Na usisahau kwamba kabla ya Adam walikuwepo wanefili walioishi nje ya Eden. Adam alivyofukuzwa akaenda kuishi na wanefili. Eden ilikuwa Iraq ya sasa
Kabla ya ADAM walikuwepo wengine "pre-adamic humans" au biblia imewaita "gentiles" ambao mpaka kesho wayahudi wanaamini wao pekee ndio uzao wa Adam na sie wengine wote ni pre-adamic humans au watu wa mataifa ambao Mungu aliwakataza wayahudi wasichangamane nao.
Adam alikuwa myahudi na baba wa wayahudi lakini sio baba wa watu wote duniani.
Kama unaamini kitabu cha mwanzo kwenye biblia jiulize swali hili: Kama Adam na Hawa ndio binadamu wa kwanza duniani, wa tatu akiwa Kaini, Je, Kaini baada ya kumuua Abeli alikuwa anawaogopa akina nani kwamba watamuua wakimuona? Unajua kisa cha Kaini kuwekwa alama kwenye paji la uso baada ya kumuua Abeli?
Pia, Kaini alipotoka kwa Adam na Hawa akaenda kuoa, je alioa nani kama hapakuwa na watu wengine "pre-adamic"? Mke wa Kaini alikuwa uzao wa pre-adamics sio uzao wa Adam.
Lakini pia mji ulioitwa mji wa Kaini ulitoa wapi watu wa kuufanya uitwe mji "City of Cain"?
Watu walikuwepo, Adam na Hawa ni waanzilishi wa wayahudi na hizi dini mbili zingine lakini walikuwepo watu wa mataifa ambao hawa uzao wa Adam walikatazwa kuchangamana nao.
Soma j.creation 13 (2):22-30, 1999
Soma j.creation 22 (3):8-13,2000.
Soma assemblyoftrueisrael.com
Mesopotamia, ulimwengu wa leo ni uleule wa jana na juzi.WanaJamii,
Kwanza tumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema na huruma kwa kufika siku ya leo. Nimeona leo tuweze kuelemishana kuhusu biblia na maandiko matakatifu.
Mwenyezi Mungu anasema, watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa. Kusoma biblia ni sehemu ya kujua mambo na kumjua uweza na utukufu wake Mwenyezi Mungu muumbaji.
Swali la leo, ningependa kujua bustani ya Eden ilikuwa wapi katika ulimwengu wa leo? Kwa kifupi tu naweza kusema, wazungu wamepotosha sana khusu hili na kuhusu image halisi ya Mungu wetu pamoja alituumba kutokana na mfano wake; lakni Mungu anaonekana ni mtu mweupe tu.
Kwahyo na mambo mengine nahisi yatakuwa yamepotoshwa kuhusu bibilia tofauti na wenzangu waislam ambao wao vitabu vyao vimebaki kama vilivyo na hadithi zao hazina utofauti na bibilia, tofauti yetu mimi sijui ni wapi!
Hivyo nafungua majadala tujuzane ni wapi bustani ilikuwepo na tutazidi kuulizana maswali pale utata unapokuwa.
Nawakaribisha waislam pia maana wengi wao wanao ufahamu wa kwenye biblia na naomba huu mjadala uwe wa amani..
Edeni haikua duniani bana tusidanganyane hapa
Kwahyo Mkuu mbinguni kunaish nyoka Mzee?Nakubaliana nawe kwa asilimia zote. Hiyo Aden mungu asingeiweka mbali nae kwani walikuwepo watu wake aliowaumba kwa mfano wake na kuwapuliza pumzi yake yaani Adam na Eva. Hivyo kusema Eden ilikuwa mbinguni ni sahihi zaidi. Baada ya kumkosea muumba wao ndio walitupwa duniani. chimbuko la binadamu wote ni hawa watu wawili na kabla ya hapo hakuwepo binadamu mwingine na tusiendelee kupotoshana.
Hahah imebidi tu nicheke si ndio wana historia wanasema fuvu la mtu wa kwanza sijui lilipatikana hapaEdeni ulikuwa Tanzania. Mito minne ni Mto Kagera (kaskazini magharibi, Mto Pangani (kaskazini mashariki), Mto Malagalasi kwa upande wa magharibi na mto rufiji kwa upande wa kusini. Hata fuvu na unyayo wa mtu wa kale vinapatikana Tanzania
Kule yanakozaliwa magaidi?bustani ya eden iko IRAQ,,, kando kando ya mto Tigris and Ephrates,..
Kabla ya ADAM walikuwepo wengine "pre-adamic humans" au biblia imewaita "gentiles" ambao mpaka kesho wayahudi wanaamini wao pekee ndio uzao wa Adam na sie wengine wote ni pre-adamic humans au watu wa mataifa ambao Mungu aliwakataza wayahudi wasichangamane nao.
Adam alikuwa myahudi na baba wa wayahudi lakini sio baba wa watu wote duniani.
Kama unaamini kitabu cha mwanzo kwenye biblia jiulize swali hili: Kama Adam na Hawa ndio binadamu wa kwanza duniani, wa tatu akiwa Kaini, Je, Kaini baada ya kumuua Abeli alikuwa anawaogopa akina nani kwamba watamuua wakimuona? Unajua kisa cha Kaini kuwekwa alama kwenye paji la uso baada ya kumuua Abeli?
Pia, Kaini alipotoka kwa Adam na Hawa akaenda kuoa, je alioa nani kama hapakuwa na watu wengine "pre-adamic"? Mke wa Kaini alikuwa uzao wa pre-adamics sio uzao wa Adam.
Lakini pia mji ulioitwa mji wa Kaini ulitoa wapi watu wa kuufanya uitwe mji "City of Cain"?
Watu walikuwepo, Adam na Hawa ni waanzilishi wa wayahudi na hizi dini mbili zingine lakini walikuwepo watu wa mataifa ambao hawa uzao wa Adam walikatazwa kuchangamana nao.
Soma j.creation 13 (2):22-30, 1999
Soma j.creation 22 (3):8-13,2000.
Soma assemblyoftrueisrael.com
katika kusoma kwangu biblia nililuona hili kuwa watu gani walikuwa upande wa east of eden?Ni baada ya maelezo yako murua umenikumbusha maandiko na sasa nabadili msimamo wangu kwenye mchango niliochangia kwenye uzi huu huu kuwa kabla ya Adam na Eva hawakuwepo binadamu wengine walioishi. Ila nabaki na msimamo ule ule kuwa Eden haikuwepo duniani bali mbinguni aliko muumba. Ni baada ya kumkosea mwenyezi mungu ndipo alipowatupa huku duniani na kuwapa adhabu kali ya kulima na kutobolewa na miiba na Eva kuzaa kwa uchungu. Ubarikiwe sana.
ndio huko huko waliishi adam na evaKule yanakozaliwa magaidi?