Burundi nao waitosa Tanzania!

Burundi nao waitosa Tanzania!

Hatuna haraka sana, ngoja kwanza tumalize oparesheni Kimbunga halafu tupeane vitambulisho vya Uraia.

Baadae tuweke kura ya maoni ili wote tutoe maamuzi kwa pamoja kama tuingie huko au tuendelee kusubiri!

Halafu tukishatoa maamuzi tuyaweke kwenye katiba ili hata aje kutuongoza mamluki wa namna gani asibadilishe kitu!
 
Hakuna ugonjwa mbaya kama ukosefu wa fikra huru, Je wote mnaosupport hao walio tutenga na kuona kuwa mkuru/ watz wana mtatizo mmeshawahi kusoma kitabu cha "An Enemy of the People "? Basi kitafuteni kama mtakielewa na kukipeg kwenye scenario iliyopo hamtabwabwaja kama mnavyofanya.

ni kweli kiongozi 'A minority may be right, a majority is always wrong'
 
Tuachane nao tu hawana mpango wowote hawa jamaa na huo mpango wao hautafika popote.
Nalog off
 
hivi nyie wabongo wenzangu mnaolalamika tunaachwa na wenzetu,Je mpo tayari ku share ardhi,kazi,resources na uongozi na wa EAC wenzenu? Kiukweli hapa tulipo tu na sheria zetu kali bado wageni wanafaidi. suala sio uoga bali ukweli. Mimi binafsi kama raia wa Tanzania sipo tayari.
 
Mkuu Wacha1, muulize GOOGLE atakupa majibu yote.....

Barack Obama: Britain should stay in the EU - Telegraph

EU exit would put US trade deal at risk, Britain warned | World news | The Guardian

BBC News - Brazil 'overtakes UK's economy'

Story za Mchina huwezi kuziona kwenye hizo Media zenu zinazotawala dunia nzima. Wengine tunachambua hadi Media ndogo ndogo za nchi tofauti na huko ndiyo waweza kusikia News za Mchina. Mchina aliingilia hata kuokoa uchumi wa Greece kwa sababu tu EU ikivunjika, Ulaya itakuwa matatani na siyo siri, EU ndiyo soko kubwa sana la Mchina.

Mchina siyo MJINGA kama tunavyomuona hapo Tanzania. Sisi wanatuletea Wadhaifu hadi wanavalishwa bendera ya CCM na Kinana/Nape. Ovyo kabisa hawa wanaoletwa Africa/Tanzania.
Unaweza kutupatia Statistics za uchumi wa UK kuporomoka kwa kiasi unachosema? Je, unaweza kuthibitisha kwamba USA na China waliwashurutisha UK kutoondoka EU?
 
Nalifahamu hilo. Ila bado napata shida moja, ni heri kuwa SAMAKI mkubwa kwenye bwawa dogo au Samaki mdogo kwenye Bwawa kubwa? Anyway, TIME WILL TELL. Kwangu mie tulivyokuwa MAPOPO enzi za nyuma ilikuwa safi sana maana tunakula huku na huku. Hata Mgeruman alipoona majirani za Russia wanamzibia kupeleka Bomba la Gas German, aliamua kulipitisha Baharini na hivyo kuvunja makubaliano ya EU ila wao hawakujali sana na wao wakawa Mapopo. Na kwa sababu tu EU Engine yake ni German na hasa ka mji ka Frankfurt, wengine inabidi wake kimya.
Tanzania siyo kwamba haipo kwenye jumuiya yoyote . Tupo SADC na tuko commited kweli na SADC. Hii EAC imekaa kishabiki mno. Tukijipanga , we wont lose anything. Let them go. After all nchi zote nne na hata South Sudan ziko politically unstable....zitavutana tu. Kila nchi pale imekaa mkao wa kula tu...
 
Mkuu, mie ningelikuwa Rais, ningeliitafuta fedha kwa udi na uvumba na nisingeliiacha hela ya Mrudi na Mrwanda.

Haki ya nani, ningelianzisha Usajiri wa biashara zote za Umalaya, Bangi na Sex. Watengeneza Video, magazeti ya Porn na Sex Shop zote ingelikuwa Ruhusa ila muradi ulipe KODI na upimwe afya yako. Masikini wa Dodoma wasingelijali sana hela hizo zimetoka wapi na wangelinishukuru sana.
Sawa; lakini hiyo ni shinikizo kwa Tz. Sioni mantiki ya kushinikizwa kwa hili; waachwe waendelee na wanalotaka kufanya kwani hao ni ndege wenye manyoya yanayofanana.
 
Tanzania ndo baba lao..waungane wao..tumekidhi vigezo vyote vya kujitegemea
 
Hasira za nini wewe?... ni vibaya mtu akiambiwa arudi kwao? Hakika MUNGU wa Mbinguni atazidi kuuanika uovu wenu. Na huyo shetani mnayemtumikia naye kawachoka maana maovu mnayoyafanya mmemzidi hata yeye! Poor tutsis! Mnatia huruma sana...

Muonee huruma mama yako kwanza.
 
Mkuu, mie ningelikuwa Rais, ningeliitafuta fedha kwa udi na uvumba na nisingeliiacha hela ya Mrudi na Mrwanda.

Haki ya nani, ningelianzisha Usajiri wa biashara zote za Umalaya, Bangi na Sex. Watengeneza Video, magazeti ya Porn na Sex Shop zote ingelikuwa Ruhusa ila muradi ulipe KODI na upimwe afya yako. Masikini wa Dodoma wasingelijali sana hela hizo zimetoka wapi na wangelinishukuru sana.

Kwa kuwa Tz iko kwenye strategic position kwa ajili ya landlocked countries, hakuna haja ya Tanzania kupanic na hiyo mikakata na michakato mingine ya wahalifu. Tanznia inachohitaji ni kuimarisha inftastructure zake kivyake, na kuweka uongozi wa kitaalamu ili ishindane kibiashara na kimataifa; ajishindanishe na matakwa yake. Nina imani kiuchumi na kibiashara kinachoamua ni soko, ubora wa huduma na bidhaa.

Tunachokosea (samahani hasa kwa serikali hii ya CCM) huwa inateka nyara mawazo ya wataalamu kabla hayajafikiwa kwenye mipango mkakakti thabiti. Inajulikana proposals zinapoattract pesa hawa watawala wetu wanakuwa wehu kuwahi kwenye pesa na kuharibu mafanikio ya mchakato. Naeleza from experience. ILA NINA UHAKIKA HAYA YANA MWISHO NA SIKU NJEMA ZA MUNGU HAZIGANDI
 
Mkuu Wacha1, muulize GOOGLE atakupa majibu yote.....

Barack Obama: Britain should stay in the EU - Telegraph

EU exit would put US trade deal at risk, Britain warned | World news | The Guardian

BBC News - Brazil 'overtakes UK's economy'

Story za Mchina huwezi kuziona kwenye hizo Media zenu zinazotawala dunia nzima. Wengine tunachambua hadi Media ndogo ndogo za nchi tofauti na huko ndiyo waweza kusikia News za Mchina. Mchina aliingilia hata kuokoa uchumi wa Greece kwa sababu tu EU ikivunjika, Ulaya itakuwa matatani na siyo siri, EU ndiyo soko kubwa sana la Mchina.

Mchina siyo MJINGA kama tunavyomuona hapo Tanzania. Sisi wanatuletea Wadhaifu hadi wanavalishwa bendera ya CCM na Kinana/Nape. Ovyo kabisa hawa wanaoletwa Africa/Tanzania.

mimi siyo mchumi lakini uchumi wa brazil kuupita ule wa britain ni sawa na uchumi wa china ulivyopita ule wa japan,siyo kwamba chumi za uingereza na japan zimezorota hapana ila chumi za brazil na china zimeongezeka,lakini pamoja na hayo zingatia kwamba brazil ina pop ya watu mill200 wakati britain ni mill60 tu hivyo basi per cap income ya england ni almost mara 3.5 ya ile ya brazil hivyo bado wanainchi wa brazil wana kazi kubwa kuja kufikia standard ya maisha ya england!!!!
 
Wakubaliana kuunda rasimu ya shirikisho la EAC
By James Gashumba, EANA
Arusha, Septemba 20 , 2013 (EANA)- Mkutano wa maafisa waandamizi kutoka Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi wa kuharakisha Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki umekubaliana kuanza kuandaa rasimu ya katiba ya shirikisho hilo.

Kama ilivyokuwa kwa timu ya wataalamu walioandaa Itifaki ya Soko la Pamoja, timu ya kuaada rasimu ya katiba ya shirikisho la kisiasa itajumuisha wataalamu mbalimbali kutoka nchi zote tano wananchama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

''Tumekubaliana juu ya taratibu na jinsi ya kuhakikisha kwamba ipo miongozo iliyowazi juu ya kuandaa rasimu hiyo ambayo hatimaye itafikia katika hatua ya mwisho ya kuundwa kwa shirikisho la kisiasa,'' Waziri wa Serikali za Mitaa wa Rwanda, James Musoni alisema baada ya mkutano wa mawaziri mjini Kampala mwishoni mwa wiki.

Wakuu wa nchi za Rwanda, Kenya na Uganda Juni mwaka huu walikubaliana kuongeza kasi ya kufikia lengo la shirikisho la Afrika mashariki.
Pia katika mkutano uliofanyika Mombasa,Kenya, Agosti mwaka huu, Burundi nayo iliunga mkono hatua hiyo ambayo pia inalenga kuimairisha miundombinu chakavu ndani ya kanda hiyo ya Afrika Mashariki.

Mkutano huo wa Kampala juu ya shirikisho la kisiasa ni wa kwanza wa aina yake ambapo maafisa waandamizi kutoka Rwanda, Kenya,Burundi na Uganda wamehudhuria tangu kikao cha utatu kilichofanyika mjini Entebe, Uganda Juni, mwaka huu.

Mawaziri kutoka nchi mbalimbali wananchama wa EAC waliopewa dhamana ya maandalizi ya shirikisho la kisiasa watatoa ripoti ya hatua iliyofikiwa mbele ya mkutano wa wakuu wa nchi za EAC utakaofanyika Oktoba, mjini Kigali, Rwanda.

Tanzania haimo katika mchakato wa shirikisho
Nchi hizo nne za EAC zinatumia baadhi ya vipembele katika mtangamano wa Afrika Mashariki ambavyo vinaeleza kwamba baadhi ya wananchama ndani ya jumuiya wanaweza kwenda kasi zaidi kuliko wengine katika baadhi ya masuala yanayohusu mtangamano.

Mahakama ya Afrika ya Mashariki (EACJ) ilitoa uamuzi mwaka 2009 kwamba hatua ya aina hii inaendana sawia na mahitaji ya muafaka katika kufikia maamuzi ndani ya EAC.

JG/IM/NI



Kaka Manyerere,

Makala nzuri. Kwa kweli, Muungano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ni muungano uliotuimarisha sana kuichumi na kisiasa hadi ulipovunjika ule mwaka wa 1977. Sasa hivi tunajikongoja kuuleta tena kama wakati ule, lakini kuna vikwazo kadhaa, hasa kwa nchi washirika kutaka kunufaika pia katika muungano huu.

Tukichukulia mfano wa Muungano wa Jumuiya ya Ulaya (European Union), nao umekuwa katika vikwazo vinavyoshabihiana na vya kwetu. Nchi kama Uingereza, Sweden, Norway, Denmark zilikataa kujiunga katika Umoja wa Sarafu (Common Currency), hatua kabla ya Shirikisho (Federation). Umoja wa sarafu ya Euro ni mojawapo ya matatizo yanayokabili chumi za nchi shiriki na kuleta mvutano mkubwa kwa nchi za Euro na imekuwa mojawapo ya ajenda katika kampeni za uchaguzi wa Ujerumani uliofanyika hivi karibuni. Ujerumani imekuwa kama mfadhili na mshirika unganishi japo ya mdororo wa chumi za nchi zinazotumia Euro.

Binafsi, nakubaliana na uamuzi wa waziri wa Afrika Mashariki, Mhe. Samuel Sitta katika kusita kukimbilia katika Shirikisho. Tuangalie tunafaidikaje katika Shirikisho baada ya kuungana katika Ushuru wa Forodha (Custom Union) na soko la pamoja (Common Market). Suala kubwa hapa katika Shirikisho litakuwa ni ardhi, ukiachilia mbali raslimali. Lazima tutathmini haya kawa umakini mkubwa tusije tukarudi tena kama ilivyotokea ule mwaka wa 1977.

Tukirudi kwenye mfano wa Jumuiya za nchi Ulaya (EU), leo hii Norway imenufaika sana na ni tajiri sana katika nchi za Ulaya tofauti na kama ingeingia kwenye Nchi za Umoja wa Sarafu (Eurozone). Wao wamebaki kwenye Eneo la Biashara Huru (Free Trade Area) na wanaenda taratibu katika kufuata hatua za kuelekea kwenye Shirikisho. Norway yenye idadi ya watu milioni tano, ina raslimali kubwa ya gesi na mafuta.

Awali ya yote, miye naona tuko katika mazingira mazuri katika Umoja wa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na Umoja wa Nchi za Maziwa Makuu (ICGLR) kuliko kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Tuzidi kushauriana na kuangalia vipi tutaelekea katika Muungano thabiti wa kiuchumi, kisiasa na kijamii wa Maeneo (Regional Integration) ikiwemo Umoja wa Nchi za Afrika Mashariki (EAC) katika kuelekea kwenye Muungano thabiti na imara wa Afrika (African Union) kama alivyofikiria na kuona mbali, Baba Yetu wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kwa Pamoja, Tunaweza!
 
mi nafikiri tujitoe wao wanataka changu chako chetu chetu wakati wanataka kuingia kwenye shirikisho la kisiasa wanasahau uganda na rwanda haziendweshi kidemokrasia wanataka tubebe hata matatizo yao sisi tuimarishe miundo mbinu yetu,gesi yetu najua tukianza watataka tuwauzie tutafanya kama russia anavyowafanyia jumhiya ya ulaya bei juu au kodi juu bidhaa zao ziingie kwa ushuru wa juu hakuna watu wao wasiruhusiwe kuja kununua mazao bali sisi wenyewe tuuze na pia wasiruhusiwe kumiliki arhi hata kama wataoa au kuolewa na watnzania
 
mimi siyo mchumi lakini uchumi wa brazil kuupita ule wa britain ni sawa na uchumi wa china ulivyopita ule wa japan,siyo kwamba chumi za uingereza na japan zimezorota hapana ila chumi za brazil na china zimeongezeka,lakini pamoja na hayo zingatia kwamba brazil ina pop ya watu mill200 wakati britain ni mill60 tu hivyo basi per cap income ya england ni almost mara 3.5 ya ile ya brazil hivyo bado wanainchi wa brazil wana kazi kubwa kuja kufikia standard ya maisha ya england!!!!
Well said mkuu, alafu watu wanacho sahua ni kwamba Uingereza imewekeza sana nje na waliamisha baadhi ya viwanda vyake kwenye third world countries ambazo mishahara ya wafanyakazi ni ya chini sana ukilinganisha na ya Uingereza kwenyewe, Waingereza wanapelekewa fished goods na ku-export nyingine worldwide. Mtu ukuishi Uingereza ndio utafahamu kwamba watu hawa wana mbinu nyingi sana za ku-maintain living standards zao, ndio maana ikija suala la kutetea maslahi ya nchi yao vijana hawaoni tabu kuingia vitani bila ya kusita au kuhuliza maswali mengi - wana umoja sana.
 
mi nafikiri tujitoe wao wanataka changu chako chetu chetu wakati wanataka kuingia kwenye shirikisho la kisiasa wanasahau uganda na rwanda haziendweshi kidemokrasia wanataka tubebe hata matatizo yao sisi tuimarishe miundo mbinu yetu,gesi yetu najua tukianza watataka tuwauzie tutafanya kama russia anavyowafanyia jumhiya ya ulaya bei juu au kodi juu bidhaa zao ziingie kwa ushuru wa juu hakuna watu wao wasiruhusiwe kuja kununua mazao bali sisi wenyewe tuuze na pia wasiruhusiwe kumiliki arhi hata kama wataoa au kuolewa na watnzania
Mkuu tukitekeleza mapendekezo yako mbona watakuja wenyewe kutuomba msamaha, nilishangaa nilipo elezwa kwamba wa Kenya kwa mfano wanakwenda mpaka Iringa vijijini kununua mazao na matunda! Wananunua vitunguu Karatu alafu wanavi-repack na kuvi-export Arabuni specifically Dubai - tatizo wanatuaona wazubaifu na wanaweza kutu-manipulate wapendavyo kama hatuko makini/macho, binafsi sioni kama Burundi hiko katika mkuo wao wana-attend mikutano yao alright lakini deep down wako commited na Tanzania - hayo ni maoni yangu.
 
mimi siyo mchumi lakini uchumi wa brazil kuupita ule wa britain ni sawa na uchumi wa china ulivyopita ule wa japan,siyo kwamba chumi za uingereza na japan zimezorota hapana ila chumi za brazil na china zimeongezeka,lakini pamoja na hayo zingatia kwamba brazil ina pop ya watu mill200 wakati britain ni mill60 tu hivyo basi per cap income ya england ni almost mara 3.5 ya ile ya brazil hivyo bado wanainchi wa brazil wana kazi kubwa kuja kufikia standard ya maisha ya england!!!!

Ubishi mwingine hauna maana. Uingereza sasa ivi ni wamechoka. Kama unaangalia per capita income basi Saudi Arabia ni tajiri kuliko USA
 
Back
Top Bottom