Burundi nao waitosa Tanzania!

Burundi nao waitosa Tanzania!

Kuna watu umu walisema sisi tujitoe EAC tutaungana na Burundi.nawasubiri mje apa kuchangia
 
Candid Scope,

Siyo kweli hayo unayoyasema. Muingereza kwa sasa anaporomoka si kawaida. Hata huduma zao za kulisha watu bure na kuwapa nyumba sasa wameanza kuzibana. Kiuchumi ameshazidiwa na Brazil na alipotaka kujitoa EU, China na USA walimwambia hata asiote kufanya hivyo.

Kuhusu Swis, hata wao wamejiingiza kimya kimya kwenye Schengen maana walikuwa wanakosa pesa kibao. Kujiondoa kwa Rwanda, Burundi na Uganda, kutakuwa na madhara makubwa sana kwetu na hapo mtu asikudanganye. Labda na sisi tuje tujifanye kawa Waswizi kwa kujiingiza kimya kimya kwenye Schengen na Uganda, Rwanda na Burundi huko mbeleni maana itakuwa na faida kwao na sisi.

Anyway, siasa za Africa zinabadilika badilika kutokana na Rais. Kesho wakija Marais wengine, watagombana na watarudisha ndoa na Tanzania. Inabidi katiba zetu kwanza zibadilike na nchi iwe na msimamo na siyo RAIS.

Sawa; lakini hiyo ni shinikizo kwa Tz. Sioni mantiki ya kushinikizwa kwa hili; waachwe waendelee na wanalotaka kufanya kwani hao ni ndege wenye manyoya yanayofanana.
 
Sisi tunawapenda majirani zetu. Kuna ule msemo kuwa unaweza kumchagua rafiki lakini huwezi kumchagua jirani. Tuwe ndugu,tusibaguane kwa kuangalia pua za watu. Sisi wote waafrika.
 
sijadili takataka kama Burundi na mliochangia hiyo mada check your brain kama sio wale tunawaita viroba
[FONT=century
gothic]Nyani Mkuu siku zote haoni.....Chezeya Kiongozi DHAIFU na
Serikali DHAIFU.
[/FONT]
 
Adui yangu mokala1989 yuko wapi? Eti tutabaki na burundi :heh::heh:. Kwa kifupi, sisi (EAC) tunaogelea downstream, nyie ndo mnaogelea upstream. Mtachoka tu.
 
[Jamaa wanatuona watu wasio makini na very slow kuchukua uamuzi,mtu asikuongopee hawa jamaa wako fast kupita maelezo when it comes kwenye business.
Sisi tutakalia kulalamika tu wakati jamaa wanachupa,tuache uswahili TUKANYAGE TWENDE.
 
Kikwete apunguze umbea kwa mataifa makubwa! Kutumika tumika tu. Majirani wanatuchukia kwa sababu hiyo

Kuna wakati Kikwete alikuwa Marekani, akazungumzia kuhusu matatizo ya Kenya, serikali ya Kibaki ikachukia kuwa kwanini kana alikuwa na kitu cha kuzungumza kuhusu matatizo ya Kenya asiongee na viongozi wa Kenya bali akasubiri akaenda Marekani na kuongea na wamarekani kuhusu matatizo ya Kenya. Ndio ntindo wake.
 
Tanzania tunahitaji katiba imara kwanza,hayo mengine yatafuata,
Muungano na z'bar tu unasua sua,huo wa nchi zaidi ya 4 tutauwezea wapi
na viongozi wetu hawa..
 
Kwa sasa hivi mustakabali wa Tanganyika na Zanzibar unahitaji kipaumbele. Watanganyika wapate nafasi ya kuamua juu ya ardhi yao na rasilimali zilizomo.
 
Mmoja katia majadiliano amabayo yanajadiliwa katika shirikisho la EAC ni free labour movement , Tanzania haitaki kuiharakisha ,maana hilo likikukbalika tutavamiwa na Wakenya na Waganda,sasa huyo mnayomwita "Dhaifu"mnaonaje alikubali???
 
Kuna wakati Kikwete alikuwa Marekani, akazungumzia kuhusu matatizo ya Kenya, serikali ya Kibaki ikachukia kuwa kwanini kana alikuwa na kitu cha kuzungumza kuhusu matatizo ya Kenya asiongee na viongozi wa Kenya bali akasubiri akaenda Marekani na kuongea na wamarekani kuhusu matatizo ya Kenya. Ndio ntindo wake.


Hiyo pia haitoshi Mkuu. Kwa nini asiongelee matatizo ya kwake? Zanzibar wanataka kutuacha, na hoja yao ina nguvu, ingawa haitoi sababu zote za hasira.

Kuna mchambuzi rafiki yangu kanikuna sana leo; Zanzibar wanaona hali ya uchumi wa nchi yetu haijakaa vizuri. Mfumuko wa bei upo juu, na moja ya sababu za hali ya uchumi kuwa mbaya ni Ujinga unaoitwa RUSHWA. Umewahi kusikia lini Watu wanakula rushwa Zanzibar? Tuna makanisa rundo hapa bara; na watu wa serikalini humohumo wanajifanya wanasaaaaali, halafu nchi inanuka rushwa. Zanzibar wanaona wapo katika ndoa na watu wachafu katika roho zao. Kwa nini hii topic Kikwete asiijali anapokuwa huko marekani?

Kikwete aongelee RUSHWA katika Tanzania. Aachane na vibanzi kwenye sura za wengine akiacha boriti usoni pake. Uchumi Unaendeshwa Vibaya, Rushwa imeharibu nchi. Mataifa hayapati heshima kwa idadi ya vijembe kwa majirani. Mataifa yanapata heshima kwa kujenga uchumi na majeshi imara. Na cha kwanza ni Uchumi.
 
Sio majirani tuu wanatuonea jealous hata mataifa ya nje
Utajiri ulioko Tz unatisha
Inahitaji tuamke tuu watz tutumie hizi fursa
hao majirani wanatapatapa tuu hawana lolote
Hatuhitani ndo za mkeka!!!!!!!

Wabongo bwana kwa kujifaragua - hatujambo! Hizi taarabu za "wanatuonea wivu tena wa kike" ambazo tumejizoesha kwenye majukwaa ya siasa: CCM vs CDM vs CUF haziwezi kutupeleka mbali mkizileta katika masuala muhimu ya ushirikiano wa kiuchumi. Wenzetu wanachanja mbunga sisi tunabakia kuimba taarabu kwa vile ndio mtazamo wa mkuu wetu wa kaya. Kama amezungukwa na washauri wenye fikira kama hizi na yeye ndio hivyo basi twafwaaaa. Baada ya miaka hamsini, Watanzania watakuwa wanakwenda nchi jirani kutafuta vibarua vya upagazi.
 
Kwa hili la ARDHI kwakweli majirani zetu endeleeni tu na umoja wenu hakuna tatizo kabisa na tunawatakieni kila la kheri!Kwasasa tu Manyang'au waki-kikuyu hawajaingia kubeba mahekari achilia mbali wanyankole na watutsi watakaoingia na makundi ya maelfu ya mifugo kujitwalia Ardhi yetu, migogoro kati ya wafugaji na wakulima inatupeleka putaputa sasa tukiruhusu na hawa wengine waingie patakalika kweli humu?

Ilimradi uwepo wa umoja wao huo wa kisisasa ndani ya EAC hauifutii kabisa uanachama Tanzania basi sisi tutaendelea tu kuwepo kuwepo kwanza.
 
Hatuwezi kujadili mada nyingine. Mbona hili tumeshalijua kuwa hawa jamaa wameanza kimpango wao??
 
Wako fast kuliko maelezo kwenye business right,
Well this is political integration,
Mfumo kwanza wapaswa kuwa sawa alafu ndio kuwa fast kuliko maelezo kwenye business,
Otherwise mbele ni kiza ndugu,
Our government is right.
 
Nyie mbona hamfatilii, ushirikiano wa kiuchumi ambao hatutonufaika nao?
Viceversa is true, wao ndio wataokuja kuomba kazi huku tena.na vibali
 
Back
Top Bottom