Burundi nao waitosa Tanzania!

Burundi nao waitosa Tanzania!

Muruto unashabikiaaaaaa, umefuraaaahiiiii,
Hata burundi wakienda kweli kwan tatizo ni nini
 
Rafiki yako mokala1989 yuko wapi? Amekukimbia? Amesoma alama za nyakati.

Mnatia huruma sana! Mnaongea kwa hasira kuonyesha how desperate you are! Mrudieni MUNGU, mziache njia zenu ovu. Yeye ni wa rehema atawasamehe..
 
Mnatia huruma sana! Mnaongea kwa hasira kuonyesha how desperate you are! Mrudieni MUNGU, mziache njia zenu ovu. Yeye ni wa rehema atawasamehe..

Nani anaongea kwa hasira? Nimekuuliza swali mbona hujibu? Wewe juzi juzi si ulikuwa unasema warundi watawafuata? Sasa na burundi nao ni "bahima empire"?
 
murutongore........hizi zao nin tabia za msichana mwenye hajavunja ungo!...SA watawamaliza (SA makes all economic decisions kwa SADC!) China imeingia and i hear wanakuja with everything (as investors they are supposed to atleast boost local economy) hata mpishi wa chai ni mchina! aaaargh! now Obama wants a piece ....where there is keen western interest chungeni! dont be fooled..TZ maybe ver rich and so is Nigeria with oil, Congo with minerals, etc mmm...my brothers msidanganyike ..tanganyika na zinj zahitaji warwanda, waganda warundi na wakenya!

Wafanyabiashara wote wanataka faida iwe Wachina, Waamerika au Wakenya. Hata Kenya siyo mbinguni watu kumi tu wanamiliki ardhi yote ya Kenya na mnafikiri mna akili kutuzidi, gawaneni kwanza hiyo ardhi mliyoporwa na Kenyata na Karume Njenga ndiyo mfikirie hiyo ya kwetu. Tutaendelea kufanya biashara na Wakenya, Uganda, Rwanda , Burundi na wengine kama majirani kwa sababu tunategemeana. Ukitaka kumpandisha mtalii mlima Kilimanjaro lazima tu afike TZ, hakuna Ngorongoro Uganda wala Rwanda, wala hakuna Bwindi Tanzania. Mkizalisha mahindi kama tuna njaa tutanunua tu vilevile nayi pia mtanunua, kifupi tunahitajiana hakuna aliye bora kuliko mwingine. Acheni chuki isiyo na sababu mnao marafiki wengi nasi tunao wengi ambao tunafanya biashara nao, wakati mlipopigana wakati wa uchaguzi wafanya biashara marafiki tuliwakopesha pesa na hata wengine hawajarudisha lakini bado tunaendelea kuwachukulia kama ndugu. Hiyo fitna ya Kagame haitadumu sana kwani hakika mtu mwovu hatakosa adhabu.
 
Candid umesema ukweli
mimi sioni sababu ya kuhangaika na hili shirikisho
Mfano mwingine mzuri ni Norway haipo kwenye shirikisho la nchi za ulaya
wanatumia sarafu yao wenyewe na uchumi wao uko imara sana
shirikisho la nchi za kusini inatosha waache hao wanaoitaka ardhi yetu kwa vitisho watapetape tuu

You are not serious! Unalinganisha Norway na Tanzania iliyojichokea?
 
Kuna wakati Kikwete alikuwa Marekani, akazungumzia kuhusu matatizo ya Kenya, serikali ya Kibaki ikachukia kuwa kwanini kana alikuwa na kitu cha kuzungumza kuhusu matatizo ya Kenya asiongee na viongozi wa Kenya bali akasubiri akaenda Marekani na kuongea na wamarekani kuhusu matatizo ya Kenya. Ndio ntindo wake.

Kikwete ni mswahili na tabia za waswahili unazijua! Tembelea Tabora, Ujiji, Bagamoyo, Tanga utazijua tuu!!
 
Nchi kutengwa na majirani si takataka kama unavyotaka tuamini. Kibwagizo ni kwamba wanataitaka ardhi yetu, lakini ukweli ni kwamba tuna uongozi ambao ni dhaifu katika kila nyanja ya utendaji hivyo hutafuta upenyo wa kutokea. Tungekuwa na uongozi madhubuti ardhi yetu wasingeigusa na kamwe wasingethubutu kututenga. DHAIFU ndani ya nchi na DHAIFU pia nje ya nchi ni janga la Kitaifa.


sijadili takataka kama Burundi na mliochangia hiyo mada check your brain kama sio wale tunawaita viroba
 
Obviously sterling ktk sarakasi hizi za EAC ni nyang'au, hawa wengine wenzangu na mimi sidhani kama wanajua kinachoendelea #mazuzu . Tz bado tuna fursa ya kuwa na uongozi imara na wa kizalendo ambao utasaidiana na serious investors kwene hot cakes za karne hii ktk mambo ya kilimo cha kisasa (food security), energy na madini. EAC yao haiezi kufua dafu mbele ya mipango thabiti kuhusu mambo niliyoyataja. Hatuna haja ya kuwakera na kuwakebehi na EAC yao, bali tuketi kitako na kuangalia bigger issues, ambazo tukichomoka wataishia kuona vumbi tu.
 
Nani anaongea kwa hasira? Nimekuuliza swali mbona hujibu? Wewe juzi juzi si ulikuwa unasema warundi watawafuata? Sasa na burundi nao ni "bahima empire"?

Sijawahi ongelea habari za burundi. Lbda unitumie hiyo comment...
 
Candid Scope,

Siyo kweli hayo unayoyasema. Muingereza kwa sasa anaporomoka si kawaida. Hata huduma zao za kulisha watu bure na kuwapa nyumba sasa wameanza kuzibana. Kiuchumi ameshazidiwa na Brazil na alipotaka kujitoa EU, China na USA walimwambia hata asiote kufanya hivyo.

Kuhusu Swis, hata wao wamejiingiza kimya kimya kwenye Schengen maana walikuwa wanakosa pesa kibao. Kujiondoa kwa Rwanda, Burundi na Uganda, kutakuwa na madhara makubwa sana kwetu na hapo mtu asikudanganye. Labda na sisi tuje tujifanye kawa Waswizi kwa kujiingiza kimya kimya kwenye Schengen na Uganda, Rwanda na Burundi huko mbeleni maana itakuwa na faida kwao na sisi.

Anyway, siasa za Africa zinabadilika badilika kutokana na Rais. Kesho wakija Marais wengine, watagombana na watarudisha ndoa na Tanzania. Inabidi katiba zetu kwanza zibadilike na nchi iwe na msimamo na siyo RAIS.

Tanzania siyo kwamba haipo kwenye jumuiya yoyote . Tupo SADC na tuko commited kweli na SADC. Hii EAC imekaa kishabiki mno. Tukijipanga , we wont lose anything. Let them go. After all nchi zote nne na hata South Sudan ziko politically unstable....zitavutana tu. Kila nchi pale imekaa mkao wa kula tu...
 
Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki halitafanikiwa, labda kama wanazungumzia 'loose confederation' kama ya European Union. Swala la shirikisho halitaweza kuhusu 'sovereignty' ya nchi washirika. Mimi sioni ni kwa namna gani washirika (Kenya, Uganda na Rwanda) watakubali kukabithi uhuru wao kwa serikali ya shirikisho. Ni maneno ya wasioelewa wanachosema, wakiongozwa na Museveni. Sisi watanzania tunajua matatizo ya unyumba wa ndoa ya Tanganyika na Zanzibar, sasa fikiria shirikisho la kisiasa la nchi 5. Kunauwezekano hili swala la shirikisho likavunja EAC, kwa maana nchi zikishaanza kugombana sioni ni jinsi gani EAC itapona. Ambacho tunatakiwa tulenge ni shirikisho la kiuchumi, jambo ambalo mpaka sasa Tanzania imekuwa ikiburuza miguu. Watanzania ni lazime tuwe jasiri na tukubali kushindana kibiashara na jirani zetu wa Afrika ya Mashariki.
 
Kama kweli Burundi wamejiunga na hawa inabidi tujichunguze kwanza,Kwanini wote 4?Kuna tatizo kubwa sana pengine kifikra au kiutendaji!

Tuangalie kwanini wenzetu wametugeuka?Then hizo sabau zao tupime tujue kama kweli.Tusichukulie kila kitu kwa mtazamo HASI,
 
Exactly the same scenario happened with Rwanda. Ila kagame huwa hamung'unyi maneno. Anakupa hapo hapo.

Kwani alifanya nini zaidi ya kukenua meno Uganda kwenye mkutano. Na sasa mpo mnalia na illegal immigrants wenu. We will expel all of them, they have been living in our for decades illegally with their animals; something not possible in your country!
 
Huwezi kuwa na social-political sustainability and economic development kwenye mazingira ya kisiasa na kiuchumi yanayobadilika badilika kila mara.

Hatuwezi kuwa na sustainability integration kati ya nchi katika maswala ya kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa kutegemea hisani ya Rais atakavyo amuka siku hiyo katika decision making.

Kama kweli tunataka shirikisho hai na endelevu, We need to look beyond Pres. Kagame na Mseveni tenure kwa sababu nchi zao bado shaky kisiasa na huku wao wakiwa ndiyo absolute decision making, katika hali hii inabidi kujiuliza maswali yanayotufanya kuwa kwenye EAC.

Tanzania tutakuwa tunafanya makosa kama hatuwezi kujifunza makosa yaliyotokea kwenye jumuiya ya zamani ya Afrika mashariki ikichukuliwa kuwa, kitakachoziunganisha nchi za EA ni uchumi na kitakachozisarambatisha ni siasa.
 
Tz mna gundu ama viongozi wenu hawashirikishi halmasauri ya vichwa vyao?
 
Back
Top Bottom