Bunge Lisionyeshwe LIVE - Wabunge!

Bunge Lisionyeshwe LIVE - Wabunge!

Spika wa Bunge amesema kuwa baadhi ya wabunge wanaandaa hoja ya kuzuia vipindi vya Bunge kuonyeshwa LIVE kwa wananchi!
Ninavyochukulia: Huku ni kulewa Madaraka!...Wanataka wachape usingizi bila kuhojiwa na wapiga kura hawa!

CHANZO: Gazeti la Mtanzania leo 13/08/2012

Mkuu PakaJimmy,sio tu kulewa madaraka, hii ni dharau ya hali ya juu. Hivi wanayoyajadilli humo mjengoni ni ya nani? Kama ni sisi ndio tulowatuma basi waache upuuzi wao na kujadili bila kificho, lakini kama wanadhani walijipeleka wenyewe basi walete huoupuuzi wao halafu tutakutana kwenye boksi la kura 2015.
Mimi mwenyewe sipendi kuandamana lakini katika hili itabidi nimsapoti kimbunga. Kama noma na iwe noma bana.
 
Ha ha ha haa kwa hiyo hawataki tuone wanavyotuwakilisha? kazi ipo
 
Aiseee baba yangu kama hawataki 2waone hata wakija kuomba kura 2siwaone


namalizia mbege
nikalime
 
Mimi nadhani ndio lile dai la Naibu spika kuwa WABUNGE WENGI WANAINGIA BUNGENI WAKIWA WAMELEWA POMBE NA SIGARA KALI KALI.
This is too abnormal!

Hii na yenyewe ilikuwa kali. Wabunge wetu ni walevi na wanavuta sigara "KALI (Majaniiiiiii P. Funk hapa)". Nadhani ndicho alichokisema Spika.
 
Kimbunga mimi sitaandamana kwanza, nitakwenda Mbeya wanipe mbinu za kupopoa viongozi, ushanfahamu!

Halafu nifanye sahihisho katika bandiko lako, hatukuwatuma bali sisi ndio tumewaajiri. Tukisema tumewatuma watasema wakirudi watatupa habari. Tumewaajiri na kama waajiri tunatatka kujua wanafanya kazi tuliowatuma?

Mkuu Nguruvi3 (Jina hili kwetu lina maana ya muumba) nimekubali sisi ndio waajiri wao.
 
Last edited by a moderator:
Hiyo hoja haiendi kokote. Bunge kuonyeshwa kwenye live kwenye walikataa miaka ya 1990 lakini wakalazimika kwamba standard ya mabunge yote ni kuonyeshwa kwenye TV. Kama wabunge Tanzania hawataki basi wajiondoe kwenye international community kama North Korea.
 
mtume!! yallab tunusuru kabisa na hoja za wabunge tuliowachagua na kula zetu wenyewe, ikiwemo na kupoteza muda wa kupanga foleni na jua kali kwenye vituo vya kupiga kura, kulinda kura zisiibiwe na matokeo yake zikaibiwa. tulisitisha shughuri zetu za utafutaji kwenda kupiga kura na kura imekuwa kura kweli mana tulio wapigia wameshiba sasa wanaropoka ovyo ovyo yasiyotakiwa
kweli nimeamini shibe mwana malevya/kuropoka njaa mwana mkalimu. mana kipindi cha njaa wanakuwa wakalimu kuomba chakula tumewapa wameshiba hawatuthamini kweli shukrani ya punda ni mateke hakika M/mungu atawalaani wenye kufanya hiyo.
 
Itakuwa ishara ya maporomoko ya ccm ,narudia kuwakumbusha kuwa kizazi cha sasa ni makini na si cha mazezeta km wanavyofikiria,wajaribu waone
 
Kabla hawajatoa hizo kauli hao wabunge pamoja na Ndugai inaonekana walikuwa wamelewa na kupiga ile sigara ambayo siyo ya kawaida. Napendekeza TV zote na redio zote nchini zirushe moja kwa moja matangazo ya bunge ili wananchi wote waone bunge lao.
 
Sijawahi kuandamana miaka ya hivi karibuni lakini yakiitishwa maandamano ya kupinga hii hoja mimi Kimbunga nitashika bango na kuwa mstari wa mbele. Hawa wabunge wetu wamepatwa na nini? Karne hii ya utandawazi, uwazi na uhuru wa kupata habari wao wanataka kutunyima kujua wanatuwakilishaje? Hivi wamesahau kwamba sisi ndio tumewatuma na tunatakiwa tujue wanatuwakulisha vipi? Wanataka kufanya siri?

Ama kweli madaraka kitu kibaya sana. Mtu akiitwa mheshimiwa basi anadhani anaweza kufanya analotaka? Mimi binafsi nataka tuendelee kupata habari za kibunge LIVE bila Chenga. Kama hawatimizi wajibu ipasavyo tuwaone wasitake kujificha.

Mkuu futa kauli yako
unaamini kuwa tumewachagua
(tumewatuma au wanajituma )
 
Ujuwe hao hawakutumwa na wananchi, walijipeleka wenyewe kwa nguvu zao za pesa. Acha waendelee hivyo hivyo watupe hoja

Sijawahi kuandamana miaka ya hivi karibuni lakini yakiitishwa maandamano ya kupinga hii hoja mimi Kimbunga nitashika bango na kuwa mstari wa mbele. Hawa wabunge wetu wamepatwa na nini? Karne hii ya utandawazi, uwazi na uhuru wa kupata habari wao wanataka kutunyima kujua wanatuwakilishaje? Hivi wamesahau kwamba sisi ndio tumewatuma na tunatakiwa tujue wanatuwakulisha vipi? Wanataka kufanya siri?

Ama kweli madaraka kitu kibaya sana. Mtu akiitwa mheshimiwa basi anadhani anaweza kufanya analotaka? Mimi binafsi nataka tuendelee kupata habari za kibunge LIVE bila Chenga. Kama hawatimizi wajibu ipasavyo tuwaone wasitake kujificha.
 
Hoja hii itakuwa kati ya hoja za kipuuzi kuliko zote zilizowai kuwakilishwa bungeni.
 
Siwezi kuwashangaa, nilisikiliza mawazo yao wakati wanaharakati wanapinga mfuko wa jimbo na sikuamini. Ni kipindi kile nilipong'amua kuwa hawa wabunge ni miongoni mwa watanzania wanaodhani wapo juu ya sheria.

Utasikia michango yao bungeni wakiwa wanawashambulia watumishi wa serikali kwa kula rushwa na huku wakiwataja majina kwa mbwembwe lakini ilipofika wao kula rushwa hawataki kabisa majina yao kutajwa!

Baada ya hapo wataamuru vyombo vya habari kutoandika habari ambazo ni "negative" dhidi zao! Huu ni ulevi usio na mfano na kama jamii itachelewa basi taifa litazidi kuongeza idadi ya "untouchables"!

Thanx mkuu, nimetafuta kitufe cha like cjakiona ila umemaliza mkuu wangu.
 
Hawa wabunge wanaopendekeza haya ni wale wanaolala bungeni. Sidhani kama hoja hii itapita.
 
Back
Top Bottom