Sekenke
Senior Member
- Mar 3, 2008
- 132
- 29
Wanabodi
Naomba kwa mwenye habari zaidi atufahamishe kuhusu hili.
Katika taarifa ya habari ya jana (3 Novemba 2008) saa mbili usiku, na leo asubuhi (04 Novemba 2008), kituo cha ITV kilionyesha habari ambayo ilionekana kuwanasa jamaa kadhaa bila wao kujua. Maelezo (ambayo hadi sasa sijayaelewa vizuri) ni kwamba hao jamaa wameonekana katika hoteli kubwakubwa jijini (bila kuzitaja), na kwamba walikuwa wakipanga kuwachonganisha na kuwachafua mfanyabiashara-mwanasiasa mmoja na mfanyabiashara flani, kitu kama hicho.
Ilionekana kwamba mpiga picha wa ITV alikuwa kajificha kwenye moja ya vyumba vya juu vya hiyo hoteli akiwachukua bila wao kujua, na akawafuatilia hadi mitaani mabako aliweza kunasa hadi sauti zao. Walionekana wakibishana kuhus kiwango cha pesa walizopewa ili kutimiza kibarua chao, jina la Manji lilisikika mara kadhaa, na kwamba baada ya mikakati hiyo watatawanyika ili kuanza kazi yao ya uchafuzi wa hali ya hewa kisiasa. Baadhi wataanzia Ruvuma (hapo sijui mlengwa), mmoja atabaki jijini kumshughulikia Kawawa.
Samahani kama nashindwa kuielezea vizuri habari yenyewe kwani ilikuwa haijakaa sawa, ndio maana nakuja kwenu na kuomba yeyote aliyefuatilia na kuelewa na mwenye taarifa zaidi atumwagie tuweze kujua nini kinaendelea.
Natanguliza shukrani
Naomba kwa mwenye habari zaidi atufahamishe kuhusu hili.
Katika taarifa ya habari ya jana (3 Novemba 2008) saa mbili usiku, na leo asubuhi (04 Novemba 2008), kituo cha ITV kilionyesha habari ambayo ilionekana kuwanasa jamaa kadhaa bila wao kujua. Maelezo (ambayo hadi sasa sijayaelewa vizuri) ni kwamba hao jamaa wameonekana katika hoteli kubwakubwa jijini (bila kuzitaja), na kwamba walikuwa wakipanga kuwachonganisha na kuwachafua mfanyabiashara-mwanasiasa mmoja na mfanyabiashara flani, kitu kama hicho.
Ilionekana kwamba mpiga picha wa ITV alikuwa kajificha kwenye moja ya vyumba vya juu vya hiyo hoteli akiwachukua bila wao kujua, na akawafuatilia hadi mitaani mabako aliweza kunasa hadi sauti zao. Walionekana wakibishana kuhus kiwango cha pesa walizopewa ili kutimiza kibarua chao, jina la Manji lilisikika mara kadhaa, na kwamba baada ya mikakati hiyo watatawanyika ili kuanza kazi yao ya uchafuzi wa hali ya hewa kisiasa. Baadhi wataanzia Ruvuma (hapo sijui mlengwa), mmoja atabaki jijini kumshughulikia Kawawa.
Samahani kama nashindwa kuielezea vizuri habari yenyewe kwani ilikuwa haijakaa sawa, ndio maana nakuja kwenu na kuomba yeyote aliyefuatilia na kuelewa na mwenye taarifa zaidi atumwagie tuweze kujua nini kinaendelea.
Natanguliza shukrani