Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Wala sijapenda taarifa za huyo katibu wa Bunge,haina maana ya kuficha kile ambacho kinafanyika ndani ya BUnge kwani mle ndani ya Bunge sio mahara pa siri,sioni sababu ya kutokuonyesha live au wanataka kuwa wana edit pale ambapo wataona kuwa wamezidiwa kwa hoja.Wala sio fair kabisa.Tunaelewa wanapigania matumbo yao,ili wananchi wasijue madudu yanaendelea selikalini.Ukifuatilia historia ya nchi nyingi zilizoingia kwenye vita utagundua kuna sababu nyingi zinapelekea kuingia huko ikiwemo na uongozi mbaya.Ila wakae wakitambua kuwa hiki ni kizazi cha dot.com sio kama kile cha enzi zile za zidumu fikra za mwenyekiti.Tahadhari yasije yakatokea kama yale ya Misri.
 
Hivi tz kweli tumelogwa? Huyu katibu wa bunge ndivyo alivyotumwa na viongozi wa bunge kuficha madudu wanayoyafanya? Kweli ndo maana imesemwa Kenya inaongoza kwa matumizi ya IT, Tanzania kwa uchawi? Kitendo cha kuficha matangazo ya bungeni live hakina tofauti na mchawi ambae mambo yake hufanya gizani!
 
Eee Mungu tuepushie baraza letu la wawakilishi Zanzibar na udikteta kama wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
 
mimi naona kuwa aliyetoa wazo hili afunguliwe shitaka la jinai kwani anavunja katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania ya mwaka 1977.
katika ibara ya 18.kila mtu
(d)anayo haki ya kupewa taarifa wakati wowote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii
.

je huyu anayeamua kumfurahisha mke wake kwa kutaka atukomoe ana uelewa wa kutosha,au ndo wale wale wenye udaktari wa zawadi?????
Vyeo vya zawadi navyo si vizuri kwani unatakiwa kumfurahisha bwana wako kila wakati
hata...............
nahisi ni hawara si mke
 
Yule jamaa wa mdahalo wa Kenya alisemaje vile?
Mtu ana Ph.D ya umeme lakini bulb yake ikiungua ni mtu wa darasa la nane anayekuja na kuibadilisha! So much for the doctorate. Msinitishe nazo tena!

Sent from my GT-P7500 using Tapatalk HD
 
kUMEKUCHA! SASA ISHARA ZOTE ZA ANGUKO KUBWA KWA CCM LIKO KARIBU. WANAJARIBU KUFICHA UTUPU AMBAO NI TUPU TAYARI. AMA KWELI SIKU YA KUFA NYANI MITI YOTE HUTELEZA. AKILI NDOGO INATAKA KTAWALA AKILI KUBWA? SUPIKS, NAIBU WAKE, KATIBU WAKE, WENYEVITI WOTE WAPISHE AKILI KUBWA ZIONGOZE BUNGE. WANAONA HAYA KUTAFUTA UZOEFU KWA MZEE WA VIWANGO NA KASI (STANDARDS AND SPEED) SAMWEL SITA?
 
Nalo hili nguvu ya umma itatumika, ni kutowatendea haki watanzania wanaotaka kujua kuwa wawakilishi wao wanafanya nini. Huyu Kashilila ni nani mpaka hatufanye watanzania 45+ tusione bunge? Hivi hawa watawala wa miaka hii nani kawadanganya kwa upuuzi huu? Yani wanadhani sie ni wajinga kwa kiwango hicho?
 
Bunge linajadili kusimamisha matangazo ya moja kwa moja ya vipindi vya bunge kurushwa katika televisheni kwa kile linachosema kupunguza wananchi kuona fujo zinazotokea bungeni. MAANA YAKE TUTAKUWA TUNAONA BUNGE LILILOFANYIWA EDITING.
Sema wabunge wa CCM na sio bunge kwa ujumla,maana lengo ni kutaka utumbo wao wanaoufanya wa kufinyanga demokrasia kwa kuwaonea wapinzani,kwa hoja za msingi zenye maslahi kitaifa zisionekane na umma,

Huu ni mtihani mwingine kwa Rais kikwete,na kama wabunge wa ccm watalipitisha hili basi bunge la wananchi litaamua kuwarudisha majumbani kwao kwani tutakuwa tumewaelewa wako pale kwa maslahi yao na chama chao na rais wao na mafisadi wao
 
Hii pia iingizwe kwenye maajabu saba asilia ya dunia...ipite pasi kupingwa.

Na vile tunapendaga sifa za Tanzania ni nchi pekee yenye blah blah..Tanzania ni mahali pekee penye blah blah...basi na hii tuiongeze kwenye litania hiyo.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Hivyo ndivyo fashist Hitler na mwnzie Mussolini walivyoanza. Power corrupts, but absolute power corrupts absolutely
 
BUNGE KUSITISHA KURUSHA VIKAO VYAKE.

BUNGE linatarajia kufuta utaratibu wa kurusha matangazo ya moja kwamoja kupitia televisheni kwa madai ya kukomesha vitendo vya baadhi ya wabunge kukiuka kanuni za bunge na kuleta vurugu kwa kutafuta umaarufu bila kujua kwamba tabia hiyo inaleta picha mbaya katika jamii.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Bunge Dk.Thomas Kashilila jijini Dar es salaam wakati akitoa taarifa ya mapendekezo ya kuanzisha kamati ya bajeti na kuvunjwa kwa baadhi ya kamati za bunge.

Amesema kuwa ili kuleta maadili kwa baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wanashindwa kufuata kanuni za bunge na kutumia nafasi hiyo kwa kutafuta umaarufu kwa sasa wameomba kufutwa utaratibu wa kurusha matangazo ya bunge ya moja kwa moja badala yake watarekodi ili kuondoa hoja zisizokuwa za msingi.

Ameongeza kuwa kuna idadi kubwa ya wabunge wamekuwa wakikiuka kanuni za bunge makusudi na kusababisha kuleta vurugu bungeni wakati jamii ikiendelea kutazama mabishano yasiyokuwa na hoja za msingi.

Dk Kashilila amesema kuwa kwa sasa kuna baadhi ya kamati za bunge ambazo zimevunjwa kutokana na baadhi ya kamati hizo kuingilia katika utendaji jambo ambalo limekuwa likipoteza maana ya kamati hizo.

Hivi karibuni baadhi ya kamati ikiwemo ile ya Mashirika ya umma POAC zimefutwa na kuacha maswali mengi kwa baadhi ya wananchi juu ya hatua hiyo.

Tanzania ni mchanganyiko wa watu wa aina nyingi, weledi na wasio weledi; majuha na wasio majuha; wakubwa kwa wadogo! watu wenye busara na wasio na busara, wenye kufatilia mambo ya ndani kwa karibu na makini na wasio kuwa wafatiliaji! wote hawa ni watanzania na wote wana haki sawa. Uamuzi wa kusitisha matangazo kama hayo ya bunge ya moja kwa moja inafaa uzingatie makundi yote hayo ya watanzania na pia kusoma alama za nyakati ili uamuzi kama huo usije kuwa na kasoro na kupelekea kadhia zaidi ya hiyo ya kuona hoja za kuudhi za vurugu. Karne ya leo kila kitu kiko wazi na hata vipindi visiporushwa live waweza kushangaa ndio mambo yakawa live zaidi kutoka humo humo bungeni! siungi mkono hoja ya kutorusha vipindi vya bunge live.
 
wastakaoumia zaidi ni CCM maana ndiyo walikuwa anajaribu angalau nao kujionesha kwamba wanawajali wananchi, likiondolewa live si ndiyo watapiga usingizi wa pono na hata wengine kwenda kwenye biashara zao harari na haramu kama kuua tembo... si hakuna atakayeona bunge live!
 
kama wabunge wengi wanavunja kanuni basi kanunizenyewe ndio zinakasoro, zibadilishwe badala ya kutufanya sisi kuwa wahanga kwa kukosa live coverage ya Parliament sessions
 
Walifute bunge kabisa. Halina tena maana kwetu wananchi.
.
Haha, I would also go for it. Kama hawawezi kuonyesha live, tuwe nalo la nini? Bora hata wakionyesha live wananchi tunafarijika kwamba kuna wanaotusaidia kupiga kelele isipokuwa serikali siyo sikivu. Lakini wakifuta kuonyesha live, then tuna haja gani ya kuwa na wabunge? Maana nje ya bunge hawana jipya. Kuna vijiji huwa vinamwona mbunge wakati wa kampeni tu. Wakishapiga kura tu mbunge akashinda ndiyo basi hawatamwona tena hadi uchaguzi mwingine atakapokuja tena kuomba kura. Sasa utaniambia wananchi kama hao wanaona faida yoyote ya kuwa na mbunge? Walifute kabisa hilo bunge halina maana.
 
Kumbe likuvunda watoto wadogo kama wakina Makinda wanauwezo wa kulitilia ubani.

Kuna kazi kubwa ya kuikomboa nchi,watu wanataka bunge la kukenuliana minjino na kupelekeana vimemo kama anavofanya LUKUVI.
 
Last edited by a moderator:
This is silly!! Kama kanuni zipo na zinavunjwa, kwa nini wahusika wasichukuliwe hatua kwa mujibu wa taratibu za uendeshaji wa bunge badala ya kuwaadhibu wananchi kwa kuwanyima haki ya kujua nini kinaendelea bungeni kwa wakati huo (live dialogue) kwa maendeleo ya wananchi wenyewe. Ama ukubwa wa pua si wingi wa makamasi. Magamba walidhani kuwa wengi bungeni watakuwa na hoja za maana kumbe wengi wao ni Low Thinkers!!, Chezea CDM!!

Below 18 years tunahakikisha hawaangalii program za TV ambazo sio productive, hapa wamechemka hata sie watu wazima hawataki tuone fujo zao wakati tunajua mema na mabaya pia tunauwezo wa kuhoji nani kachemka na nani hajachemsha, waache uzushi warushe live tutachuja wenyewe yaani wanatufanya watz wote tupo under 18 kwa kutuwekea Parental guidance kama tunavyowawekea watoto wetu kwenye ving'amuzi
 
Hivi hawaoni kuwa wanawapatia umaarufu upinzani. Jamani ccm fikirien reaction zenu.
 
Hizi porojo alizotangaza Katibu wa bunge zinawaangukia CCM - na hasa wabunge wake. Ni juu yao (wabunge wa CCM) kuhakikisha katibu wa bunge haendelei na maandilizi ya kitanzi cha kuwanyonga. Kama watasitisha kuonesha vikao vya bunge live CCM watapata tabu sana huku uraiani.

Kama wabunge wanakiuka kanuni, solution ni nini? Kale kakitabu anachopiga kelele nacho Makinda kuwa ni kanuni za bunge, kinasemaje pale mbunge/wabunge wanapokiuka kanuni?
 
Back
Top Bottom