Bunge Lisirushe Matangazo yake 'LIVE' - Nape

Bunge Lisirushe Matangazo yake 'LIVE' - Nape

NIMEYATOA HAYA KWENYE WALL YA FB YA NAPE.

"Naunga mkono juhudi za kulifanya bunge letu liwajibike zaidi kwa wananchi na kuwa na heshima zaidi. Lakini naamini kutolionyesha "live" si moja ya juhudi hizo!
Lakini ni muhimu kujadili pia muda wa kurusha bunge ambapo wananchi wengi wanapata muda wa kuliangalia badala ya utaratibu wa sasa ambapo naamini watu wengi wapo/wanapaswa kuwa kazini."
 
Hivi haya mawazo ya kipuuzi yanatoka kichani kwa mwanasiasa msomi?Hivi Taarifa ya habari na vipindi vinavyoonyeshwa na TBC muda wa kazi vinawalenga akina nani hasa?

Kanuni na sheria zipo kama Bunge linavunjiwa heshima kanuni zitumike.Wabunge wanatunga sheria lakini bunge linashindwa kutumia sheria na kanuni kujiongoza?

Ukiona mmefikia hatua ya kupingana na teknolojia na tunarudi enzi zile za zamani kwa ajili ya maslahi ya kichama na kuwanyima wananchi haki karne hii ujue hiki ni kifo kibaya kinawanyemelea.
 
hao wasioenda kazini au maofisini unafikiri huwa wanazubaa ndani kuangalia bunge?kwa taarifa asilimia 80 ya nyumba mda huu ziko empty,au wapo mahousgal au wamama wa nyumbani na wako busy wanafanya usafi,kupiga deki kuosha vyombo,kufua,kuenda sokoni,kuandaa mlo wa mchana etc.
Wanaongaliaga TV mida kama hii hawazidi 5000 nchi nzima.

Wacha urongo na hizi theorem zako za kimagumashi. Unawaza kama wanavyowaza wanaccm wengine nilidhani wewe utakuwa wa tofauti.
Mimi niko ofisini lakini kila siku naangalia bunge nikiwa ofisini session ya asubuhi, ya jioni ndio naiangalia nikiwa nyumbani. Nafahamu maeneo mengi ya kazi yenye television set ambapo wakati wa bunge kila mtu anapenda na huangalia vipindi hivyo vya bunge.

Hayo mahesabu yako ya watu wasiozidi 5000 umeyapata wapi? maeneo ya kariakoo tu wanaooangalia bunge ni zaidi ya hao 5000 unaowataja.
 
Hii ni kuthibitisha kwamba uamuzi wa kutaka bunge lisionyeshwe live umefanywa na ccm na katibu wa bunge ndugu Kashilila ameutangazia umma maamuzi ya ccm kwa mgongo wa ofisi ya bunge.
Nape Nnauye anachekesha sana tena huyu bwana mdogo ni wa kuhurumiwa. Yani hajui kwamba kuna watu wengi sana wanafuatilia bunge? ni ukweli kwamba wananchi wengi wanafuatilia bunge na ndio maana wamekuwa mstari wa mbele kukosoa mwenendo mbaya wa uendeshaji wa vikao vya bunge hasa kwa vitendo vya spika na naibu wake kusigina kanuni kukipendelea chama chao.
mkumbusheni kuwa kipindi cha jioni huanza saa 11 jioni hadi saa moja hao wa maofisini huwa wameshatoka, halafu wametuambia huu mfumo wa digital tv tutaona kupitia simu zetu kwa hiyo tutaaccess bunge waache uoga, wanatuthibitishia kuwa ni kweli mbunge 1 wa cdm ni 10 wa ccm
 
Nape akipata wasaa, asome tena hiyo nukuu aliyotoa kwenye gazeti la Nipashe. Inamvunjia heshma - yeye Nape- na pengine ni vema , in the future, akavuta pumzi na kutulia kabla ya kuongea na waandishi wa habari.

Kuonesha ni jinsi gani Nape amelikoroga, anasema: 'anaunga mkono jambo lolote linalota heshma kwa bunge'. Lakini anaendelea kwa kusema kuwa bunge linarushwa 'live' wakati wa asubuhi, na wakati huo (kwa maoni ya Nape) watu wako makazini, hivyo hawana muda wa kufuatili'

Kwa maneno mepesi sana, Nape anataka watu waazima na akili zao waamini kuwa kuonesha vikao vya bunge live- asubuhi kunalivunjia heshma bunge! Hii ni hadithi ya ajabu kabisa toka kwa Nape, na ndio maana nashauri asome tena nukuu yake ili aepushe chama chake na taifa kwa jumla na haya masimulizi ya kuanga-unga.

Heshma ya bunge haina uhusiano wowote na kurushwa live asubuhi, mchan, jioni au usiku wa manane. Kama bunge linaendeshwa kihuni kihuni, bila kufutata kanuni na taratibu zilizowekwa, usitegemee heshma. Kwa bahati nzuri tunayo mifano halisi. Bunge la Tanzania lilipata hesham kubwa wakati wa Spika Sitta. Na hii ni kwa sababu ya uelewa wake na kuheshimu utawala wa sheria lakini pia kuelewa kuwa bunge ni mhimili huru na wa muhimu kwa uhai wa taifa. Sitta aliongoza bunge kwa HAKI.

Makinda, kwa sababu anazozijua yeye, licha ya kuwa Naibu Spika wakati wa Sitta, amerudisha nyuma hatua zote tulizofikia, kama taifa kwenye suala zima la utawala wa sheria. Bunge haliwezi kuwa na heshma kama anayeongoza haelewi 'equation' ya heshma ya bunge inajumuisha nini? Bunge haliwezi kuwa na heshma kama mkalia kiti cha Spika anavuruga kanuni, taratibu,tamaduni/desturi zilizowekwa kuongoza bunge? Ukisshavuruga kanuni maana yake unaruhusu 'chaos'. Na dawa yake si kutoonesha vikao vya bunge 'live'. Hivyo, hoja ya Nape ni ya kipuuzi na haiwezi kutatua tatizo la msingi linaloharibu bunge.

Inamvunjia heshima gani na wewe? Nape amewahi kuwa na heshima??
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nauye, amesema kuwa jambo lolote ambalo linaleta heshima kwa Bunge analiunga mkono.

“Suala la Bunge kurushwa ‘live’ halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?” alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.

Source:Nipashe Ijumaa

Hana lolote huyu kijana mwenzetu, kwanza inavyoonekana hata haelewi sababu ya hao wanaotaka kutunyima haki yetu ya kufuatilia majadiliano ni ipi hasa.
Namshauri tu kabla ya kuropoka anapaswa kwanza kuelewa mjadala unaoendelea kwani undani ndipo atoe maoni yake, huku kukurupuka kunamdhalilisha sana.

Atambue kuwa kupiga marufuku matangazo ya moja kwa moja ya mijadala ya bunge, hakutarejesha heshima ya bunge na wabunge wenyewe, badala yake ndo heshima itashuka zaidi.
Sisi wapiga kura tunataka kufahamu kwa kuona na kusikiliza wenyewe namna wale tuliowapa dhamana ya kutuwaklisha bungeni kama wanatimiza wajibu tuliowapa ipasavyo ama la!
Tunataka kufahamu kwa sura na majina yao kabisa ni akina nani wanatuhujumu bungeni kwa kukumbatia upuuzi wa kutetea vyama vyao na kuacha kutetea maslahi yetu.
Hii itatupa uwezo kwenye uchaguzi ujao,kufanya maamuzi sahihi ya kuwakataa wale wote wasiotupigania,wasaliti.

Pia yeye na chama chake waache woga, waache kutudharau sisi waajiri wao.....WANATAKA KUFICHA NINI?
 
Dalili za mwisho wa Uhai wa ma CCM. Bado kidogo tu wapige marufuku vikao vya bunge kwa singizio hakuna pesa za kuendesha shughuli za bunge
Naam, swadakta maumivu ya kichwa huanza pole pole na huko ndio tunakoelekea.
 
mawazo ya kitoto haya
ukienda maofisi karibu yote ya serikali hata mahakamani kuna TV ni za nini?
osifi nyingi watu wana viredio hata mimi ninacho ofisini kwangu huwa nachapa kazi na kusikiza bunge
usiku saa 5 ni muda wa kulala au kuangalie bunge?
magamba wote akili zenu mgando bure uwe kama mimi nisie na chama.
natamani shetani aje awachukue wote awapeleke kuzimu mkatawale huko mtuachie uhuru wetu.

Asubuhi ni muda wa kazi. Ukienda ofisini halafu usihudumiwe kisa mfanyakazi yupo busy kwa kuangalia bunge utajisikiaje?

Bunge lisionyeshwe live, wawe wanaonyesha marudio yake yote saa tano na nusu usiku.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hivi? Kwanini yatokee sasa? Mabunge yote yamekuwa yanaonyeshwa na tunapata habari? Leo Makinda ma wasaidizi wake wsmeamua kukandamiza haki na usawa kwa maslahi us ccm mnataka kufucha udhaifu wa spika na kusema bunge linatia aibu. MBONA MNASHINDWA KUMUAMBIA MAKINDA KITI KINAYUMBA???? Ccm acheni ubabe hautawasaidia tumieni njia sahihi kwa matokeo sahihi. Zima moto ilikuwa wakati wa siasa us ujamaa na zidumu fikra za.....
 
Asubuhi ni muda wa kazi. Ukienda ofisini halafu usihudumiwe kisa mfanyakazi yupo busy kwa kuangalia bunge utajisikiaje?

Bunge lisionyeshwe live, wawe wanaonyesha marudio yake yote saa tano na nusu usiku.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

WE KWELI SUMU!
Tangu bunge limeanza kuoneshwa live ni mara ngapi ulikosahuduma kwenye maofisi sababu ya watendaji kufuatilia vikao vya bunge ? ebu kuwa mtu mzima kidogo bwanaaaa!
Kwa hiyo mnataka kwanza mu-edit ndo mturushie
 
Kwa maana hiyo na TV ambazo zinaweka vipindi kazaa mida hiyo hawana maana kufanya hivyo?!
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nauye, amesema kuwa jambo lolote ambalo linaleta heshima kwa Bunge analiunga mkono.

“Suala la Bunge kurushwa ‘live’ halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?” alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.

Source:Nipashe Ijumaa

zile television kwenye ofisi za umma wafanyakazi wanaziangalia saa ngapi?
 
Nape sababu ilizozitoa hazina mashiko kurushwa kwa habari "live" Zinatoa nafasi kwa kwa wananchi kuelewa ni wabunge gani wanatetea haki zao na wabunge wapi wanatetea matumbo yao na wapi wanaosinzia bungeni.Kutokana na tabia ya CCM kuogopa ukweli wanafanya kila mbinu kuzuia vitu hivyo.Ebu Nape tueleze sababu za CCM kukataa midahalo wakati wa chaguzi mbalimbali ikiwemo wa Rais?
 
hao wasioenda kazini au maofisini unafikiri huwa wanazubaa ndani kuangalia bunge?kwa taarifa asilimia 80 ya nyumba mda huu ziko empty,au wapo mahousgal au wamama wa nyumbani na wako busy wanafanya usafi,kupiga deki kuosha vyombo,kufua,kuenda sokoni,kuandaa mlo wa mchana etc.
Wanaongaliaga TV mida kama hii hawazidi 5000 nchi nzima.

Kwa hiyo unataka kutuambia kuwa bunge kuoneshwa live KUNALIVUNJIA HESHIMA?
HEBU TUJARIBU KUTAFAKARI NA KUCHAMBUA MASUALA NYETI YAHUSUYO TAIFA LETU KAMA WATU WAZIMA WENYE BUSARA.
MwanaJF mmoja amesema nanukuu "asiyejiheshimu sebuleni, hawezi kujiheshimu chumbani"
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nauye, amesema kuwa jambo lolote ambalo linaleta heshima kwa Bunge analiunga mkono.

“Suala la Bunge kurushwa ‘live’ halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?” alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.

Source:Nipashe Ijumaa
POOR Nape..
 
Kutoonesha Bunge live ni sawa na Mtu mzima Kukiri kuwa kajamba mbele ya watoto. Kwamba aibu imewazidi kwa hiyo wafanye kimya kimya.
 
Back
Top Bottom