!!!!!!!!!! WanaJF hivi JK naye yumo kwenye hizo siku 90????? YETU MACHO NA MASIKIO!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Huwezi kuamini watu wazima, wanafanya na kujifikirisha kitoto namana hii.
Asili ya ufisadi ni tofauti kabisa na asili ya Gamba!

Ufisadi unapotokea SIPO gamba linapotokea wala havikaribianai kwa namna yeyote ile.
Ufisadi unatokea MOYONI na Gamba linatokea MWILINI.

Huu ni upofu mkubwa kwa ccm kujifanya kuwa wako serias... Kwani wajifanye hawajui tofauti ya MOYONI na MWILINI????

NI HAKIKA TATIZO LA CCM NI KUBWA KULIKO LINAVYONEKANA KWA SASA..JUST WAIT AND SEE
 
Aslaaam aleikhum waheshimiwa?

Nimefuatilia kwa makini sana kitendo cha sie sie emu na kubaini kuwa ni kama ujio wa Kikombe cha babu wa Loliondo.

Sie sie emu wametumia ujanja ujanja, uongo uongo kuweza kuwateka wananchi, na has jamii ya wenzetu wa vijijini ambao maskini ya mungu hawaelewi chochoooote, wao ni fuata upepo tu.

Sie sie emu watapita kila mkoa kumwaga sumu yao "ku- brain wash" wananchi wasiojua kuchambua mambo na wanaweza uteka uma mkubwa sana huko remote areas.

watu hawajui kwamba, nyoka akijibandua gama hujenga sumu mpya tena kali ile mbaya na akikugonga nyoka aliyejitoa gama ukipona ww ujue una mungu wako.

Kwa mtizamo wangu, Sie sie emu ni km kinyonga anayejibadili rangi kulingana na mazingira na hatupaswi kufumbia macho hili. Lazima tukabiliane na huyu kinyonga asije akatung'ata maana kinyonga akuuma haachii mpaka umnusishe ugolo!

Shime wana CDM kuweni makini sana na hili halahala mti na macho!
 
The peeling exercise was received with mixed feelings – there are groups who believe the exercise was fruitful and another group that finds the exercise is partial and bias.
In any way, anti-ufisadi groups were fighting jointly against the so-called Fisadis. For a good strategist, there is lesson worth noting with caution that is clear out of the exercise - the fisadi group is calm, united and never spelled-over the beans in terms of their strategies before the mass as they always do. They now know expressly their enemies with strategies.
In short, they have the common objective and enemy (the ant-fisadi groups) whereas ant-fisadis have same enemy with different objectives. Ant-fisadis are moved by the agenda but they are not the same they belong to different camps, they never have tete-tete talks thereafter. This is dangerous especially when one gets lessons from Richmond aftermath!

A word of caution:
Strategists and other groups need to learn the lessons from the past fights when some figures fade away in attempt to pursue the agenda otherwise the isolated group may tear each anti-fisadi group off and the group will retain ability to function better than ever!
 
Source: Magazeti ya Rai, Alhamisi Aprili 14-20,2011;na Mtanzania Jumatano APRILI 13,2011;
kATIKA Rai nimevutiwa mno na nukuu za viongozi wapya hawa wawili, Nape Nnauye, Katibu wa Itikadi na Uenezi; na Katibu wake Mkuu Wilson Mukama:-
Nape: Uk wa 2 "Kuna mapinduzi makubwa yanakuja. Maadili kwa wengi wao yamepotea. Kwa hiyo basi nawaomba wajipange upya kama kuna mtu anajiona ni mchafu na hataki kubadiklika basi ajiondoe kabla ya kuondolewa,"
Wilson: "Ni lazima tukijenge upya chama chetu, watu wenye kashfa watalazimika kujiondoa wenyewe kabla hatujawafukuza."

Katika Mtanzania nimevutiwa na taarifa hii ya kipekee:-
Kichwa cha habari iliyopewa uzito wa kwanza kwamba "CHILIGATI, NAPE WAMCHIMBA JK" Kichwa hiki kiliambatana na habari iliyosheni utamu kwamba Chiligati na Nape saa chache baada ya kushika nyadhifa hizo wameanza kumchimba Mwenyekiti wao, Rais Jakaya Kikwete; , ambaye kwa mujibu wa habari hizo ni kwamba ni mtuhumiwa wa 11 kwenye orodha ya watu wanaotuhumiwa kuwa mafisadi kwa mujibu wa orodha ya LIST OF SHAME ya iliyosomwa na CDM DSM Mwembeyanga miaka kadhaa iliyopita nakurudiwa katika viwanja vya Jangwani mwaka jana 2011; na mpaka leo ushahidi wa dhahiri umethibitisha kulingana na kashfa za EPA, KAGODA, RICHMOND, DOWANS, IPTL, nk.

Bila shaka matamko ya aina hii yanazidi tu kujenga maswali mengi zaidi ndani ya waTz wanaofuatilia utekelezaji wa dhana ya Kujivua Gamba yenye Kaulimbiu "Towards New CCM"

Wakati nikitafakari kama kweli kuvua gamba kwa staili hii kutazaa CCM Mpya, nilikumbuka maneno ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CDM kwamba CCM inaumwa kansa kwenye damu, na siyo kwenye gamba; tena nikajuiliza kwamba hawa jamaa Nape na Chiligati ni wazao wa hawa wazee wanaotuhumiwa??? Je wana ubavu wa kutikisa hili dude CCM bila support ya waasis wa ufisadi walioenguliwa katika CC ya CCM na kupewa eti siku 90 kujitoa wenyewe!!!!!!!!!! WanaJF hivi JK naye yumo kwenye hizo siku 90????? YETU MACHO NA MASIKIO!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
sidhani kama kuna maajabu yatakayotokea badae. JK afanye juhudi kupatikane sheria kali inayolenga maadili ya viongozi. Yale ya azimio la Arusha yana umuhimu kwa sasa na Mwalimu Nyerere aliona mbali!!
 
sio siri chadema ndio chama kikuu cha upinzani kwasasa lakini kimekuwa kina kashfa nyingi sana kama vile swala la udini,ingawa walijaribu kumuita kundini prof safari ili kufuta dhana ya udini lakini bado swala la udini halijafutika mioyoni mwa watu,pia liko swala la kupewa fedha na mataifa ya nje,liko swala la ukabila,pia liko swala la vurugu,mfano hai ni pale mbunge machachari Godbless Lema alipotamka live bungeni kuwa milango ifungwe watu wapigane!(mwananchi ya leo) hivi kweli mtu aliyepewa dhamana na wananchi anaweza kutamka maneno kama hayo katika chombo kikuu cha maamuzi nchini?? sasa je chadema kuvua gamba na kuwa na sura mpya katika macho ya watu?
 
Kilichowekwa wazi na CCM ni kwamba wamekiri kuna UFISADI au ndani ya CCM ama ndani ya serikali yao ama vyote viwili. Kingine kilichowazi ni kuwa wanaotuhumiwa na UFISADI au uchafu wowote wana nguvu kubwa kifedha au kiushawishi kuliko Kamati Kuu ya Makamba na wengine ambao wamejiuzulu. Hata kama waliombwa kujiuzulu, au kulazimishwa - tunachoona kwa nje ni kuwa hawako tena katika vyeo vyao!!

Inastaajabisha kuwa watu wanaotegemewa kujiondoa ni watu waliofanya makosa na kuiumiza jamii ya kiTanzania kwa wizi na matumizi mabaya ya madaraka. Hao wanapewa nafasi ya "kujiondoa" na sidhani mashtaka yatafuata. Napata hamu kuona watu wakijiuzulu baada ya siku 90. Ninachotegemea ni kutoona hilo likitokea na badala yake CCM kufanya mabadiliko (baada ya siku 90) mengine ambayo watuhumiwa wanaojulikana kwa CCM watakuwa na roles mpya kabisa ili wasisemwe!!!

CCM wamefanya kosa watalokuja kujutia siku za usoni. WaTanzania watataka kuambiwa ni nani CCM wanamjua kama fisadi na amekataa kujiuzulu. Tunarudi kwa EPA na makampuni kufanya deal ya kurudisha pesa bila kutajwa wala kushitakiwa. Hii ndio Tanzania inayoongozwa na CCM na kusema inafanya utawala wa sheria!!
 
sijaona hoja ya msingi hapa, labda hapanihusu... sibishi hodi na wala sikai:A S-key::A S-key::A S-key::disapointed::disapointed:
 
Mafisadiza walioorodheshwa na CDM, na ushahidi wa wazi kuthibitika ni 11; Kukimbiza habari za Rostam Aziz peke yake wakati wqako 11 ni ufisadi wa namna nyingine ya UVCCM; Kuweni wazi UVCCM vinginevyo mtazidi kuikoroga CCM na hatimaye kufa kifo cha mende kama ya KANU ya Daniel Arap Moi:
WaTz bado wanadai kujua hatima ya kesi za akina EPA, DOWANS, IPTL, KAGODA, na mengine mengi.
Kuilaumu JF ni kupoteza muda; Msekwa amezeeka kiasi cha kusahau kuwa na yeye ni foisadi kwa mgongo wa Rostam Aziz. Kwa nini siku 90 na siyo 30??? Kuna nini ndani ya 90?????
Tunataka watuambie kwamba mizizi 11 ya ufisadi iliyojificha ndani ya CCM imefumuliwa, ni pamoja na JK ambaye ni mzao wa Ufisadi wa Rostam, Chenge na Lowasa;
Hata hivyo mimi kwa karibu sana naona kifo na mazishi ya CCM!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hapo gamba liko wapi? Yapi maoni yako kuhusu hizo kashfa, unazielewa na kujua chimbuko lake? You stop being naive on critical issues.
 
Think global, na usiongee issue usizozijua. Unaonekana ni old fassioned m2
 
Kashanga bana!!! Tehetehetehetehe! Umeishiwa staili wewe! Si utafute staili mpya uje nayo?? Hii tumeshaizoea! Aibu huna jipya!
 
  • Thanks
Reactions: LAT
there is a change of key players but the strategy remains the same.
Huko ndio kujivua gamba!!!
Mimi nasubiri kusikia kishindo cha ccm kuanguka.
 
Back
Top Bottom