Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Watanzania wenzangu tutumie fursa ya katiba mpya kuingiza kipengele kwenye katiba mpya kitakachotamka wazi kuwa bunge ni shariti lionyeshwe live na TV ya taifa na hata zile za binafsi zitakazokuwa tayari kurusha matangazo hayo.

Hatua hii itatuondolea aibu na fedheha hii ya kutaka kusitisha matangazo kama ilivyotangazwa jana na katibu wa bunge Dr.Thomasi kashilila.Uamuzi huu bila shaka umelenga kuficha madudu ya serikali na aibu ya viongozi wa bunge na wabunge wa ccm wasiowajibika kwa wapiga kura wao.

Moja ya kauli iliyoripotiwa na magazeti ya leo ni kuwa eti ni marufuku kupiga picha wabunge waliolala bungeni.Hakika hili ni tamko la ajabu sana kutolewa na kiongozi wa bunge.

Hatua hii itawafanya wapiga kura kushindwa kupima utendaji kazi na uwajibikaji wa wabunge wao.Mbunge yeyote asietaka jamvo hili ajiuzulu kwani halazimishwi.

Tutumie fursa hii adimu ya katiba mpya kuondoa ufedhuli huu.
 
kUMEKUCHA! SASA ISHARA ZOTE ZA ANGUKO KUBWA KWA CCM LIKO KARIBU. WANAJARIBU KUFICHA UTUPU AMBAO NI TUPU TAYARI. AMA KWELI SIKU YA KUFA NYANI MITI YOTE HUTELEZA. AKILI NDOGO INATAKA KTAWALA AKILI KUBWA? SUPIKS, NAIBU WAKE, KATIBU WAKE, WENYEVITI WOTE WAPISHE AKILI KUBWA ZIONGOZE BUNGE. WANAONA HAYA KUTAFUTA UZOEFU KWA MZEE WA VIWANGO NA KASI (STANDARDS AND SPEED) SAMWEL SITA?

Kumbukumbu kwa samuel sitta
 
katika hilo watanzania tutakosa haki ya kuhabarishwa,kama kuna watu wanavunja kanuni washughulikiwe kulingana na kanuni

Mkuu hapo umenena, nina wasi wasi na huo udaktari wa katibu wa bunge, hivi kweli dawa ya mvunja kanuni ni kumficha asionekane wakati anapo zivunja? Ina maana bunge letu ni butu kiasi kwamba haliwezi kumwajibisha aliyevunja kanuni mbadala wake ni kumficha ili asiaibishe? something is very wrong somehwere!
 
Halafu "oooh, Tanzania ni nchi yenye uhuru wa habari".

Nyoooo.

Nani ataondoa hoja "zisizo za msingi"? Kwa muongozo gani?

Kama kuna wabunge wenye "hoja zisizo za msingi" kwa nini bunfe lisiache wananchi waone wabunge wao wanavyotoa "hoja zisizo za msingi" live ili kuwaelewa zaidi na kuweza kuamua vizuri zaidi kama wataendelea kuwachagua au watawamwaga uchaguzi ujao?

Kwa nini bunge linaingilia uhuru wa vyombo vya habari?

Kwa nini wanahabari wasilishitaki bunge mahakamani?

Kwa nini wabunge wasitunge sheria ya "freedom of information" itakayohakikisha bunge haliwezi kupitisha maazimio ya kidikteta kama haya?

na inasikitisha sana ikiwa bunge inakiuka katiba ya sasa ya jamuhuri ya muungano wa tanzania

sehemu ya tatu ya katiba haki na wajibu
haki ya uhuru wa mawazo 18
, subsection 2.
. Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.
kwa kweli inasikitisha sana.
 
mbona spika hatajwi kuwa yeye ndio anaharibu kanuni za bunge na kupelekea vurugu bungeni?
wapinzani ndio wanaoharibu kanuni bila sababu?
huu ni upuuzi
 
hii kali ya mwaka.....hatuna solution nyingine zaidi ya hii.?
bora ukose mali lakini uwe na hekima na busara..........hizi ndo busara za magamba.
 
nikisema maccm ni mashetani napigwa ban,si mnasikia maazimio yanayotolewa kwa niaba ya shetani?
 
Hivi wabunge wa upinzani wako robo ya wabunge wote the rest ni ccm, lakn bunge linapelekwa mchaka mchaka mno, je ingekuwa 40% to 60% ingekuwaje? Kumbe ukiwa mtu wa facts unaweza kusimama against watu mia... Nashangazwa sana na swala la dr. Kashilila eti mbunge akisinzia marufuku kupigwa picha, hv anataka wakalale kule?
Niwaambie tu ccm, m2 akiwa na anatafuta umaarufu bungeni kwa kuongea hovyo sisi tuna uwezo wa kuchambua mbichi na mbivu, huko bungeni mnataka mfiche nini?
Au mnataka kuwarushia wabunge wa upinzani vitu vizito vya ncha kali?
 
BUNGE KUSITISHA KURUSHA VIKAO VYAKE.

BUNGE linatarajia kufuta utaratibu wa kurusha matangazo ya moja kwamoja kupitia televisheni kwa madai ya kukomesha vitendo vya baadhi ya wabunge kukiuka kanuni za bunge na kuleta vurugu kwa kutafuta umaarufu bila kujua kwamba tabia hiyo inaleta picha mbaya katika jamii.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Bunge Dk.Thomas Kashilila jijini Dar es salaam wakati akitoa taarifa ya mapendekezo ya kuanzisha kamati ya bajeti na kuvunjwa kwa baadhi ya kamati za bunge.

Amesema kuwa ili kuleta maadili kwa baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wanashindwa kufuata kanuni za bunge na kutumia nafasi hiyo kwa kutafuta umaarufu kwa sasa wameomba kufutwa utaratibu wa kurusha matangazo ya bunge ya moja kwa moja badala yake watarekodi ili kuondoa hoja zisizokuwa za msingi.

Ameongeza kuwa kuna idadi kubwa ya wabunge wamekuwa wakikiuka kanuni za bunge makusudi na kusababisha kuleta vurugu bungeni wakati jamii ikiendelea kutazama mabishano yasiyokuwa na hoja za msingi.

Dk Kashilila amesema kuwa kwa sasa kuna baadhi ya kamati za bunge ambazo zimevunjwa kutokana na baadhi ya kamati hizo kuingilia katika utendaji jambo ambalo limekuwa likipoteza maana ya kamati hizo.

Hivi karibuni baadhi ya kamati ikiwemo ile ya Mashirika ya umma POAC zimefutwa na kuacha maswali mengi kwa baadhi ya wananchi juu ya hatua hiyo.

siungi mkono hoja ya dokta thomas kashilila
 
Kumbe tunaweza kuona bunge likijadili mabadiliko ya katibu ikiwa recorded?
 
Hivi wanavyofanyaga maamuzi ya namna hii huwa hawana hata watu wa kuwashauri??

Hii ni aibu sana! Does it mean wamekosa kabisa namna ya kuwawajibisha hao wabunge?

ALWAYS THE BOSS IS RIGHT.. So whether this deciosion is beneficial or not we have to agree.. As magamba ndo wamesema.

But I'm sorry for them coz kwa mwendo huu wa digital hakuna uozo utakaojificha lolz.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Halafu "oooh, Tanzania ni nchi yenye uhuru wa habari".

Nyoooo.

Nani ataondoa hoja "zisizo za msingi"? Kwa muongozo gani?

Kama kuna wabunge wenye "hoja zisizo za msingi" kwa nini bunfe lisiache wananchi waone wabunge wao wanavyotoa "hoja zisizo za msingi" live ili kuwaelewa zaidi na kuweza kuamua vizuri zaidi kama wataendelea kuwachagua au watawamwaga uchaguzi ujao?

Kwa nini bunge linaingilia uhuru wa vyombo vya habari?

Kwa nini wanahabari wasilishitaki bunge mahakamani?

Kwa nini wabunge wasitunge sheria ya "freedom of information" itakayohakikisha bunge haliwezi kupitisha maazimio ya kidikteta kama haya?


Mkuu Kiranga kinachofanywa na serikali ya CCM ni sawa na kuziba ndoo inayovuja ilhali maji chanzo cha maji kingali wazi, matokeo yake maji yatajaa kwenye ndoo na yatavuja kutoka kinywani mwa ndoo.
Ni dhahiri CCM wameishiwa mbinu za kuongoza, bora tuanze kuipa buriani mapeeeeeeeeema
 
BUNGE KUSITISHA KURUSHA VIKAO VYAKE.

BUNGE linatarajia kufuta utaratibu wa kurusha matangazo ya moja kwamoja kupitia televisheni kwa madai ya kukomesha vitendo vya baadhi ya wabunge kukiuka kanuni za bunge na kuleta vurugu kwa kutafuta umaarufu bila kujua kwamba tabia hiyo inaleta picha mbaya katika jamii.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Bunge Dk.Thomas Kashilila jijini Dar es salaam wakati akitoa taarifa ya mapendekezo ya kuanzisha kamati ya bajeti na kuvunjwa kwa baadhi ya kamati za bunge.

Amesema kuwa ili kuleta maadili kwa baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wanashindwa kufuata kanuni za bunge na kutumia nafasi hiyo kwa kutafuta umaarufu kwa sasa wameomba kufutwa utaratibu wa kurusha matangazo ya bunge ya moja kwa moja badala yake watarekodi ili kuondoa hoja zisizokuwa za msingi.

Ameongeza kuwa kuna idadi kubwa ya wabunge wamekuwa wakikiuka kanuni za bunge makusudi na kusababisha kuleta vurugu bungeni wakati jamii ikiendelea kutazama mabishano yasiyokuwa na hoja za msingi.

Dk Kashilila amesema kuwa kwa sasa kuna baadhi ya kamati za bunge ambazo zimevunjwa kutokana na baadhi ya kamati hizo kuingilia katika utendaji jambo ambalo limekuwa likipoteza maana ya kamati hizo.

Hivi karibuni baadhi ya kamati ikiwemo ile ya Mashirika ya umma POAC zimefutwa na kuacha maswali mengi kwa baadhi ya wananchi juu ya hatua hiyo.

Dr Kashililah huwa naamini kwamba bosi hakosei lakini kwa hili Dr umekurupuka,kama ni kweli hamna sehemu yoyote ambayo wananchi wameguswa kwa namna yoyote,lakini wanapewa adhabu ya kutokuangalia Bunge na ukiangalia umedai wabunge wanakiuka taratibu za Bunge,kwa jinsi hiyo hautaki wananchi waangalie wawakilishi wao wanavyowawakilisha Bungeni,sio fair hauwatendei haki Watanzania au ni nini mnachokifanya humo ndani ambacho hamtaki Wananchi wakione?
Kama hamtaki wananchi waone bunge kuna haja gani kurudi kuomba ridhaa ya wananchi au wananchi kuwachagua watu amba hawajui wanafanya nini huko Bungeni make mnafanya siri humo mjengoni MNATAMBIKA humo?
Tunaanza kupiga kelele ili wananchi wasusuie uchaguzi sababu upo kwa kuwasaidia wengine au mnawawakilisha wakina nani? Kama mnawawakilisha wananchi mnaficha nini ambacho hamtaki wananchi waone poor thinking kama wewe Dr ndie ulietoa wazo hilo wewe mjinga na mpumbavu kwa kufanya watu fulani ni bora kuliko wengine
Wabunge msirudi kuja kuomba ridhaa ya wananchi
 
Nakumbuka (EWURA) walishindwa kusimamia kanuni za mafuta, kisha wakapandisha bei ya mafuta ya taa. Sasa ugonjwa unaelekea kichwani, wanataka kutunyima haki ya kukatiba; wanataka kukiuka ibara ya 18 ya Katiba.
Hili halikubaliki popote duniani.
 
Back
Top Bottom