wanabodi JF,
Kwa mara nyingine jioni hii katika taarifa ya habari kwenye Luninga kadhaa,amejitokeza bwana kashilila ambaye ni katibu wa bunge,ametoa tamko kwamba wabunge wa ccm,wanakusudia kupitisha hoja ya kuzuia matangazo ya moja kwa moja kutoka kwenye vikao vya bunge kupitia luninga..
Hii ni kwa kile alichokiita kuwa ni kuzuia vioja vya utovu wa nidhamu kwa baadhi ya wabunge wakati wa kuwakilisha hoja zao au kuomba miongozo ya spika jambo ambalo kwake yeye amesema linalifedhehesha bunge kwa wananchi.
MY TAKE:
hivi serikali yetu inashindwa kuiga mfano wa wenzetu KENYA ambao pamoja na kuhitilafiana kiitikadi na hata sometimes kikabila,lakini wamefanya kile ambacho hata serikali ya ccm ilikiogopa kupitia mgombea wake ambaye kwa wakati huo aliukacha mdahalo wa wagombea urais na hata ile midahalo majimboni ilipolazimishwa na uongozi wa TBC,ulimponza Bw Tido mhando,na hatimae kufuzkuzwa kazi kinyemela kabla ya mkataba wake kuisha.
Leo hii nchi imegubikwa na kashfa kila kona,ambazo wananchi tulitarajia kuona serikali kupitia mhimili wake ambao ni bunge lake,ikiacha demokrasia ikitumika ili kuisimamia serikali katika kuhakikisha hoja muhimu na zenye maslahi kwa wananchi na raslimali zetu zikijadiliwa ili kuliokoa taifa huko shimoni tunakopelekwa na mafisadi zikijadiliwa kwa kina na kwa usawa bila kusukumwa na itikadi za vyama,bali na uzalendo kwa maslahi ya taifa letu kwa sasa na vizazi vijavyo.
Hali imekuwa kinyume na matarajio ya wananchi.Bunge letu limegeuka kuwa kijiwe cha wana CCM kwa kutumia wingi wao ndani ya bunge na kupindisha kanuni kwa maslahi yao na chama chao na badala ya kuisimamia serikali,bunge limegeuka mbeleko ya serikali katika kuibeba kwa madhila yote tunayoyaona
Yakifanyika bila serikali kuchukua hatua madhubuti nitaorodhesha machache na yeyote humu anaweza kuongezea
.
*Tatizo la mgogoro wa Gesi asiiia kule mtwara
*Tatizo la ukandamizaji wa mhimili wa vyombo vya habari vinavyoikosoa serikali
*Tatizo la mitaala mibovu katika sekta ya elimu na maslahi duni kwa walimu.
*Tatizo la udini linalochipuka kwa kasi.
*mabilioni yanayosadikia kufichwa uswisi.
*spika kuvunja kamati muhimu za bunge kinyemela wakati ambao ndio zilihtajika kufanya kazi
*mauaji ya raia yanayofanywa na polisi bila hatua madhubuti kuchukuliwa na serikali,
*janga la ujambazi linaloongezeka kila kukicha nchini na kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.
*Ujangili wa maliasili zetu hasa meno ya tembo unaofanywa na waandamizi wa serkali.
*kero ya uhaba wa maji na ukame unaolikabili taifa
*Wananchi kuanza kutokuwa na imani na jeshi letu la polisi,
*ombaomba na watoto wa mitaani wanaoongezeka mijini kila kukicha. Nk.....
HALAFU BUNGE LINATAKA KUZUIA MATANGAZO YA MOJA KWA MOJA,jE?
Hii ni nini kama sio kutaka kuficha uozo mbalimbali utakaoibuliwa na wapinzani wachache ndani ya bunge usionekane kwa wananchi,ili kuilinda CCM kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa,ambao uko mbioni kufanyika.na pia hata uchaguzi mkuu ujao.?
Je hii si aibu kwa wafadhili na mataifa tunayoita wahisani kwa kutaka wasijuwe jinsi misaada yao inavyotumika ndivyo sivyo?
Hivi kama hilo litafanyika,Rais wetu bado ataendelea kusafiri ughaibuni akiwa kifua mbele,au ndio mwanzo wa kutaka kuwekewa vikwazo kama kwa mu***e
Jamani narudia hii ni aibu kubwa kwa taifa linalojiita la kidemokrasia mbele ya jamii za kimataifa wakati,hapa ndani ya mjengo tukitaka hata raia wasijuwe kama mnafanya kile walichowachagua ili mkawawakilishe kwayo
Inauma sana sana-tena sana,ebu kama taifa tujiridi na viongozi wetu mumuungamie mungu mwenyezi.