Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nauye, amesema kuwa jambo lolote ambalo linaleta heshima kwa Bunge analiunga mkono.
"Suala la Bunge kurushwa ‘live' halirushwi kwa wakati ambao watu wanafuatilia kwani wakati wa asubuhi watu wanakuwa maofisini, wakati wa mchana wao wanakuwa wako mapumziko wanakula na Bunge nalo linakuwa mapumziko, sasa wanaangalia saa ngapi?" alihoji Nape.
Alisema hawezi kupinga suala ambalo linaonekana lina faida na kuleta heshima kwa Bunge hivyo anaafiki uamuzi huo.
Source:Nipashe Ijumaa
Hapa ndipo unapoweza jua kuwa Tanzania kwa sasa hatuna viongozi makini. Maana ukisikilza kauli za waheshimiwa hawa kila mtu anajaribu kutoa sababu zake ambazo hazina chembe yoyote ya ukweli. Kwanza Makinda aliwahi kuwasifia TBC kwa kuonyesha Bunge LIVE,na akaipongeza serikali kwa kuongeza Bajeti ya Wizara ya Habari.
Lakini juzi baada ya kiti cha Spika na Naibu wake kuanza kupoteza mwelekeo Watu walewale wameanza kutoa sababu za kipuuzi kabisa. Katibu wa Bunge Bwana Kashililla anasema kuanzia sasa hakuna kuonyesha Bunge LIVE kwasababu ili kuzuia VURUGU za Wabunge wa CHADEMA wanaotaka umaarufu kupitia runinga!!!Lakini akaongeza pia kuwa itakuwa ni marufuku kwa waandishi wa Habari ku-recor/ku-mpiga picha Mbunge/Waziri anayelala Bungeni!!!Kwa hiyo kuanzia sasa watakuwa wana-RECORD, wana-EDIT na baadaye ku-BROADCAST hewani vipindi hivyo vya Bunge kwa ajili kulinda Heshima ya Bunge!!!
Naibu wa Spika Bwana Job Ndugai yeye amedai kuwa sababu ya kuondoa matangazo ya Bunge LIVE ni kutaka KUIMALIZA CHADEMA kisiasa kwa kuiondolea Umaarufu wa bure inaopata kutokana na vipindi vya Bunge kurushwa LIVE!!!
Leo Nape yeye anasema anaunga mkono maana wakti vipindi vya Bunge vinarushwa Watanzania wanakuwa hawaangalii maana wako makazini!!!!Hiki ni kichekesho cha karne. Hivi huyu Bwana Nape anataka kutuambia kuwa Watanzania wote ni Wakulima na Wafanyakazi tu??? Hivi Nape hajui kuwa kuna Watu kama wafanyabiashara wanaangalia Runinga wakiwa kwenye Bisahara zao???Mtu yuko dukani anasubiri Wateja au anasimamia bisahara zake na kuna wafanyakazi chini yake kwanini asiangalie runinga na akiwa amechagua chaneli ya TBC Bungeni Dodoma????Mbona hata kwenye maofisi haya haya ya serikali tunakuta Runinga zimewekwa maofisini na zinaangaliwa. Nimepitia ofisi kama Mabenki,Halmashauri za Miji, Wilaya na majiji kuna TV, ingia ofisi zote za Wakurugenzi, RC na DC wote wana ving'amuzi na wametune TBC!!!!
Kwa hiyo hoja ya Nape ni dhaifu sana wala haina mashiko. Pengine aliyesema sababu hasa za kutaka kuwamaliza CHADEMA kwa kuzuia umaarufu wao wanaoupata siku kwa siku kutokana na HOJA zao nzito zinazoitia serikali ya CCM KIWEWE!!Huu ndiyo ukweli na sababu za serikali kutaka kuzuia progrmmmes za TBC Bunge live kutorushwa LIVE!
CCM wamegundua kuwa Upinzani Bungeni na hasa CHADEMA unaendelea ku-gain popularity kutoka na HOJA nzito zinazoibuliwa na Wabunge wake na kuibana Serikali kiasi cha kushindwa kujitetea.Watu wanaweza kuhoji na kujiuliza mambo kama haya hayakuwahi kujitokeza wakati Bunge likiwa chini ya Spika Sam Sitta(Spika wa Speed)! Miaka 5 ya Sitta hatukusikia vurugu za Upinzani, Wabunge kupigwa picha wamelala(Walikuwa wakilala) kwa sababu Sitta aliliendesha Bunge kama inavyostahili kwa Bunge la Vyama vingi bila ya Upendeleo wala kuionea serikali aibu!!!
Sababu zingine zote zilizotolewa na hazina mashiko. Lakini CCM wajue kwamba Bunge hili si mali ya mtu fulani,si la CCM wala Makinda,Ndugai, Kikwete au Fisadi yoyote anayefikiri hivo. Bnge hili ni mali ya Watanzania wakiwa ni waajiri wa Wabunge wote,Mawaziri,Spika na Naibu wake maana ndiyo waliowapa ridhaa ya kutuwakilisha Bungeni kwa kura zetu. Sasa hatuwaelewi wanapoanza kutaka kutunyima uhuru wetu wa kuangalia Bunge LIVE. Hatutaki wala hatuhitaji kuona vipindi RECORDED and EDITED kujaribu kuficha UDHAIFU wa Serikali ya CCM ili kutaka kujiandalia ushindi hewa wanaouita wa KISHINDO!
Nahitimisha kwa kusema kuwa aktika hoja hii DHAIFU ya Uongozi wa Bunge akiwemo Spika Anna Makinda,Naibu Job Ndugai,Katibu Thomas Kashilila na Serikali wa kutaka kuondoa matangazo LIVE ya BUNGE nikutaka kujidanganya wenyewe. Tayari Watanzania wameshagundua na kung'amua sababu kubwa hasa ya kuondoa LIVE Broadcast ni
KUTAKA KUFICHA UDHAIFU WA SERIKALI YA CCM NA HASA UDHAIFU WA SPIKA ANNA MAKINDA NA NAIBU WAKE JOB NDUGAI AMBAO WAMEDHIHIRISHA KUWA HAWAWEZI KUSIMAMIA WALA KUONGOZA BUNGE LA VYAMA VINGI!