Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 944
BUPE MWAKANG'ATA - AHOJI UJENZI BARABARA INAYOPITA MBUGA YA WANYAMA KATAVI
MASWALI NA MAJIBU BUNGENI
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Rukwa Mhe. Bupe Mwakang'ata katika kikao cha bajeti Bungeni kwenye kipindi cha maswali na majibu ameuliza swali lililoelekezwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.
"Ni lini Serikali itajenga Barabara ya kutoka Lyazumbi inayounganisha Mkoa wa Rukwa na Katavi kupitia mbuga ya wanyama Katavi"? - Mhe. Bupe Mwakang'ata
"Barabara hii ni Barabara kuu, lakini kabla ya kujenga Barabara hii tumeanza kujenga Barabara ya Kiji Kibaoni kwenda Itarike, kwa sababu Barabara zinakwenda sambamba baada ya kukamilisha tutahamia Barabara inayopita katikati ya Mbuga ya wanyamapori ya Katavi" - Naibu Waziri Ujenzi na Uchukuzi