S. S. Phares
JF-Expert Member
- Nov 27, 2006
- 2,138
- 88
Hizi dini zitatumaliza. Wewe angalia hata watu ambao ungetegemea wapinge hoja kwa hoja..likija swala la dini wanachanganyikiwa kabisa.
Masanja,
Ubarikiwe, haya maneno ni mazito sana.
Hizi dini zitatumaliza. Wewe angalia hata watu ambao ungetegemea wapinge hoja kwa hoja..likija swala la dini wanachanganyikiwa kabisa.
mhhhh ok
![]()
naona umesahau lile kundi linalolipwa kuwetha threads kwa ajili ya kuwafurahisha wanao walipa pesa....sijui hili ni la pili au lipi?
maana naona kila mtu humu ana interest na of course huwezi kuwakataza watu wasi criticise au wasikubaliane na mawazo yako
mfano tulikuwa na thread humu kuuliza watu kwa nini wanakubali kumwimba Mungu ambaye haluna aliyewahi kumwona wala kutuletea evidence kama yupo mwishowe tukaambiwa kuwa tunapenda kubisha tuuu
And then kuna lile kundi na SUPERMARKET JOURNALISTS ...kundi ambalo naona hujalizungumzia
Wahadhiri wa Kiislamu wainyooshea kidole ITV
Godwin Myovela
Daily News; Wednesday,November 05, 2008 @21:15.
Mkuu heshima kwako, hii habari Mwanakijiji alishaiweka kule kwenye thread yake.
Hii habari ndivyo ilivyoripotiwa na Habari Leo:
Habari Leo
Kamati ya Wahadhiri wa dini ya Kiislamu nchini, wamekanusha habari iliyotangazwa na Kituo cha Televisheni cha ITV, iliyodai kuwa kuna kikundi cha dini ya Kiislamu kinachotumika kuchafua jina la mfanyabiashara maarufu na mwanasiasa nchini kwa kutumia nembo ya udini na ukabila.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Chifu Hussein Msopa, alizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, na kutoa tamko la kukitaka kituo hicho cha utangazaji kuiomba kamati hiyo radhi kwa kipindi kisichopungua siku saba kuanzia jana.
"Sisi tulikuwa kwenye mkutano wetu siku hiyo, hatukualika vyombo vya habari tulikuwa tukijadili masuala matatu; OIC, Kadhi na ukabila," alisema Msopa, na kuongeza kuwa katika ajenda hizo, walilazimika kuachana na ajenda mbili ambazo ni OIC na Kadhi kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete aliwasihi wananchi kuiachia serikali masuala hayo.
Alisema kitu cha kushangaza ni pale televisheni hiyo ilipofuatilia kwa siri mkutano huo bila kualikwa, na kurusha mjadala na mawazo ya baadhi ya wajumbe badala ya kusubiri nini kiliamriwa au baada ya kikao, kitu kilichowatia shaka juu ya usalama wao.
Aidha, Mwenyekiti huyo alisema taarifa hiyo ilipotosha umma na kuleta uzushi na uhasama baina ya Waislamu na Wakristo wanaoitakia mema dini hiyo, baada ya kueleza kuwa kikundi hicho kinachotumika kumchafua mfanyabiashara huyo, kinafadhiliwa na mtu aliyejulikana kwa jina moja la Manji.
"Tunatamka kwamba endapo ITV hawatatuomba radhi kwa siku hizo saba… tutahamasisha Waislamu na Wakristo nchi nzima kuacha kutazama taarifa yoyote ndani ya kituo hicho, pia kusitisha ushirikiano wowote wa kibiashara na Kampuni za IPP, na mwisho tutaomba dua na kulaani kituo hicho," alisema Msopa.
Alisema kamwe Waislamu hawataacha kujadili suala la ukabila ambalo linazidi kuota mabawa nchini siku hadi siku, na kufanya baadhi ya sekta na idara za serikali kuendeshwa kikabila na bila ufanisi, sababu zinazopelekea migomo, maandamano na hata uzalishaji na huduma mbovu.
Juhudi za kumtafuta msemaji wa ITV ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa ITV/Radio One, Joyce Mhavile, hazikuzaa matunda, baada ya Katibu Muhtasi wake, kueleza kuwa anahudhuria mkutano, na kwamba hatazungumza na mtu ye yote. Kwa mujibu wa maelezo ya Msopa, taarifa hiyo ilitangazwa na kituo hicho Novemba 3, mwaka huu na kurudiwa siku iliyofuata, pamoja na kuonyesha picha za wahadhiri hao wakihudhuria kikao hicho.
My Take:
Angalia kile wanachotishia kukifanya baada ya siku saba na kile ambacho nilikiripoti jana kuwa kilirekodiwa kabla ya kipindi hicho kurushwa (kwamba uamuzi wa kufanya kinachotishiwa kufanywa baada ya siku saba ulifanyika kabla ya habari hii kutoka hewani- inawezekana vipi?). Je siyo kwamba baada ya siku saba watakukwa wanatekeleza hiki:
Sasa baada ya siku saba mkisikia habari ni hii itakuwa ni kwa sababu ITV wamekataa kuomba radhi au kwa vile uamuzi huo tayari ulishachukuliwa? Kwanini wasitishie kwenda mahakamani kama wanavyofanya wengine?
Mwanakijiji,
..ningeyapuuza madai haya kama jina la Bw.Mtawa lisingetajwa.
..Mtawa amekuwa msaidizi, na mtu wa karibu na Raisi, kwa zaidi ya miaka 15.
..sidhani kama ni vizuri kumhusisha na tuhuma kama hizi bila kuleta ushahidi usioweza kutiliwa mashaka.
Mkuu
mtu kufanya kazi na mkuu wa nchi kwa muda mrefu hakumuondolei tabia yake mbaya aliyonayo.
Mfano Uganda two weeks ago presidential bodyguard alihusishwa na wizi wa mamilion, Je Museven alimtumaaa?????
mfano mwingine Viongozi wetu waliofanya kazi tangu enzi ya JKN wameonekana kuiba hela za umma na sasa wanapelekwa mahakani, je pamoja kufanya kazi kwa muda mrefu wametumwa na nani. So it is a weak excuse....
Hizo mahakama zetu nazo ni kichekesho kitupu, Watanzania hatuziamini na hata Jaji Mkuu alitamka kwamba Mahakama zimejaa rushwa. Hivyo hakuna uhakika wowote kwamba hao 'mamluki' watatendewa haki na mahakama. Je, kainzi kalidaka udaku? Habari nyeti zina uzuri wake lakini zile ambazo zina mambo ya udini ambayo yanatugawa Watanzania kuliko kingine chochote kile zifanyiwe kazi ili kuhakikisha ukweli wake kwa kupata ukweli toka upande mwingine wa shilingi, vinginevyo mnaweza kukuta JF inaanza kupata sifa mbaya ya kuweka udaku.
Mkuu siku zote ninaheshimu sana mchango wako na nitaendelea kufanya hivyo, lakini kwa hapa umekwenda kusiko, tumeanza lini kutoziamini mahakama kwa kiasi hicho? mbona ulikuwa mstari wambele kutaka mafisadi wa EPA na Richmond wapelekwe mahakamani? au ndo double standards.
Ninachofahamu mimi kazi ya media ni kutoa habari, na hii ni habari tena habari muhimu kwani inahusu mstakabari wa Taifa na watu binafsi. Hivi hatuoni kama kunawatu wanataka kutuingiza kwenye makundi ya kidini na kikabila?. Tukifikia mahali pa kususia bidhaa za mtu/watu kwa misingi ya kidini tutaliharibu taifa ni litaadhiri wafanya biashara wengi hivyo kuhujumu uchumi wa nchi.
Kwa maneno ya huyu mwenyekiti wao kwamba watawaomba Wakristo wasusie huduma za ITV kwa kuwa wametangaza kikao kilichokuwa kinajadili kwa siri mambo ya OIC, kadhi na ukabila mbona kichekesho? si ndo Wakristo watapenda zaidi huduma ITV?
Mambo haya yanahitaji umakini mkubwa, ninadhani hawa Ndg. wamekosa uvumilivu, walichopaswa ni kwenda mahakamani endapo wanahisi kutotendewa haki. otherwise, tunaelekea pabaya.
Ninachofahamu mimi kazi ya media ni kutoa habari, na hii ni habari tena habari muhimu kwani inahusu mstakabari wa Taifa na watu binafsi. Hivi hatuoni kama kunawatu wanataka kutuingiza kwenye makundi ya kidini na kikabila?. Tukifikia mahali pa kususia bidhaa za mtu/watu kwa misingi ya kidini tutaliharibu taifa ni litaadhiri wafanya biashara wengi hivyo kuhujumu uchumi wa nchi.
Kwa maneno ya huyu mwenyekiti wao kwamba watawaomba Wakristo wasusie huduma za ITV kwa kuwa wametangaza kikao kilichokuwa kinajadili kwa siri mambo ya OIC, kadhi na ukabila mbona kichekesho? si ndo Wakristo watapenda zaidi huduma ITV?
Mambo haya yanahitaji umakini mkubwa, ninadhani hawa Ndg. wamekosa uvumilivu, walichopaswa ni kwenda mahakamani endapo wanahisi kutotendewa haki. otherwise, tunaelekea pabaya.
Yebo Yebo,
Naona watu mnazidi kupotosha hoja hapa...
Kwanza kabisa habari imezungumzia waislaam kukutana kuzungumzia maswala ya OIC, mahakama ya kadhi na Ukabilai hiyo ndio tuseme ilikuwa agenda ya mkutano.. Hilo halina taabu kabisa kwangu na wala sio jambo tunalolipigia kelele unless nyie ndicho kilichosumbua... Na nimesema itakuwa ajabu ikiwa kuwepo kwa mkutano huo unaohusu OIC na Mahakama ya kadhi ndio imebeba kichwa cha hoja hiii yaani Mkakati wa Mamluki Wafichuliwa na maswala ya Udini..kwani ni maswala haya nyote huko nyuma wakati tunazungumzia kupitia serikalini mlipinga sana na kudai yabakie ya dini inayohusika... Hivyo maswala haya hayakuwa ktk huo mkutano wa siri..
Niliposoma report ya Mwanakijiji nilijua haikuwa Udini mkusanyiko wa hao viongozi kuzungumzia maswala ya OIC na Mahakama ya kadhi kama mlivyopendekeza isipokuwa kuna jingine lililojificha ndani ya mkutano wa siri ambalo ndilo linaleta Udini..
Hapa ndipo Utata wa habari nzima umeanza na kama utasoma maelezo ya viongozi waliohudhuria mkutano ule wamesema walikutana kweli, hakuna kati yetu aliyesema hawakukutana. Kulikuwepo na Mkutano kweli Ijumaa hakuna aliyepinga isipokuwa kichombezo kilichoongezwa ambacho ndicho kimewaudhi wengi iwe kwa kuunga mkono ama kupinga Utunzi wa hizo hadithi za Mkakati wa Udini na Ukabila walengwa wakiwa Mengi na Mbowe katika maswala ambayo hata sielewi mwanzo wake.
Labda wenzangu mnafahamu vizuri swala hili tuambieni huo Ukabila unamhusu Mbowe na Mengi umeanza wapi? Kama ni Chadema hawa viongozi wa dini sio wanachama na haiwahusu ktk dini kwani hiki ni chama tu... tutajadili sisi hapa JF kwa sababu kuna nafasi ya kutazama pande mbili za shilingi..Ni mjdadala.. Iweje watu wakutane, kisha waandishi wa habari wawafuate hadi Hotelini kwa usiri ikiwa kweli nyie mwenyewe hamna matatizo na mkusanyiko huo!.. Je, ni mara ya kwanza wamekutana? hapana iweje leo iwe swala la kufukuziwa hadi video huku mkidai kwamba wao ndio wadini kufanya mikutano ya siri hotelini na mkajenga hadithi nzima wakati hamkuwepo hata karibu na mkutano huo wa siri!.
Haya naona tena kumezuka swala la Waislaam kususia IPP/ITV, sasa mlitaka wataje chombo gani ikiwa habari hii imetolewa na vyombo hivi, kisha kwa nini mnafikiria anayetakiwa kuomba radhi ni Mengi na sio mwandishi/editor, msemaji/mwandalizi wa kipindi hicho!..Yote hii inatokna ana habari iliyotanguliwa kama jina la Megji lingeandikwa ktk taarifa iliyotangulia mngesema Megji wakati hakuna sehemu hata moja jina la Mengi limetajwa..Hili jina limeibuka wapi kama sio kutokana na hadithi ya Mwanakijiji..
Na kuhusu mahakama, mbona hata Marekani na nchi za Ulaya kuna habari za Uongo hutolewa ktk TV na watu wakataka kuombwa radhi bila kwenda mahakama!..na hata siku moja hakuna mtu aliyefikiria kwamba mlengwa ni mmiliki wa kituo hicho cha habari..Hii sheria ya kwenda mahakamani inatoka wapi? hata mimi kuna watu nimeshaomba samahani ama kuwaambia waombe samahani kwa maneo waliyosema na sikufikiria kabisa kuwa mahakama ndio sheria. Hapa JF kila siku watu tunaombana samahani mbona hamsemi waende mahakamani?.. Jamani vipi akili zetu zinaanza kuganda ama! Inashangaza sana..
Bowbow,
Tunachobishana hapa ni habari ya Mwanakijiji ambaye hana tape wala hajaiona...hilo kwanza.. Pili ukisoma hoja nzingi humu zinazungumzia zaidi mkutano wa OIC na mahakama ya kadhi jambo ambalo hakuna anayebisha isipokuwa kipengele cha kilichoongezwa..
Nimekipinga, wahusika amekipinga na wewe unakiunga mkono wakati hujaiona hiyo Video..wakati huo huo bdio nyie wa kwanza kuomba ushahidi kwa habari yoyote ile leo imekuwa mtuhumiwa a prove innocent hata kama hakuna ushahidi...
Tatu nasdhangaa mnaposema waende mahakamani wakati IPP/ITV wenyewe hawajasema lolote kuhusiana na ukweli wa habari hiyo..
Kwa nini msipate kuhakikisha kwanza kuhusiana habari hiyo kuunga mkono wakati mnajua kabisa Udini ndio tamko zito lililobeba uzito wa mada hii..