CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

Mzee Mwakijiji,
Haya mathlan tukubali kwamba CCJ ni hao waliojitokeza ikiwa ni pamoja na wewe. Sawa kabisa, lakini mnashindwa kutuvuta kwa sababu moja kubwa. Nyie Kushindwa kuelewa TATIZO la wananchi hivi sasa ambalo ndilo linatangulia kabla ya hizo Itikadi zenu.
Nitakwambia tena na tena ili upate kunielewa vizuri natokea wapi.
Wengi wetu tunajiona kama wafungwa ndani ya gereza hili la chama CCM...Tunachokitaka ni kuondoka ktk hali hi ya ufungwa, na ndio maana nikatumia ule mfano wa ndege iloanguka kisiwani. Sasa unapokuja na idea ya kuroroka ni muhimu kwetu kusikia master Plan ya kutuwezesha ku escape toka kifungoni au kuondoka ktk adha za kisiwani hiki na kuwa HURU.

Sisi sote kwa ujumla wetu hapa JF tunataka kusikia mtaweza vipi kutuondoa ktk Utawala huu wa CCM na sio siasa za baadaye. Hata hao TANU chini ya na mwalimu Nyerere walitupa siasa za kujikomboa kwanza toka utawala wa mkoloni kabla ya itikadi za huo Ujamaa kuja miaka saba baadaye. Ndivyo wanavyofanya wana Mapinduzi wote duniani kutafuta support ya wananchi ili watoke ktk utawala unaowagandamiza.

Nachokiona mimi CCJ wanakuja na siasa za Itikadi kama vile nchi yetu haina matatizo, mkuu wangu sivyo wananchi wengi wanavyoitazama Tanzania ya leo..na kibaya zaidi viongozi na wanachama wa CCM wamekaa kama makaburu hawaoni shida hizi kwa sababu wao wako ktk hali nzuri ya kimaisha. Na kwa makosa ya wazi kabisa Utawala mzima unawanufaisha wale wanakubaliana nao kwa kuvaa magwanda ya Kijani kujionyesha wao ni watu tofauti kabisa na watawaliwa. Tofauti na makaburu, waliokuwa na Ubaguzi wa rangi sisi tunatumia ubaguzi wa mavazi na bendera za chama...na kwa bahati nzuri sii wananchi wengi wanakubali mfumo huu wa utengano.

Njia pekee ya CCJ kuweza kufanikiwa ni kuja na master Plan ya kuwakomboa wananchi toka gereza hili la CCM. Na ndio hapo tunapokuja na mchango wetu kwamba, hii great escape haiwezi kufanikiwa pasipo muungano wa makundi mengine yanayotaka pia kuondokana na kifungo hiki, pamoja na kwamba huko nje ya kifungo kila jumuiya inaweza kuwa na mipango yake. Walifanya Zimbabwe, South Africa nchi zote za Ulaya ya mashariki, Bosnia na majuzi tu Poland, Kenya, Zimbabwe tena na Liberia. Wote hawa walijenga mbinu za kukiondoa chama tawala pale wananchi hawakuwa na matumaini - Tumaini jipya kwa wananchi waliokosa Uhuru huanza na mbiu ya FREEDOM..na Uhuru hauwezi patikana pasipo wapinzani kuwa na nguvu moja japokuwa wana imani za kiitikadi tofauti..

Mkandara,

a. kwanini muungano wa kuiondoa CCM umeshindikana sasa hivi miaka 15 tangu kurudi kwa mfumo wa vyama vingi?
b. Kwanini muungano huo utamanike na uonekane unawezekana kwa ujio wa CCJ?
c. Kwanini vyama vilivyopo sasa (ukiondoa CCJ ambacho hakina itikadi, hakielewi matatizo ya wananchi na hakina mpango unaoeleweka wa ukombozi wa Mtanzania kutoka katika utumwa wa CCM) visiungane mara moja kwani tayari vina usajili wa kudumu na vina sera na mipango kamambe ya kuiondoa CCM?
 
Mkandara,

a. kwanini muungano wa kuiondoa CCM umeshindikana sasa hivi miaka 15 tangu kurudi kwa mfumo wa vyama vingi?
b. Kwanini muungano huo utamanike na uonekane unawezekana kwa ujio wa CCJ?
c. Kwanini vyama vilivyopo sasa (ukiondoa CCJ ambacho hakina itikadi, hakielewi matatizo ya wananchi na hakina mpango unaoeleweka wa ukombozi wa Mtanzania kutoka katika utumwa wa CCM) visiungane mara moja kwani tayari vina usajili wa kudumu na vina sera na mipango kamambe ya kuiondoa CCM?
Shukran, swali zuri sana..
Mimi kama mwananchi ndicho nilichokiona kimekosekana toka vyama hivyo vinginevyo..Nimesema sana kuhusu haya hata kabla ya ujio wa CCJ. Sasa maadam kimekuja chama chenye kutangaza tumaini jpya, nategemea kitakuwa tofauti na vyama vilivyotangulia na sio kurudia siasa zile zile..Why NCCR-Mageuzi, CUF, Chadema, TLP wote walishindwa ni kutotambua Umuhimu huu kwani huwezi kumwondoa CCM kwa kutumia siasa za Itikadi ambazo wananchi wengi walalahoi hawafahamu tofauti zake. Na Ajabu, kulingana na madai yako umasemna CCJ wamekuja tofauti na vyama vilivyotangulia hali ukweli ni kwamba wanakuja na siasa zile zile za kina Mrema, Mtikila na Mbowe badala ya master plan. Again nitakukumbusha kwamba tatizo letu sio Kikwete hili nitapinga hadi kesho, maanake naona kilamwanasiasa anamtazama JK kama ndio tatizo.. Tatizo letu ni chama kizima cha CCm na limeanza toka Mwinyi - tulipokubali vyama vingi pasipo kubadilisha mfumo wa mamlaka ya rais, serikali na chama tawala.
 
Mzee Mwanakijiji,
Kwa kuongezea tu nitakupa ukweli ambao wengi hatupendi kuuweka maanani leo hii. Waislaam waliutaka Uhuru wa Tanzania mapema lakini wasingeweza kufanikiwa pasipo support ya Wakristu. Ndipo walipokuja na plan ya kuwavuta Wakristu na mwalimu akapewa Uenyekiti.
Pamoja na tofauti za kiimani, itikadi na malezi yao mwalimu alipokea kitu kicho akiwa pia na nia moja tu - kumwondoa mkoloni kwanza. Mwalimu aliweza kuwatumia waislaam na Wakristu kwa pamoja (umoja wao) kuleta Uhuru na kisha kuleta itikadi zake za Ujamaa na Kujitegemea, jambo ambalo kina Marealle na Mtenvu walishindwa kuliona - We should learn from Him..
 
Hiyo ni dhana potofu na propaganda za maliberali tu. Matajiri mabilionea wengi ni Democrats....
Mr Ngabu point yangu siyo nani tajiri au maskini kati ya Republican na Democratic, nachotaka kujua hapa kwetu TZ mtu akisema yuko Chama "A" na mwingine yuko chama "B" hawa watu wawili wanatofauti gani za kiitikadi zinazowafanya wawe kwenye vyama tofauti. Mfano mtu kukosa uteuzi wa chama chake na kuamua kukihama je kuhama kwake kunasababishwa na tofauti za kiitikadi au uchu wa madaraka? Mtu akiondolewa kwenye uongozi na kuhamia Chama kingine, je hapo amesukumwa na tofauti za kiitikadi au kusaka ajira?.

We have a long way to go to realise benefits of multiparty system.
 
Kauli ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa ya kutangaza kuipa kipaumbele Sheria ya Gharama za Uchaguzi katika shughuli za ofisi yake kipindi hiki dhidi ya mambo mengine, ikiwamo uhakiki wa wanachama wa Chama Cha Jamii (CCJ) kwa ajili ya kupatiwa usajili wa kudumu, imezua mkanganyiko mkubwa miongoni mwa viongozi wa chama hicho. Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mwenezi wa CCJ, Costantine Akitanda, alisema wameipokea kauli ya Tendwa kwa uzito mkubwa, hivyo wamelazimika kukutana ili kuitafakari kwa kina.
“Ni kauli nzito sana aliyoitoa. Inahitaji kuitafakari kwa kina. Hivyo, viongozi wanakutana, na tutatoa tamko letu baadaye,” alisema Akitanda.
Awali, Katibu Mkuu wa CCJ, Renatus Muabhi, alisema pamoja na kauli hiyo ya Tendwa, wanachoamini wao ni kwamba, wamekamilisha yote yaliyohitajiwa katika nyaraka za maombi ya kupatiwa usajili wa kudumu waliyoyawasilisha ofisini kwa Msajili wa Vyama vya Siasa Ijumaa wiki iliyopita.
“Hayo mambo kwamba hana pesa, anaipa kipaumbele Sheria ya Gharama za Uchaguzi, sisi hayo hayatuhusu. Tunachokijua sisi ni kwamba, tumekamilisha kila kitu. Hivyo, tunakutana na baadaye tutatoa taarifa yetu,” alisema Muabhi.
uzi Tendwa aliitisha mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake na katika jumla ya mazungumzo yake, alieleza bayana kwamba, suala linalopewa kipaumbele na ofisi yake katika kipindi hiki, ni kushughulikia Sheria mpya ya Gharama za Uchaguzi.
Tendwa alitoa kauli hiyo zikiwa zimepita siku tano tangu viongozi wa CCJ, wawasilishe ofisini kwake maombi ya usajili wa kudumu, huku wakielezea matumaini yao ya kupatiwa usajili huo katika muda mwafaka ili waweze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, mwaka huu.
Mkutano huo uliitishwa na Tendwa kwa lengo la kuwaomba waandishi wa habari waisadie ofisi yake kuielimisha jamii kuifahamu vyema Sheria ya Gharama za Uchaguzi, ambayo alisema kuwa ni “ngumu”.
Alisema anazo taarifa za CCJ kuwasilisha katika ofisi yake nyaraka za maombi ya kupatiwa usajili wa kudumu zenye orodha ya wanachama wao kutoka mikoa 10 ya Tanzania Bara na Zanzibar.
Hata hivyo, alisema nyaraka hizo ziliwasilishwa katika ofisi yake Ijumaa wiki iliyopita, lakini hadi kufikia juzi, zilikuwa hazijafika mezani kwake.
Alisema kwa sasa ofisi yake haina fedha za kufanya uhakiki ili kujiridhisha kama wanachama walioorodheshwa kwenye nyaraka zilizowasilishwa na CCJ katika ofisi yake, hawana utata wowote wa kisheria.
Alisema hata ofisi yake kama itakuwa na fedha, itabidi akutane kwanza na uongozi wa CCJ kupanga lini waanze safari ya kwenda mikoani na waanzie mkoa gani kufanya uhakiki wa wanachama wao.
Hata hivyo, Tendwa alisema: “Priorities (vipaumbele) kipindi hiki ni Sheria ya Gharama za Uchaguzi.” na kuhitimisha kwa kusema: “Agosti 19 ni tarehe ya mwisho kwa vyama kuwasilisha majina ya wagombea wao. Sasa kama kufikia tarehe hiyo CCJ watakuwa wamekamilisha taratibu za usajili (wa kudumu), watashiriki uchaguzi.”
Aidha, alisema watahakikisha wanafuata taratibu na sheria na kwamba, wataiendea haki CCJ.
CHANZO: NIPASHE
 
Come to think of this - Sheria ya Gharama za Uchaguzi.. Hivi hiyo kazi ya kuhakiki gharama zake wanaolipa ni kina nani kodi za wananchi? na inatarajiwa kiasi gani kitatumika!
 
Come to think of this - Sheria ya Gharama za Uchaguzi.. Hivi hiyo kazi ya kuhakiki gharama zake wanaolipa ni kina nani kodi za wananchi? na inatarajiwa kiasi gani kitatumika!

Mkandara.. unajua kuna kitu kinaitwa kujipachika madaraka; Tendwa madaraka yake ya kwanza kabisa kisheria ni kusajili vyama vya siasa na kuhakikisha vinapata usajili wa kudumu na vinafanya kazi kwa mujibu wa sheria. Hana jukumu la kuacha hayo na kuanza kutoa semina za sheria sijui kutoa elimu ya uchaguzi. Hili ni jukumu aidha wizara ya sheria na katiba (ambayo yeye hayuko chini yake) au ni jukumu la ofisi ya Mwanasheria Mkuu.

Sasa anaposema ati hana fedha ya kufanya kile alichoapishwa kufanya na badala yake kudandia majukumu ya wizara nyingine anaamua kutufanya sisi wengine wote ni wajinga. Sheria ya Gharama za Uchaguzi tulishasema ni mbaya siyo "ngumu" kama yeye anavyosema. Wanachotaka ni watu washawishike waikumbatie pamoja na ubaya wake.
 
Mkuu nadhani ungepitia kwanza tovuti yao na kusoma majukumu ya Tendwa na Ofisi yake kabla hatujaanza kumhukumu visivyo - HAPA
 
Mkuu nadhani ungepitia kwanza tovuti yao na kusoma majukumu ya Tendwa na Ofisi yake kabla hatujaanza kumhukumu visivyo - HAPA

nimepitia mara nyingi na kusoma kwa undani sheria iliyoiunda (Sheria ya vyama vya siasa ya 1992 na mabadiliko yake). Jukumu la kwanza la msajili wa vyama vya siasa ni kusajili vyama vya siasa (ndio maana ya jina). Anatakiwa kutoa usajili wa muda au wa kudumu kwa kila chama ambacho kimetimiza masharti. Hawezi kuacha hilo na kusema ati naendesha semina ambayo ingeweza kuendeshwa na wizara au idara nyingine na siyo jukumu lake. Siyo jukumu lao kutoa semina ya sheria ya uchaguzi! Labda kuna mahali mimi sijapasoma unawezakunielekeza

kwenye sehemu inayohusu statement from the registrar inasema:
Written by Admin Wednesday, 27 June 2007 Statement of the Registrar of Political Parties
The main responsibilities of the office of the Registrar of Political Parties is to register political parties and monitor their administrative and political function in accordance with laws and regulations governing multiparty democracy in this country.


Major laws governing registration and monitoring of political parties are the constitution of the United Republic of 1977 and the Political Parties Act No. 5 of 1992. To-date there is eighteen political parties with permanent registration. These are CCM, CUF, CHADEMA, UMD, NLD, TLP, NCCR-MAGEUZI, CHAUSTA, JAHAZI ASILIA, TADEA, DP, FORD, NRA, SAU, DEMOKRASIA MAKINI, UDP, PPT-MAENDELEO UPDP.


The office is also responsible for aligning the political parties constitutions with the national constitution by ensuring political parties' constitutions do not overlap or ruin the interests and integrity of the mother constitution.


Other responsibilities of this office are to manage disbursement of government subvention to political parties, which have members of parliament and members in the local government councils and it also link the government with political parties.



The office is later responsible for receiving the returns on expenditure for analysis, scrutiny and publication of the audited Accounts for public consumption. The office is also expected to disclose any other sources financing to political parties. The office communicates to the public any information related to political parties and is also reports on National multiparty democracy by virtue of this position the office closely participates in monitoring and observation in all national electoral processes. The office hence serves as a link of the ruling party to the opposition parties.


The office is also held responsible for creating civic awareness to the public, which is implemented through educative seminars and workshops, and media, which has minimized political disputes amongst parties and within parties themselves. And this has also promoted good governance and enhancing democracy.

tunaweza kuona kuwa mambo ya seminda yako kwenye "creating awareness to the public" ambayo wao wenyewe wameweka ni mambo ya chini kabisa ukilinganisha na "main function". Tatizo ni kuwa wao wamepindua hilo na kuweka civic awareness kwanza na registration mwisho tena mwisho kabisa na hata kutokuwa na fedha ya kufanya. Sielewi kama mtu ambaye hana fedha za kufanya kazi yake ya msingi anaweza vipi kufanya kazi zile nyingine. NI sawa sawa na daktari anayesema kuwa hana fedha za kunguza wagonjwa wala tiba lakini anaweza kutoa tu semina za usafi na hivyo kufanya hospitali yake iwe ya kutoa semina za usafi siyo kutibu. HOspitali isiyofanya kazi ya kugundua na kutibu magonjwa na kubakia kutoa semina haiwezi kuitwa tena hospitali bali KITUO CHA SEMINA ZA AFYA.

Kwa vile Ofisi ya Msajili (kwa maneno yake mwenyewe) haina fedha za kufanya jukumu lake la kwanza kabisa la kikatiba na kubakia kutoa semina basi inatakiwa iitwe "OFISI YA UTOAJI WA SEMINA ZA ELIMU YA URAIA" or something similar.
 
Mwanakijiji; I'm 100% not conviced;
Naamini CCJ=CCM B;
Ukiacha maneno ambayo hata kwenye kanga yapo; kupigania rushwa aliyeanzisha tena Mwembeyanga pale alitaja majina-jemedari yupo; ajenda zingine zote ziko exhausted already na vyama; ukiacha mikauli mbiu ambayo mie naona kila mahala ipo na haisaidii; nasema Chadema ndio chama ambacho kama hata hao CCJ wangekuwa seriuos wangejiunga huko kuleta mapambazuko maana hata kila kelele wanazopiga ziko exhaused. Samahani mwanakijiji mie sio mwanachama ila napenda mageuzi; naamini hii ni danganya toto; watu wahamishe maskio CCJ then waue vyama ambavyo falsafa zao zilianza kujulikana sasa kama za Chadema; naamini hivyo wengine mtanijuza zaidi nisiyojua
 
Mwanakijiji; I'm 100% not conviced;
Naamini CCJ=CCM B;
Ukiacha maneno ambayo hata kwenye kanga yapo; kupigania rushwa aliyeanzisha tena Mwembeyanga pale alitaja majina-jemedari yupo; ajenda zingine zote ziko exhausted already na vyama; ukiacha mikauli mbiu ambayo mie naona kila mahala ipo na haisaidii; nasema Chadema ndio chama ambacho kama hata hao CCJ wangekuwa seriuos wangejiunga huko kuleta mapambazuko maana hata kila kelele wanazopiga ziko exhaused. Samahani mwanakijiji mie sio mwanachama ila napenda mageuzi; naamini hii ni danganya toto; watu wahamishe maskio CCJ then waue vyama ambavyo falsafa zao zilianza kujulikana sasa kama za Chadema; naamini hivyo wengine mtanijuza zaidi nisiyojua

nimekusikia wewe endelea kuunga mkono Chadema na itikadi yake ndiyo uzuri wa demokrasia.
 
Mkuu wangu,
Katika hili la Usajili mkuu wangu tuliache kama lilivyo lakini kama utaniuliza mimi nitakwambia kwamba sioni kama mna nia njema kabisa..samahani lakini!
Usajili wa CCJ unahitaji fedha za serikali kuendesha kampeni zake. Hali hii ni nchi maskini kabisa, nchi ambayo kila matumizi ya senti yake ni kumkwaza Mfanyakazi na Mkulima. Nchi yenye vyama 18 na bado vingine vinazaliwa ni Ulevi na upumbavu mkubwa sana.. Vyama vyetu havina tofauti za kiiikadi 3 kubwa na sio vyama vyote vimezifuata hizi tatu. Wote wamejirundika ktk Progressive na Social Demokratic tofauti zao ni vichwa vya viongozi tu. Hivyo vyama vyetu vinatofautiana vichwa vya watu ktk Utekelezaji.

Mkuu hii ni hatari kubwa ya kupoteza maana ya Demokrasia, kama tulivyopoteza maana ya dini na Uhuru wa kuabudu. Madhehebu yameundwa kutokana na kutokubaliana na mawazo ya viongozi pamoja na kwamba kimsingi wote wanakubaliana na Gospel. Hii italeta matabaka ya wananchi hata kufikia watu kujiita wao wanaCCM bila kujali ni itikadi gani mwana CCM anapaswa kuifuata.

What's wrong with kina Mkapa, Lowassa na hata Kikwete ni wao kuishi nje ya mafundisho ya kiimani (itikadi) ya chama CCM. Kinachotakiwa kifanyike ni kuwafukuza waumini hawa uanachama wakaanzishe wao chama chenye imani tofauti, lakini mnapowakimbia nyie na kuwachia kanisa inatupa wasiwasi watu wengi nini haswa malengo ya kukimbia kanisa hilo..Pia nimeona watu wakifukuzwa uanachama kwasababu hawakubaliani na kiongozi! Jamani chama ni Itikadi, huwezikumfukuza mtu uanachama kwa makosa nje ya itikadi ya chama. Ni sawa na kumfukuza mtu dini ati kwa sababu aligombana na Sheikh au Padri. Inachukua mtu kuvunja sheria za kiimani za dini au chama kufukuzwa na sio kukosana na kiongozi.
Hivyo mkuu wangu pengine mimi nipo at another level ya demokrasia kiasi kwamba siwezi kuelewa siasa za Bongo, lakini kwa kufahamu njaa iliyopo Bongo kuanzishwa kwa vyama vya siasa vingi ni moja ya matumizi mabaya ya kodi za wananchi..Vyama vingi vinajiandikisha kama njia ya ajira na kupata fedha za kutumia kwani Uchumi wa Tanzania (mzunguko wa fedha) huanza baada ya fedha hizi za Uchaguzi kutolewa.

The best option you guys had (Wanachama wa CCM) sio kukimbia chama isipokuwa kupambana na utawala huu dhalimundani ya chama CCM ktk uchaguzi wa ndani. Huu ulikuwa ni wakati wa kukisambaratisha chama toka ndani yaani hao kina Salim, Sitta na wengineo wagombee ndani ya chama against kundi hili la mashetani. Nina hakika kuna baraka za wazee wengi tu including Mzee Mwinyi na pia kuna laana za wachawi wengi against JK kina Mkapa, Sumaye na Lowassa. Hivyo vita ya ndani haiweza kuamlika kirahisi kwa sababu itakuwa vita ya vichwa (Uongozi)kuliko nyie kujitoa nje kukabiliana na chama kizima cha CCM...U dont need registration ya chama, vita ya ndani ibakie ndani na kufuli wekeni mlangoni hakuna kuamlia mtu..huku nje tuachieni sisi tulozoea kurusha mawe kisha tunaingia mitini..
 
Mkuu wangu,
Katika hili la Usajili mkuu wangu tuliache kama lilivyo lakini kama utaniuliza mimi nitakwambia kwamba sioni kama mna nia njema kabisa..samahani lakini!

bila ya samahani; unaonaje kama wakiifuta hiyo ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa au hata kuibadilisha jina? Polisi anayekataa kufanya kazi ya polisi aweze vipi kuendelea kuwa polisi?

Usajili wa CCJ unahitaji fedha za serikali kuendesha kampeni zake. Hali hii ni nchi maskini kabisa, nchi ambayo kila matumizi ya senti yake ni kumkwaza Mfanyakazi na Mkulima

Ni kweli, lakini ofisi hiyo hiyo inazo fedha za kutumia kuendesha semina, na kuwasafirisha vigogo wake sehemu mbalimbali. Lakini zaidi ni kuwa kuna fedha zinatengwa kila mwaka kwa ajili ya kazi hii ya kusajili vyama na sijui zimeenda wapi au hata tusiulizie?
. Nchi yenye vyama 18 na bado vingine vinazaliwa ni Ulevi na upumbavu mkubwa sana..

Ashakum..
Vyama vyetu havina tofauti za kiiikadi 3 kubwa na sio vyama vyote vimezifuata hizi tatu. Wote wamejirundika ktk Progressive na Social Demokratic tofauti zao ni vichwa vya viongozi tu. Hivyo vyama vyetu vinatofautiana vichwa vya watu ktk Utekelezaji.

Hili linaweza kuwa kweli kwa vyama vyenye usajili wa kudumu vilivyopo sasa. CCJ siyo kimojawapo.


Mkuu hii ni hatari kubwa ya kupoteza maana ya Demokrasia, kama tulivyopoteza maana ya dini na Uhuru wa kuabudu. Madhehebu yameundwa kutokana na kutokubaliana na mawazo ya viongozi pamoja na kwamba kimsingi wote wanakubaliana na Gospel. Hii italeta matabaka ya wananchi hata kufikia watu kujiita wao wanaCCM bila kujali ni itikadi gani mwana CCM anapaswa kuifuata.

Kuna tofauti za msingi ambazo haziwezi kuwafanya Shia wawe Sunni au Walutheri wawe Wakatoliki. Siyo tofauti ndogo. CCJ inataka kuleta tofauti kubwa kati ya CCM na CCJ.. ukiondoa herufi!


What's wrong with kina Mkapa, Lowassa na hata Kikwete ni wao kuishi nje ya mafundisho ya kiimani (itikadi) ya chama CCM. Kinachotakiwa kifanyike ni kuwafukuza waumini hawa uanachama wakaanzishe wao chama chenye imani tofauti, lakini mnapowakimbia nyie na kuwachia kanisa inatupa wasiwasi watu wengi nini haswa malengo ya kukimbia kanisa hilo..

Martin Luther alijaribu kujenga hoja 95 pale Ujerumani ili kulirudisha Kanisa Katoliki katika kile alichoamini ni njia sahihi. Ilikuwa vigumu mno na matokeo yake Kanisa likameguka. Kuna mambo mengi ni ya msingi mno kiasi kwamba haiwezekani kupatana.

Pia nimeona watu wakifukuzwa uanachama kwasababu hawakubaliani na kiongozi! Jamani chama ni Itikadi, huwezikumfukuza mtu uanachama kwa makosa nje ya itikadi ya chama. Ni sawa na kumfukuza mtu dini ati kwa sababu aligombana na Sheikh au Padri. Inachukua mtu kuvunja sheria za kiimani za dini au chama kufukuzwa na sio kukosana na kiongozi.

Ni kweli.

Hivyo mkuu wangu pengine mimi nipo at another level ya demokrasia kiasi kwamba siwezi kuelewa siasa za Bongo, lakini kwa kufahamu njaa iliyopo Bongo kuanzishwa kwa vyama vya siasa vingi ni moja ya matumizi mabaya ya kodi za wananchi..Vyama vingi vinajiandikisha kama njia ya ajira na kupata fedha za kutumia kwani Uchumi wa Tanzania (mzunguko wa fedha) huanza baada ya fedha hizi za Uchaguzi kutolewa.

Kuna ukweli lakini kila kazi ina malipo yake, nisingetegemea chama kianzishwe na watu wanaofanya kazi kwa kujitolea wasilipwe au wasipate maisha. Hata ng'ombe hula anapoperua. CCJ itaweka mfumo mpya kabisa katika utumishi wa chama. Sasa hivi karibu wote wanafanya kazi ya kujitolea na Chama kitajengwa na kusimamiwa na nguvu ya wananchi.

The best option you guys had (Wanachama wa CCM) sio kukimbia chama isipokuwa kupambana na utawala huu dhalimundani ya chama CCM ktk uchaguzi wa ndani. Huu ulikuwa ni wakati wa kukisambaratisha chama toka ndani yaani hao kina Salim, Sitta na wengineo wagombee ndani ya chama against kundi hili la mashetani. Nina hakika kuna baraka za wazee wengi tu including Mzee Mwinyi na pia kuna laana za wachawi wengi against JK kina Mkapa, Sumaye na Lowassa. Hivyo vita ya ndani haiweza kuamlika kirahisi kwa sababu itakuwa vita ya vichwa (Uongozi)kuliko nyie kujitoa nje kukabiliana na chama kizima cha CCM...U dont need registration ya chama, vita ya ndani ibakie ndani na kufuli wekeni mlangoni hakuna kuamlia mtu..huku nje tuachieni sisi tulozoea kurusha mawe kisha tunaingia mitini..

I think this is the best option as you see it not as it actually is. The best option is to return the country back to the people not by negotiating with a corrupt party or colluding with the enemies of our state; we have to create a new mechanism to do this noble and sacred duty. CCJ is such.
 
uzuri wa watendaji wengi wa Tanzania ni kutabirika kwao, wanafanya mambo kwa woga na kutekeleza matakwa ya walio juu yao. This has been a fundamental problem and the source of poor leadership in the country.

Watu kama msajili wa vyama ilibidi watekeleze majukumu yao katika mazingira ambayo hayaruhusu raia kukosa imani na ofisi husika na watendaji wake pia
 
Kwa muda mrefu niliokaa kazini na uku uraiani nimegundua kiini cha wananchi kushindwa kufanya mabadiliko ni ukosefu wa mwamkko wa kisiasa.

Maisha yetu wengi wetu tumeyajenga katika imani ya kwamba tutatumia mbinu yoyote kuendelea kuishi na kusogeza siku mbele kivyovyote vile ata iwe tunanyonywa, uchumi ni mbovu. Maadam unamudu kulisha familia yako basi mustakabali wa nchi kiujumla haukuhusu
 
We need to change, and that change is not necessarily embedded within a political party rather our attitude.
 
Najua jinsi vyama vingine vilivyotulet down.. this is the best chance we have.. NN kwa muda wote huu umewahi kuniona lini napigia debe chama chochote cha siasa and why this?

Yawezekana wewe ni kama Ng'walimu alivyompigia debe "mwenzetu, mpole, ndugu yetu, jamaa yetu, nabaadaye cleanman......" bado tukajikuta tunajutia ukapa japo tulifurahia ruksa. Umeshika kifimbo mwanakijiji?
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu huwezi kuchukulia mfano wa Shia na Sunni kwa juu juu pasipo kuelewa nazungumzia kitu gani. Utengano wa Shia na Sunnia ndio ulowafanya Waislaam wote kuwa weak kama dini, so are Christians na wengineo wote. Sasa ukirudi nyuma kutafuta kiini cha utengano wao utakuta ulitokana na kutokubaliana kwa VIONGOZI waliopewa dhamana ya kuongoza. Hii ndio ilivyotokea ktk Uislaam sijui zaidi ktk Ukristu lakini waasisi wa dini walikuwa kitu kimoja wakifanya ibada sawa hadi pale walipoondoka wao wakaja wajuzi wasomi wenye kutumia Elimu dunia ku question baadhi ya imani na ibada. Hawa ndio wakajitoa na kuunda dhehebu lao wakifuata misingi wanayoamini wao.

Sasa nikirudi ktk swala la CCM na CCJ, nakuta sii kweli kwamba Utengano huu unatokana na kutokubaliana ktk Katiba, Ilani na malengo ya waasisi wa chama isipokuwa utengano huu unatokana na Viongozi wabovu (wasomi uchwara) wanaoendesha nchi kinyume cha malengo yaliyokusudiwa kilipoundwa chama CCM. Mara nyingi kama sii zote ikitokea hivi, viongozi kama hawa waliosaliti mafundisho hufukuzwa Uanachama, hutengwa na jamii kwa sababu wanaitumikia itikadi nyingine. Maadam viongozi hawa wanaona wana itikadi pinzani na ile ya CCM watajitenga na kuanzisha chama chao wakitangaza imani yao wao lakini sii kuwaacha watu hawa wakitumia itikadi ya chama CCM wakifanya ibada zao kinyume kabisa.

Kwa nchi ya Wajinga na Malimbukeni kama Tanzania, wengi hawatatambua tofauti, as a fact hadi leo hakuna mtu, watu wala hata huyo msajili wa vyama aliyewahi ku question mbona CCM inaendesha utawala wake kinyume cha Itikadi yao?. Nitarudia kusema mkuu wangu kwamba IMANI yaani Itikadi ndio huunda waumini wake (chama) na sio sura za watu kukubaliana kutokubaliana. Maadam tumepotosha maana ya Demokrasia ni lazima wasomi kama nyie mrudishe au kufundisha nini demokrasia kiasi kwamba Ukisema wewe ni CCM watu wanajua unaamini kitu gani. Kama vile dini zetu nikisema mimi Muislaam moja kwa moja mtu mwingine anajua nini ibada zangu na mimi najua wazi natakiwa kufanya nini ili niwe Muislaam safi. Myahudi, Mkristu, Budha, Hindu wote hawa wametengana kutokana na Imani yao na sio tofauti zao kutokana na - Watu Kukubaliana kutokubaliana.

Mkuu wangu mimi nimekwisha sema Ni mfuasi wa Conservative, Huwezi kuliondoa hili akilini mwangu na huwezi kunipa Uanachama wa CCJ au Chadema pasipo chama hicho kufuata misingi ya Conservative..Na hakuna chama chenye uwezo wa kuniondoa uanachama kwa sababu sikubaliani na Uongozi uliopo kwani Imani yangu ktk Conservative haiwezi kupimwa kwa Uanachama. Kama simpendi Kiongozi wangu, sintampigia kura lakini siwezi kuwapa kura viongozi wenye ilani inayopingana na imani yangu.

Hivyo mkuu wangu unaweza kupinga sana mawazo yangu lakini tafadhali nakuomba sana wewe na wenzako kulitazama upya wazo langu hili. CCJ haiwezi kumshinda CCM wakitoka wao nje ya chama walichokijenga kwa imani safi. Mnaweza kuibomoa CCM ndani na kuna wakati CCM iliyumba sana hadi JK akaitisha vikao vya kusuluhisha. CCM ilikuwa inaondoka hivyo, na hakika kila mtu aliomba Mungu wavurugane na kutengana lakini nadhani JK kwa mara nyingine tena alitumia vitisho watu waka slow down na mwisho kufikia maamuzi ya kujiengua wao wenyewe. This will be a big mistake mkuu wangu utakuja nambia November.

Hivi sasa tu usajili wa CCJ uko matatani na hamna nguvu ya kumlazimisha msajili wa Vyama. sasa kama hamna hata nguvu ya kupambana na msajili mnafikiri mtaweza vipi kupambana na CCM ktk Uchaguzi mkuu? Yes, yawezekana mnayo nianzuri sana kama Chadema walivyokuja mwaka 2005. Mwanakijiji sijui kama unakumbuka. Nilijaribu kwa kila hali kuwashauri lakini nao wakaziba masikio yao wakiwa na hakika kubwa ya ushindi dhidi ya CCM. Hawakuona tuliyoyaona sisi na laukama wangechukua muda kutusikiliza bila kujali kwamba sii lazima tuwe wana Chadema kuweza kuwashauri wao pengine Chadema ingechukua nafasi kubwa zaidi ya ushindi.

Pamoja na yote haya mkuu wangu Ujio wa CCJ ni kutuongezea matumizi makubwa zaidi na kibaya zaidi ni pale mnaposhikilia haki YENU pasipo kufahamu kwamba nia na malengo ya chama ni kuwakilisha Umma mzima wa Watanzania. Kila Mtanzania kwa nia njema anatakiwa kuwapa ushauri maadam lengo lenu ni kuangusha utawala wa CCM, ambao leo ni adui wa kila Mlalahoi. Kama mtajitoa CCM basi unganeni na wale watakaokuwa tayari kuungana, mnahitaji kila nguvu ya Mlalahoi..
 
Najua jinsi vyama vingine vilivyotulet down.. this is the best chance we have.. NN kwa muda wote huu umewahi kuniona lini napigia debe chama chochote cha siasa and why this?
Unajikatia pande au unataka tuamini kila unachoamni au kutaka kuamini?
 
Back
Top Bottom