Bungeni: Mwigulu Nchemba achafua hali ya hewa!

Bungeni: Mwigulu Nchemba achafua hali ya hewa!

Naomba kutoa hoja kwa JF management, nadhani huu si wakati wa kuwa na wanachama wenye akili kama za Mwigulu, ni aibu kwa forum yetu. Naomba kutoa hoja apigwe life time ban.
 
Tundu Lisu anaanza kampeni ndani ya bunge na kuanza kutukana ovyo anaomba kura kwa wananchi ndani ya mbunge!! badala ya kujikita na mjadala wa budget. sipendi wanachofanya wabunge wetu tena ni aibu wamegeuza bunge kama bar.
 
Jaziba na chuki alionyesha Mwigulu kwa CDM siwezi kataa sasa kwamba huyu jamaa amekua anashiriki matendo machafu dhidi ya upinzani. Kuonyesha ujinga na utovu mkubwa wa nidhamu ni pale alipo rusha/tupa hotuba ya kambi ya upinzani. Hana tofauti na yule jamaa wa Uamsho Zanzibar alivyofanya mbele ya Waziri Sitta.
Mwigulu anajua ana tuhuma ya mauaji kule Arusha kwa hiyo ni lazima aonyeshe ana mapenzi ya dhati na ccm. Anataka ccm iweke mkono wake mahakamani!!!
 
Silly Season hasa kwa wabunge wanaounga mkono hoja kwa 100%
 
Jamani pamoja na matusi yote hayo kwa mwigulu tafadhali hebu nijuzeni hoja ya gari aliyoitoa Mwigulu kwa maana ya gari analo tumia mbowe ikoje? ina majibu au ni hoja ya kupika hebu tuanzie hapo tunapojadili wehu wa mwiguli ili nami pia niweze kuona kweli Mwigulu ni mwehu vinginevyo niungane na wote wanaoamini kuwa kawashika pabaya!
 
Nimesikiliza Bunge la budget kweli lugha zinazotumika mwisho wake naona nchi yetu inaelekea kubaya sana kwa mtu aliyesikiliza bunge na leo jioni utakubaliana na mimi kabisa kuwa maadili ndani ya waheshimiwa wa bunge imeisha na hawajui kama wananchi tunawasikiliza na sii hivyo tu hata nchi za nje wanasikiliza nini kinaendela ndani ya bunge letu. Swali kweli tutafika?

watu watatukanana,,,na hakuna hatua zitakazochukuliwa,,,,yaan hilo litatokea,na makinda bunge la safar hii LITAMSHINDA,
why???.kwa sababu wabunge wa vyama vyote wana JAZBA(CCM+CDM),Pili wabunge wengi ni vijana(busara F),then kila mbunge anataka asikike na aonekane na apate coverage(kesho gazeti la uhuru na tanzania daima) unadhan yataongelea nini????unadhan HEADING ZITAKUWAJE????basi matus ya NGUON YATASIKIKA MDAU,,,,,SUBIRI LUSINDE AJE,na si bungeni tu,hata kwenye wall za fb za waheshimiwa hawa tutasoma mengi sana(kwa wale wanaowafatilia kwenye wall zao)
 
Mwigulu nilikuwa sijawahi kumsikia live .kumbe ndivyo alivyo ,ama kweli ccm imekwisha' Lisu alijua jamaa anafuata kuchangia ,aka rusha kigongo jama akaanzakuto povu kama nguruwe.
 
Naona kuna haja ya kuweka semina maalumu kwa wabunge otherwise heshima hamna. Wengine naona wapo kiushabiki kuliko uhalisia..mtu kama Komba anaisifia budget alafu baadaye anasema jimbo lake ni maskini na limesahauliwa katika maendeleo ya nchi sasa sijui alikuwa anamaanisha nini. Alafu busara na hekima yake ni sifuri pale anapodai wabunge wanatakiwa kupimwa akili coz wengine walikosea walitakiwa wawe Mirembe.. lakini kwa upande wangu nikifanya tathmini yangu Komba alitakiwa awe wa kwanza kuwa Mirembe kutoka na vapour anazoongea bungeni

jaman sasa komba na lusinde nani amuuguze mwenzie
 
Nashukuru sana bunge hili linarushwa live kupitia tv pamoja na radio ili kuwapa watanzania fursa ya kujua nani ni mtetezi wa maslahi ya taifa na nani ni mtetezi wa unyonyaji.
 
Jamani pamoja na matusi yote hayo kwa mwigulu tafadhali hebu nijuzeni hoja ya gari aliyoitoa Mwigulu kwa maana ya gari analo tumia mbowe ikoje? ina majibu au ni hoja ya kupika hebu tuanzie hapo tunapojadili wehu wa mwiguli ili nami pia niweze kuona kweli Mwigulu ni mwehu vinginevyo niungane na wote wanaoamini kuwa kawashika pabaya!
Uzushi wa Mwigulu muulize katibu wa bunge! Mbona huulizi jambo hilo lingeboresha vipi bajeti mbovu ya serikali?
 
Ningefurahi sana kama Mwigulu angekuja hapa JF na kutueleza uzuri ya budget ya CCM. I want to hear from this first class economist why should people support ccm budget and not the alternative budget by the opposition camp?

Lakini pia ningetaka kujua kwa nini serikali isiweke bayana what is in the OC?
 
Niko katani kwa Nchemba Kyengege maji tatizo sugu Mugundu hali ni mbaya wanasaidiwa na mto makata na mzanga huko kijijini kwake Makunda unaogopa kuomba maji utapewa yenye viluilui halafu wewe umekalia matusi bungeni nenda kajiunge na mzee Yusufu kwenye mipasho tuachie iramba yetu mwisho mungu akujalie maisha marefu usuhudie mtakavyo angukia pua
 
watu wanatafuta umaarufu kwa wapiga kura wao wanapopata njia ya kupitia basi inakuwa taabu.
 
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI!!
Jamani eti Bungeni kuna wasomi!*

Nimemuangalia kiumbe aitwaye Mwigulu akibwabwaja. Pia nimemsikia Tundu akitumia neno 'silly.' Neno hili silly hutumika sana nchi za magharibi wakati wa uchaguzi kwamba ni silly moment. yeye kaamua kusema wakati wa bajeti ni silly time.

Ubaya mkubwa wa Lisu ilikuwa kuanza kushambulia moja kwa moja CCM badala ya kuishambulia bajeti ya hovyo iliyo bungeni ili angalau apate kuungwa mkono na baadhi ya wana CCM. Wapo wengi tu wasiyopenda ujinga kama huo ulioletwa bungeni.

Tatizo la Mwigulu naona hajapata exposure ya kutosha dunia hii. Hana mifano ya kweli, alichonacho ni theories za mambo aliyoyasoma darasani. Anadhani yanamsaidia kujadili bajeti bila fahamu kwamba shida ya mwanakijiji siyo supply-demand curve.

Hili ni tatizo linaloongezeka kwa watu wengi wenye viji-digrii vyao pale bungeni. wanajisahau na kuanza swaggers za taaluma zao wakidhani ndo umaarufu. Kwa mtu kama Mwigulu naona hakuzoea kushangiliwa maana aliposhangiliwa ndo kabisaaa! akaongeza manjonjo kama mcheza mdundiko. Nikimuangalia hana jipya zaidi ya theories za vitabuni na internet. Amejiita senior economist wa bank kuu. Mimi mara moja nika google jina lake kama limewahi kuchangia uelewa wowote wa uchumi dunia hii. Wapi! nimejisemea mwenyewe, rubbish Mwigulu

Ndo maana sasa wakaingia na akina Komba kwa kudhani kushangiliwa ndo kufanya vizuri.*

Mwigulu,*Komba, et al., nawaomba waache kusubiri kushangiliwa. Hakuwapi lolote katika jamii. Kuna watu bungeni wana taaluma ambazo wakizitumia hakuna hata atakayewaelewa.
 
Hamna siku niliyoshikwa na hasira wakati naangalia Bunge kama leo.......................baadae zimepoa baada ya kufurahia matokeo ya ujinga wa Mwigulu na Komba za kuzidi kujifunua mbele ya Watanzania my advice to you Mwigulu LN Nchemba and co ni kutiririkaaaaaaaa muwajulishe wengi zaidi how weak you are though mnakuwa na tambo za kitoto..............SILLY is your middle name now
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom