Caught on Tape: Mkakati wa Mamluki wafichuliwa!

Status
Not open for further replies.
Hii habari imekaa kiuda daku hivi. Waislam wanakaa kumkataa Kiongozi wa kichaga ilhali kuna wachaga waislamu wengi tu this doesnt add up...

Habari ina mkanganyiko na mgoloko mwingi, mara ukabila mara udini muradi kukidhi haja ya kuchochea watanzania. Huu ni mzuka wa OIC na Kadhi utatuletea habari nyingi watu wasipokuwa makini na kummeza nzima nzima kuna hatari mbeleni huko.

Point!

The whole thing has the look and feel of a spy novel. Hey, that's my opinion which I am entitled to it!
 
Jamani huu mara nataka kuuliwa na Shabbir Dewji mara Manji sa]udaku typical Mengi sa mchaga hatakiwi kugombea urais halafu waislam wanatumwa Songea! sijui wapo waislam wangapi Songea.

Only JF

Masatu sijui unataka upate nini, kama uko Dar nenda Radio Kheir jana walifanya kupindi maalumu na hayo ya uchaga walisema na wewe kusema Mengi kasema wachaga hawafai, unasema wewe hapa katika post ya kwanza na ya mkjj hakuna hilo. Unasema mawazo yako.

Jambo la msingi kwa mtu makini kama wewe, kama hukubaliani na jambo nenda kwa Obama kama ulivyosema awali umerudi kufanya nini humu? Huku wako wala nguruwe na wewe Muislamu nenda kwenye kahawa. Lakini yote ni utani jambo la msingi ni kama unajua jambo wajulishe watu usikanushe bila kujibu hoja nzito za msingi, kuna tape, audio na video, kuna picha, na wanajulikana unaambiwa Regency Hotel, unaambiwa Golden Tulip, unaambiwa Kinondoni Kazima namba 38, unapewa namba za magari, wewe unakanusha kwa maneno mepesi kama
"udaku typical Mengi"
unajidhalilisha.
 
Currently Active Users Viewing This Thread: 63 (13 members and 50 guests)
Halisi, Gelange Vidunda, Jamco_Za, Jmpambije, Juakali, Kichwangumu, Kitia, Mkora, Mong'oo, Mtindiowaubongo, Pipiro, Utamaduni, Zion Train

Nyie semeni udaku wakati watu wamejaa tele wanafanya kazi, na watu walikuwa pale Falcon wanapokea fedha za safari kwenda mikoani. Subirini mahubiri huko mikoani. Hoja hapa udini na ukabila ni geresha hoja ni siasa, ndio maana Waislamu wanamsema IGP Mwema ambaye ni muislamu kwa sababu ni mchaga na katika wahubiri yuko mchaga na Albert asili yake ni Mkristo, hapo AKILI KICHWANI
 
Naona watu wanajitahidi kubadilisha Thread na kupinga Hoja kwa Vioja.

Wakuu wote mlioweka data na hofu yenu juu ya habari iliyoonyeshwa na ITV (binafsi sijaiona) tunawashukuru kwa taarifa na ushahidi mliouweka ambao kuukataa ni mtu binafsi mwenye akili zake timamu aamue tu kuukataa.

Na kwa wale mnaokataa hakuna kitu kama hicho na kulipeleka suala hili katika udini, tunaomba mkatae kwa kusema kuwa Mkjj amedanganya, ila ukweli ni .............. muuseme nyinyi kwa ushahidi ili tuamini badala ya kukataa tu hakuna kitu, hakuna kitu bila ushahidi.

Tujitahidi kuzuia hisia zetu za Kidinbi na Ukabila pale inapofika ktk kutetea maslahi ya Taifa, inawezekana ukawa Muislam au Mkristo safi mwenye lakini waamini wenzio wakawa na lengo tofauti na lako kwa kutumia dini hiyo hiyo unayoamini wewe, Badala ya kukataa hawajafanya ni bpra ukachunguza na kugundua ukweli.

Mungu ibariki Tanzania tusielekee kwenye Udini na Ukabila, tukaanza kuuana wenmyewe kwa wenyewe.
 
Kwa wale wote wenye doubts (kama kweli ni doubts au you are just scared kutokana na ukubwa wa habari yenyewe) should read between the lines. I know the news is too bad to be true, lakini if u read it carefully na kama uliona ile tape ya ITV, basi you can simply conclude that something fishy is going on. Huyu anayesema kuna ubaya gani kwa masheikh kuzungumzia OIC. The thing is, mazungumzo yalikuwa ni zaidi ya OIC. Watu tumesikia kuhusu mkakati wa kuchafua watu. Not just OIC. Watu tumesikia kuhusu kugawana fungu la kutekeleza mkakati etc. Habari ndio hiyo. If you are not convinced, then stay tuned. Cause you will be surprised!
 
Currently Active Users Viewing This Thread: 63 (13 members and 50 guests)
Halisi, Gelange Vidunda, Jamco_Za, Jmpambije, Juakali, Kichwangumu, Kitia, Mkora, Mong'oo, Mtindiowaubongo, Pipiro, Utamaduni, Zion Train

Nyie semeni udaku wakati watu wamejaa tele wanafanya kazi, na watu walikuwa pale Falcon wanapokea fedha za safari kwenda mikoani. Subirini mahubiri huko mikoani. Hoja hapa udini na ukabila ni geresha hoja ni siasa, ndio maana Waislamu wanamsema IGP Mwema ambaye ni muislamu kwa sababu ni mchaga na katika wahubiri yuko mchaga na Albert asili yake ni Mkristo, hapo AKILI KICHWANI

Hainishangazi kuwa mkristo anatumika kupinga ukristo au mwislamu anatumika kupinga uislamu, ukweli ni kwamba usicheze na mtu mwenye njaa huwa hatabiriki he/she can go very low for money! Shame on you people.
 
Lakini Mkuu usisahau kuwa in the midst of chaos, kuna order...kama ukiangalia kwa makini!
 
Wakati mwingine kunapotokea tetesi lakini linalobeba ujumbe uzito kama alioutoa Sekenke, yeyoye mwenye data kupinga ama kusupport anatakiwa ajitokeze. Anapokosekana mtu wa kufanya hivyo habari inabakia kuwa tetesi na huishia kwenye udaku.

Lakini akitokea mtu akaunga mkono tena kwa kutoa data kama alivyofanya Mwanakijiji, tunakuwa na majukumu mawili kama wana JF makini. Ama tunatoa hoja kupinga yaliyosemwa au kuyaunga mkono pia kwa kutoa data.

Tusichotakiwa kufanya kama hatuko upande wowote ni aidha kuibeza habari hiyo ama kujaribu kuipinda kwa kuingiza yasiyohusiana na habari. Ni afadhali mara mia kukaa kimya na kusubiri ufafanuzi zaidi kutoka kwa wenye data zaidi.

Wanaobeza ni wazi wanaogopa kwa kuhisi uwezekano wa habari kuwa kweli na wanaojaribu kupindisha ni kwa sababu ya kuhusika kwao na hivyo hawataki habari ifichuke zaidi. Wanaogopa kuumbuka kwa kuhusishwa ama wao wenyewe au ndugu na marafiki zao.

Asante Sekenke na Mwanakijiji kwa kulinda hadhi ya JF ya kumkoma nyani bila kuangalia uso wake na kupambana na uovu bila kujali urefu wa mapembe yake. Ni vema kuzuia kuliko kuponya, a luta continua.
 
Mwanakijiji said:
Miongoni mwao ni mashehe na viongozi wengine wa kidini; baadhi yao ni pamoja na Shekhe Mazinge, Mwaipopo, Said Liko, Chifu Msokwa, Ustaadh Twaha, Dr. Salehe, Abubakar Bonde, Sheikh Amour Jongo, Rajabu Jazba, na Ustaadh Ramadhani. Waliokuwemo kwenye mkutano huo pia ni pamoja na Albert Marwa (inadaiwa ni mtoto wa kulelewa wa Generali Marwa) pamoja na mtu mmoja aitwaye Mtawa (huyu yasemekana ni mtumishi wa ngazi ya Juu ikulu). Walikuwepo baadhi ya watu wengine ambao wanadaiwa kuwa ni maafisa wa Usalama wa Taifa ambao kutokana na sheria hatuwezi kuwataja majina yao.

Mwanakijiji,

..ningeyapuuza madai haya kama jina la Bw.Mtawa lisingetajwa.

..Mtawa amekuwa msaidizi, na mtu wa karibu na Raisi, kwa zaidi ya miaka 15.

..sidhani kama ni vizuri kumhusisha na tuhuma kama hizi bila kuleta ushahidi usioweza kutiliwa mashaka.

..naungana na Game-Theory kuomba kideo cha hilo tukio kwenye You Tube, au kwenye mtandao wa KLH news.

NB:

..naomba sana safari hii msichezee akili za wananchi kama wakati mlipo ule wa kashfa ya Chenge na mambo ya ushirikina bungeni.

..wengi tunapenda mabadiliko nchini kwetu, lakini hatuko tayari kufikia lengo hilo kwa kutumia mbinu za kihuni-huni.
 
Mwanakijiji,

..ningeyapuuza madai haya kama jina la Bw.Mtawa lisingetajwa.

..Mtawa amekuwa msaidizi, na mtu wa karibu na Raisi, kwa zaidi ya miaka 15.

..sidhani kama ni vizuri kumhusisha na tuhuma kama hizi bila kuleta ushahidi usioweza kutiliwa mashaka.

..naungana na Game-Theory kuomba kideo cha hilo tukio kwenye You Tube, au kwenye mtandao wa KLH news.

NB:

..naomba sana safari hii msichezee akili za wananchi kama wakati mlipo ule wa kashfa ya Chenge na mambo ya ushirikina bungeni.

..wengi tunapenda mabadiliko nchini kwetu, lakini hatuko tayari kufikia lengo hilo kwa kutumia mbinu za kihuni-huni.

kama umeshaonaa ni mbinu za kihuni huni, unahitaji kideo ya nini? Kwamba ukiona video ndio utabadili mawazo? Unaomba kideo wewe ili kuthibitisha nini? kama ulikuwa ni mkutano wa kawaida tu na kideo kinamuonesha Mtawa pia au mtu mwingine 'vip' na hakina sauti utaamini nini? Na ukisikia sauti ikisema "milioni tatu, nimetumwa n.k" utataka nini kingine kuthibitisha.

Kwa vile huu ni udaku, hauitaji ushahidi utakufa wenyewe kama udaku mwingine.
 
Wakuu heshima mbele, the dataz

1. Mkutano wa siri wa mafisadi Jumamosi usiku, umeamua kuweka nguvu zote by any means necessary kwa mgombea wa UV-CCM wa Zenji anaiyeitwa Masauni.

2. Mafisadi wamemtumia ujumbe mzito sana muungwan, kwamba ni lazima wapewe nafasi ya katibu mkuu wa UVC-CCM, ama sivyo watajitoa.

3. Leo saa saba mchana ulikuwa mkutano wa wabunge wa CCM, agenda Makamba.

Ahsante na Kwaherini, maana sina access ya mtandao hata huu nimeomba tu kwa mtu.

Respect!
 
Mwanakijiji,

..yale madai yaliyokosa ushahidi ya Chenge na ushirikina ndiyo ninayoita uhuni.

..Bw.Mtawa ni mtu nyeti mno serikalini na sidhani kama ni busara kumtuhumu kiasi hiki bila kutuletea ushahidi wa kuridhisha.

..sisi ambao tuna mapenzi mema na nchi yetu tunaomba huo ushahidi wa kideo unaodai umeuona.
 
Mwanakijiji,

..yale madai yaliyokosa ushahidi ya Chenge na ushirikina ndiyo ninayoita uhuni.

ni ushahidi gani wa Ushirikina ungeweza kukuridhisha?


..Bw.Mtawa ni mtu nyeti mno serikalini na sidhani kama ni busara kumtuhumu kiasi hiki bila kutuletea ushahidi wa kuridhisha.

utaridhishwa na ushahidi wa namna gani ambao utakufanya uamini au ukubali tuhuma dhidi ya Mtawa?

..sisi ambao tuna mapenzi mema na nchi yetu tunaomba huo ushahidi wa kideo unaodai umeuona.

ina maana sisi wengine hatuna mapenzi mema na nchi yetu ila "nyinyi" mnaoomba ushahidi?
 
Wakuu heshima mbele, the dataz

1. Mkutano wa siri wa mafisadi Jumamosi usiku, umeamua kuweka nguvu zote by any means necessary kwa mgombea wa UV-CCM wa Zenji anaiyeitwa Masauni.

2. Mafisadi wamemtumia ujumbe mzito sana muungwan, kwamba ni lazima wapewe nafasi ya katibu mkuu wa UVC-CCM, ama sivyo watajitoa.

3. Leo saa saba mchana ulikuwa mkutano wa wabunge wa CCM, agenda Makamba.

Ahsante na Kwaherini, maana sina access ya mtandao hata huu nimeomba tu kwa mtu.

Respect!

Duh!

taratibu mzeee


Btw
oN A FLIPSIDE sasa mimi namtafuta nambua unazo contacts zake?
 
Mwanakijiji,

..ningeyapuuza madai haya kama jina la Bw.Mtawa lisingetajwa.

..Mtawa amekuwa msaidizi, na mtu wa karibu na Raisi, kwa zaidi ya miaka 15.

..sidhani kama ni vizuri kumhusisha na tuhuma kama hizi bila kuleta ushahidi usioweza kutiliwa mashaka.

..naungana na Game-Theory kuomba kideo cha hilo tukio kwenye You Tube, au kwenye mtandao wa KLH news.

NB:

..naomba sana safari hii msichezee akili za wananchi kama wakati mlipo ule wa kashfa ya Chenge na mambo ya ushirikina bungeni.

..wengi tunapenda mabadiliko nchini kwetu, lakini hatuko tayari kufikia lengo hilo kwa kutumia mbinu za kihuni-huni.

Mzee, kwa hiyo wengine wana mbinu za kihunihuni!!

Ok, naomba utueleze hatua utakazichukua pindi utakapoona kideo na kuhakikisha kuwa waliomo ndio hao tunaowasema! achililia mbali kuwa hujatumia nguvu hizihizi kutafuta ushahidi wa EPA,RICH.....

waberoya
 
Hii habari ndivyo ilivyoripotiwa na Habari Leo:

Habari Leo

Kamati ya Wahadhiri wa dini ya Kiislamu nchini, wamekanusha habari iliyotangazwa na Kituo cha Televisheni cha ITV, iliyodai kuwa kuna kikundi cha dini ya Kiislamu kinachotumika kuchafua jina la mfanyabiashara maarufu na mwanasiasa nchini kwa kutumia nembo ya udini na ukabila.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Chifu Hussein Msopa, alizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, na kutoa tamko la kukitaka kituo hicho cha utangazaji kuiomba kamati hiyo radhi kwa kipindi kisichopungua siku saba kuanzia jana.

"Sisi tulikuwa kwenye mkutano wetu siku hiyo, hatukualika vyombo vya habari tulikuwa tukijadili masuala matatu; OIC, Kadhi na ukabila," alisema Msopa, na kuongeza kuwa katika ajenda hizo, walilazimika kuachana na ajenda mbili ambazo ni OIC na Kadhi kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete aliwasihi wananchi kuiachia serikali masuala hayo.

Alisema kitu cha kushangaza ni pale televisheni hiyo ilipofuatilia kwa siri mkutano huo bila kualikwa, na kurusha mjadala na mawazo ya baadhi ya wajumbe badala ya kusubiri nini kiliamriwa au baada ya kikao, kitu kilichowatia shaka juu ya usalama wao.

Aidha, Mwenyekiti huyo alisema taarifa hiyo ilipotosha umma na kuleta uzushi na uhasama baina ya Waislamu na Wakristo wanaoitakia mema dini hiyo, baada ya kueleza kuwa kikundi hicho kinachotumika kumchafua mfanyabiashara huyo, kinafadhiliwa na mtu aliyejulikana kwa jina moja la Manji.

"Tunatamka kwamba endapo ITV hawatatuomba radhi kwa siku hizo saba… tutahamasisha Waislamu na Wakristo nchi nzima kuacha kutazama taarifa yoyote ndani ya kituo hicho, pia kusitisha ushirikiano wowote wa kibiashara na Kampuni za IPP, na mwisho tutaomba dua na kulaani kituo hicho," alisema Msopa.

Alisema kamwe Waislamu hawataacha kujadili suala la ukabila ambalo linazidi kuota mabawa nchini siku hadi siku, na kufanya baadhi ya sekta na idara za serikali kuendeshwa kikabila na bila ufanisi, sababu zinazopelekea migomo, maandamano na hata uzalishaji na huduma mbovu.

Juhudi za kumtafuta msemaji wa ITV ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa ITV/Radio One, Joyce Mhavile, hazikuzaa matunda, baada ya Katibu Muhtasi wake, kueleza kuwa anahudhuria mkutano, na kwamba hatazungumza na mtu ye yote. Kwa mujibu wa maelezo ya Msopa, taarifa hiyo ilitangazwa na kituo hicho Novemba 3, mwaka huu na kurudiwa siku iliyofuata, pamoja na kuonyesha picha za wahadhiri hao wakihudhuria kikao hicho.

My Take:
Angalia kile wanachotishia kukifanya baada ya siku saba na kile ambacho nilikiripoti jana kuwa kilirekodiwa kabla ya kipindi hicho kurushwa (kwamba uamuzi wa kufanya kinachotishiwa kufanywa baada ya siku saba ulifanyika kabla ya habari hii kutoka hewani- inawezekana vipi?). Je siyo kwamba baada ya siku saba watakukwa wanatekeleza hiki:

a. Kuwaonesha waislamu kuwa Bw. Reginald Mengi na Freeman Mbowe ndio maadui wakubwa wa maslahi ya Waislamu nchini.
b. Kwamba Mengi na Mbowe wana mkakati wa kuhakikisha kiongozi anayekuja ni kutoka kabila la Wachagga. Katika hili la dhidi ya "Uchagga" wanamkakati walikuwa wana uhakika wa kutobughudhiwa na polisi kwenye mikutano ambayo waliipanga kuifanya hasa wakiamini kuwa IGP Said Mwema yuko upande wao. Hata hivyo mmoja wao aliapa kuwa aliwahi kuambiwa na Dr. Nchimbi kuwa Mwema ni Mchagga (sijui kwa upande wa mama) na hivyo wasitarajie sana.
c. Walioleta mpango huo wamemhusisha kiongozi wa juu serikalini kuwa ndiye aliyewatuma kutekeleza mpango huo hasa kuonesha kuwa vyombo vya IPP vinatumika kueneza Ukristu, kukandamiza Waislamu, na kuinua Wachagga. Hili litaelezwa ili Waislamu waanze kuvisusisa vyombo vya habari vya IPP.
d. Kuendelea kuwahusisha Mengi na Mbowe katika vifo vya Chacha Wangwe na Gavana Ballali.

Sasa baada ya siku saba mkisikia habari ni hii itakuwa ni kwa sababu ITV wamekataa kuomba radhi au kwa vile uamuzi huo tayari ulishachukuliwa? Kwanini wasitishie kwenda mahakamani kama wanavyofanya wengine?
 
Mwanakijiji indirectly wewe ndio umewafundisha hilo, meaning wamedesa kutoka kwenye kauli yako.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom