Bunge Lisionyeshwe LIVE - Wabunge!

Bunge Lisionyeshwe LIVE - Wabunge!

Sawa mkuu. Vinginevyo baada ya kusoma taarifa hiyo, that was my personal belief/judgement and all along kama umenisoma vizuri, its simply an opinion that is not founded on proof or certainty;

Kumbuka: I am entitled to my own opinion, but not my own facts; and so are you;

Mkuu Mchambuzi,

I respect your opinion but I the have rights to question the basis of your opinion, the reason I keep questioning is simply that some people in JF doesn`t know the differences between the two so what I am trying is make the records clear, don`t get me wrong I am not challenging your intelligence; your are one of the few who members in JF who I have much respects.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
mbona bunge letu hata halipo wazi?
Tunataka "voting records" za kila mbunge ziwepo kwenye hansard.
wasituletee ujinga.

Kobello,

..hilo ni wazo zuri sana.

..tatizo ni utaratibu wa kupiga kura wa bunge letu.

..kura hupigwa kwa kutumia makelele au mayowe.

..spika husema:" wanaoafiki waseme ndiyo." halafu wabunge huitikia kwa mayowe/makelele wakisema ndiyo, na hoja hupitishwa.
 
MMJ
Waweza kuzitaja baadhi ya faida hizo?

Sidhani kama atakujia hiyo sababu siku amekuwa ni wa kusema hapana kwa kila jambo hata halina maana anajitahidi sana kufanana na Rush Limbaugh yeye ni hapana hata kama jambo lina manufaa kwa jamii, hili ni tatizo la hawa waandishi wetu wa habari wa Tanzania wao wanaona njia pekee ya kupata sifa za kiuandishi ni kuandika uongo na uzushi, wanasahau miiko ya kazi zao.

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Sio bunge tu ... Nilitamani hata shughuli anazofanya raisi wetu kila siku zionyeshwe live.. Kwani naamini ndugu yetu Huyu hafanyi kazi zake sawasawa.
 
Wanajamvi,
Wenyewe wanasema 'I stand to be corrected'.
Hoja ya thread ipo wazi na ni dhima yetu tuijadili kama ilivyo na si kama hoja ya PakaJimmy. Tutakuwa tunafanya makosa kwa kumshambulia PakaJimmy kwa hoja aliyosikia na kutuletea. Kwahiyo tuna wajibu wa kuishambulia hoja ima kwa kuitetea au kuikosoa tukiheshimu uhuru wa kila mmoja kutoa mawazo yake katika jukwa hili huru.

Binafsi nimeikataa hoja hii kwa sababu zifuatazo
1. Bunge ni eneo la uwakilishwi wa wananchi na ni mahali huru kwa wawakilishi na wawakilishwi kuwasiliana. Wabunge ni waajiriwa wa wananchi na ni haki ya mwajiri kujua mwajiriwa wake anafanya nini na kwa wakati gani. Hakuna mahali popote duniani bunge limefanya kazi kwa siri. In fact sisi tumechelewa sana katika teknolojia, wenzetu majirani wamekuwa na utaraibu wa kuwa na vyombo vya habari kama Radio na TV miaka dahari.

2. Kuna jambo gani ambalo wabunge wanadhani ni siri na halipaswi kuonekana na jamii wanayowakilisha?

3. Wakati wa kuomba ubunge, wawakilishi wetu walikuja kutushika mikono na hata kupiga hodi majumbani.
Walifanya hivyo kwa kuelewa kuwa tulihitaji kuwajua kwa mambo mengi:

Jinsi wanavyowasilian nasi (communication), wanavyojenga hoja (Argument), wanavotusikiliza na wanvyotujibu (communication tena), wanavyojistahi(behave), ucheshi wao (humour), weledi wao( intellect) n.k.
Hawakufanya hivyo kwa kutumia mikanda ya kaseti au kupitia radio au video, walikuja na kutushika mikono tena wakigonga nyumba zetu na kufunguliwa na mahausi geli.
Iweje leo wanapotuwakilisha wahisi kuwa hawana haki ya kuonekane wakitetea sifa hizo hapo juu zilizowapeleka Dodoma?

4. Teknolojia ya mawasiliano imemleta mwanadamu karibu na mazingira yake. Ilianza ya audio kama radio na hatukuwahi kusikia malalamiko, sasa TV ambayo inatufanya tuwe karibu na mwakilishi wetu kwanini ionekane kama ni chombo kinachojenga uadui kati ya mbunge na mwananchi?

5. Ni kwa kipengele gani cha maadilli ya kazi(ethics), haki za mfanyakazi (Labor laws), haki za binadamu (Human right), sheria za nchi (Laws and regulations) amabacho kinakiukwa (Infringed) kwa mbunge ambaye ni mwakilishi wa wananchi kuonekana akifanya kazi?

Haya ni maoni yangu na si lazima yashabihiane au yapingane na mtu. Hakuna usahaihi au makosa kwa maoni binafsi ili mradi hayavunji haki za mwingine.

PakaJimmy ameuliza swali la uchokozi pengine kutak kujua nini mtazamo wa hoja ya Mwanakijiji kama ambavyo anaweza kuchagua hoja nilizozitaja na kuniuliza. Yaweza kuwa alitaka kufahamu au ku-provoke ili mtu afunguke zaidi.
Hakuna kosa katika hilo ni sehemu ya ku-moderate nyuzi yake na nampongeza.

Tatizo ni pale tunapoacha mada halisi kwa kuishambulia hasi au chanya na kuanza kushambulia watu (character assassination) au kushambulia wajihi ( personality attack).

Tumetoka nje ya mstari kwa kuacha hoja na yatokanyo na hoja na kuanza kushambuliana. It is very unfortunate!
Ningependa mtu azishambulie hoja zangu na si mimi kama Nguruvi3. Ubaya wa jina langu, uzito au wepesi wa hoja zangu usiwe sehemu ya mjadala.
 
Kati ya wanaoandaa hoja hakosi Mzee wa usingizi[Wasira].Wangeweza wangesema hata TV ipigwe marufuku Tanzania.
 
Kweli, wala siyo maswala ya kichama wala nini, ila hii imeniudhi sana jamani. Hata wale wajinga wanaochagua ccm ni muda wao kujiuliza hii ni kwa sababu gani....!
 
Kweli, wala siyo maswala ya kichama wala nini, ila hii imeniudhi sana jamani. Hata wale wajinga wanaochagua ccm ni muda wao kujiuliza hii ni kwa sababu gani....!
Tanga, Morogoro, Lindi Mtwara, Dar Es Salaam mpo?
 
Kweli wabunge wetu vihiyo sana.Kwanza hawana tija yeyote kwa taifa letu,huu ndio ukweli ambao kila mwananchi wa Tanzania anaujua.As if that is not enough wanaleta upuuzi mwingine tena,wananchi hawa hawa ambao ndio waajiri wao hawataki wawaone ili waweze kuwa-asses.Jamani unapoajiri mtu si unatakiwa pia kufanya assesment ya utendaji wake.Sasa kama hawataki tuwaone ina maana hawataki tuwafanyie tathmini,waondoke. Inamaana hawataki kazi.Afterall ni liability tu kwa watanzania!
Spika wa Bunge amesema kuwa baadhi ya wabunge wanaandaa hoja ya kuzuia vipindi vya Bunge kuonyeshwa LIVE kwa wananchi!
Ninavyochukulia: Huku ni kulewa Madaraka!...Wanataka wachape usingizi bila kuhojiwa na wapiga kura hawa!

CHANZO: Gazeti la Mtanzania leo 13/08/2012
 
Jamani hivi kweli Tanzania tuna kitu kinachoitwa bunge?mimi nafikiri kuna kijiwe tu cha watu wa daraja fulani tu ambao hukutanika sehemu kupiga porojo na kupanga dili za wizi na rushwa,ni kama kijiwe cha Saigon pale Kariakoo
 
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]

TUMESHTUSHWA na habari kwamba baadhi ya wabunge hawataki vikao vya Bunge vionyeshwe moja kwa moja kwenye televisheni. Akifungua semina ya waandishi wa habari za Bunge mjini Dodoma juzi, Naibu Spika, Job Ndugai alisema wabunge hao hawataki shughuli zote za chombo hicho zionyeshwe ‘live’ kwa wananchi, isipokuwa tu kipindi cha maswali na majibu na wakati wa kupitisha vifungu vya bajeti baadaye jioni.

Kiongozi huyo, pamoja na kupinga hoja hiyo ya baadhi ya wabunge alisema suala hilo linahitaji mjadala mkubwa na kusema kitendo cha kutoonyesha vikao vya Bunge ni sawa na kuturudisha huko tulikotoka badala ya kusonga mbele. Alisema wabunge wanaotoa hoja hiyo wanadai kwamba kabla shughuli za Bunge hazijaanza kuonyeshwa moja kwa moja, baadhi ya wabunge walikuwa hawafanyi vitendo wanavyofanya hivi sasa kwa lengo la kuonekana katika televisheni.

Hizi ni habari mbaya na uthibitisho kwamba demokrasia yetu siyo tu iko kitanzini, bali pia zinaonyesha kwamba wabunge wengi hawaungi mkono au hawaelewi dhana ya uwazi na utawala bora katika uendeshaji wa mhimili huo wa dola. Tulitegemea kwamba wabunge wetu ndiyo wangekuwa msitari wa mbele kuhakikisha shughuli zote za Bunge zinaendeshwa kwa uwazi na wananchi kuwezeshwa kuzifuatilia kupitia televisheni na vyombo vingine vya habari, zikiwamo redio na magazeti.

Hakuna aliyetegemea kwamba ungefika wakati wabunge wakapinga hatua ya Bunge kuendesha shughuli zake kwa uwazi na badala yake kutaka chombo hicho kufanya shughuli zake kwa kificho. Hakuna ubishi kuwa, tayari imethibitika kwamba wananchi wamehamasika kwa kiwango kikubwa tangu shughuli za Bunge zianze kuonyeshwa moja kwa moja katika televisheni. Wananchi sasa wamekuwa na mwamko mkubwa kiasi cha kufuatilia uwajibikaji wa wawakilishi wao bungeni na hii bila shaka ndiyo sababu baadhi ya wabunge wasiowajibika wameona matangazo hayo ya shughuli za Bunge kupitia televisheni yatasababisha anguko lao.

Nani asiyejua kwamba matangazo ya moja kwa moja ya shughuli za Bunge yamesaidia kubadilisha taswira ya Bunge? Ni kupitia televisheni wananchi wameweza kuona matendo ya wawakilishi wao na hiyo imewasaidia kurekebisha mienendo yao, ikiwa ni pamoja na kujitahidi kuwa waungwana na kuepuka jazba wakati wakitoa hoja zao. Wengi wamelazimika kuwa makini kwa lengo la kuwa na mwonekano wa kibunge, hasa kwa kuwa na mavazi stahiki wakati wote wanapokuwa bungeni.

Naibu Spika Ndugai amefanya vyema kupangua hoja mgando za baadhi ya wabunge wanaotaka Bunge lifanye shughuli zake katika giza totoro ili wananchi wasijue kulikoni. Tunakubaliana naye asilimia 100 anaposema mabunge yote duniani yanayoendeshwa katika mazingira ya kidemokrasia huonyesha shughuli zake moja kwa moja kupitia televisheni na kwamba kufanya vinginevyo ni kinyume cha demokrasia na utawala bora. Ni kwa njia hiyo wananchi wanaweza kupima uwezo na uwajibikaji wa wawakilishi wao katika maeneo mengi wakiwa bungeni, ikiwamo mahudhurio, ujenzi wa hoja, kauli na mienendo yao kwa jumla.

Inakuwa vigumu kuelewa msingi wa msimamo huo wa wabunge wanaotaka kuturudisha enzi za kale za usiri na udikteta. Lakini jambo lililo bayana ni kwamba hao ni wabunge walioingia bungeni wakidhani huko ni mahali pa kupumzika na kuponda raha. Kumbe wamekuta Bunge likiendeshwa kwa uwazi wa ajabu na likiwa na shughuli nyingi na nyeti tofauti na ilivyokuwa miaka 15 hivi iliyopita. Wamekuta Bunge siyo tena kichaka cha kupiga usingizi au porojo na wameshuhudia wabunge wanaofanya hivyo wakiumbuliwa na picha za magazeti na televisheni.

Naibu Spika huyo anasema wabunge hao pia wanahoji matangazo hayo ya televisheni ni ya nini wakati yapo magazeti, kwa maana kwamba haiwezekani televisheni zionyeshe leo halafu kesho yake wanunue magazeti? Hizo ni hoja hafifu na dhaifu zinazoonyesha jinsi baadhi ya wabunge wasiowajibika walivyozongwa na hofu ya ajabu[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Fikirieni bunge linaonyeshwa live lakini tunashuhudia matusi fujo na kejeli sa lisipoonyeshwa live wabunge si watakua wanachapana mangumi kabisa
 
Back
Top Bottom