CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

CCM kujivua ‘gamba’ Dodoma

Wajivue gamba (sijui ni nani aliwavalisha hilo gamba) wasijivue bado CCM ni chama cha mafisadi.
 
HUYO SIO GAMBA TU NI SABABU YA VIFO VYA WANA -ARUSHA LAKINI BADO YUKO MADARAKANI MPAKA LEO, 4o zake ziko njiani
 
Hawa wanacheza na nguvu ya umma eh? Hii nguvu ya umma ndo imesbabisha wao kujivua magamba, muswada wa katiba mbovu umekataliwa, na sasa rahisi hajui aendako wala atokako na sasa bado tunasubiri yeye mwenyekiti wao ajivue hilo gamba na riziwani wake baada ya kuwavua wenzake.
 
Tofauti yao na sisi ni kuwa wao wanafanya wanachokiamini, lakini sisi tunafanya tusichokiammini. Ndani ya ccm hakuna mwenue mtazamo tofauti na mwezake , tofauti iliyomo ni nani ana fisadi sana na nani anafisadi kidogo , anayefisadi kidogo anataka apate nafasi ya kufisadi zaidi, hii ndo tofauti ya mtazamo wao.

Kwa bahati mbaya hata wapinzani nao hawana mtazamo tofauti na waliomo ccm, kama mtu anafuatilia uhalisia na si ushabiki basi anaweza kubaliana na mimi.

Angalia samples: Mrema tulisukuma hadi gari lake yuko wapi, angalia akina Tambwe, angalia akina Marando na nccr leo wako chadema, angalia akina Lipumba.
Angalia Maalim Seif amesababisha watu kuawa kupoteza wapendwa wao akijifanya anapigania haki hadi machozi yanamtoka leo yuko wapi? Hakuna lolote.
 
Kwa kuwa CCM wanawaambia Watanzania kwamba MAGAMBA yao ni WATU WANAOTUHUMIWA KWA UFISADI na si MFUMO UNAOLEA UFISADI. Sasa ningependa kuwauliza CCM kwamba je Baada ya Siku Tisini MAGAMBA yafuatayo watayavua?

1. Jakaya Kiwete
2: Rostam Aziz
3. Edward Lowasa
4. Nazir Karamagi
5. Zakia Meghji
6. Anderw Chenge
7. Basil Mramba
8. Benjamin Mkapa
9. Yusuph Makamba
.
.
...
....
.......

Sio Vibaya tukiendelea kuwakumbuka akina Nape Magamba ya CCM ni yapi.
 
Umenena,

Hatukatai kuwa wamepiga hatua kwani hata kuukubali msamiati wa ufisadi ni hatua na wengi waliwahi kunukuliwa kukataa kuwa huo msamiati haupo. Pia kukubali kuwa ndiyo unaitesa CCM nayo ni hatua kubwa tu mara nyingi tumetafuta wachawi wakubumba leo tunasema wazi mafisadi ndani ya CCM ndiyo wabaya wetu. Sasa hili la kukataliwa litakuja pale watakaposhindwa au kukwepa kwa makusudi kuwashughulikia hao mafisadi!

We give them benefit of doubt but they have walked this lane b4.
 
Hawajavua Gamba ila wamelipaka rangi gamba lilelile na rangi yenyewe imewaishia bila kumaliza kichwani!
 
Nawashangaa sana wana CDM kila kukicha nyimbo zile zile ambazo mmeimba leo mwaka wa 6 hamjui kuwa mwisho watu wamechoka kuusikia kwa nini hamtafuti wimbo mpya? CCM wameamua kujivua gamba ,kila kukicha nyinyi ndo mnajifanya mnaelewa yote waliyopanga CCM kufanya kiasi cha kujifanya sasa nyinyi ndo mnaoijua sana CCM kuliko waliomo! kama mnazani CCm haijajivua gamba uoga wenu nini?
Mkatoriki akiamua kuokoka na akaamua kubatizwa kwa maji mengi kwa nini waliombatiza huamini kuwa sasa ni mlokole mwenzao?
 
Hawajavua Gamba ila wamelipaka rangi gamba lilelile na rangi yenyewe imewaishia bila kumaliza kichwani!

yani wewe!!!

mimi bado sijapona kuhusu ile ripoti iliosomwa na Mwakyembe bungeni mwaka juzi kuhusu richmond, hivi waziri mkuu alivojikomiti iliishia wapi vile??? mimi mbona bado nasubiri majibu ya utekelezaji?
 
Gamba aliwavalisha nani? Mwaka gani? Mlilivaa gamba hilo wakati wa awamu ya Mwinyi, Mkapa au Kikwete? Na kwanini mliamua kulivaa hilo gamba? Miaka yote hii hamkulishtukia hilo gamba hadi 2011? Hivi kuondoa hao mafisadi wachache ndio CCM kimekuwa kisafi? Mbona bado kuna mafisadi wa kumwaga tu ambao hata kutajwa hadharani hawatajwi? Acheni usanii wenu!! CCM bado ni Chama Cha Mafisadi Watanzania hawawezi kuzugika eti sasa mmejisafisha na si chama cha mafisadi tena. Nitafurahi kama kuna kada yoyote atakayeweza kuyajibu maswali hayo hapo juu.
 
Ukisema wana CDM una maana wana JF?
unaposema wana hofu una maana kupigana na ufisadi au ipi? manak eninavyojua mie, walioiba hela yetu watakaporudisha ndio lugha itabadilika, au wewe ulielewaje? labda kidogo ufafanue.
Lugha inayotumika na itakayotumika kwa kurudia kila siku na wakati ni kuhusu vita ya ufisadi, wizi, kutokuwajibika kwa wananchi, kutokutilia maanani dhamana ya uongozi.
hakuna kipya hapa.
 
Sasa na wewe inakuuma nini..........ungependa kuona leo CDM inaacha kuwasema wewe na baba ako na wale majambazi wengine mliowaficha kwenye chama lenu.....................

Mbona unahofu sana na CDM...........BTW nani kakutuma kuwasemea wananchi...who are you? Lakini pia huo ni mtazamo WAKO na sio wa WANANCHI.........Na ukitaka kujua hili cheki jana watu walivyokuwa na hamu ya kusikia majambazi wapya
 
Tutasema na kuwataja mafisadi pamoja na miaka mingine hadi hapo mafisadi watakaporudisha pesa zikajenge madarasa na zahanati na kuwawekea maji wananchi,Makamba alishawahi kusema tutasemasema halafu tutasahau lakini leo yeye amelazimisha kujiuzulu eti magamba yanavuliwa,Kikwete alishasema hatumnyimi usingizi leo amepauka ,midomo imemkauka,ametumbukia kucheza tune ya Chadema ,chama chake hakina miezi mitatu kitakuwa kimekatika mapande makubwa sana.
 
Inavyoonekana ccm tatizo limo katika mwonekano wote wa chama. Yaani mfumo mzima umejengwa kwenye msingi wa rushwa, kulindana na unafiki. Kwa kuwa chama hiki kinatambulishwa na rangi ya kijani, hivyo tunaweza kusema rangi ya kijani ndiyo gamba lenyewe. Hivyo, ni lazima chama hiki kibadilike chote ndani na nje ili kizaliwe upya. Kubadili cc na sekretarieti haitoshi.

:angry:
 
Thats image of ccm for many years. Killing our grand fathers and mothers by refusing safe water, better education, electricity and many many problems they created for our country. ccm was just a killer like this one,

green-snake.jpg


Now we can say bye bye for good.

Pallbearers-from-the-Zambian-Scouts-Association-ferry-the-casket-for-late-Anti-Corruption-COmmission-chairman-Valentine-Chileshe..jpg
 
Tuwe makini sana hapa, silaha ya Nyoka ni (venom) hata kama atalivuwa gamba lake mara 10 bado anabakia ni tishio kwa mwandamu kwa kubakiwa na sumu yake.pia kuna uwezekano mkubwa kuitumia Venom kwa mashambulizi.
 
Back
Top Bottom