Budapest Memorandum: Ulaghai wa kihistoria Warusi waliowafanyia Marekani, Uingereza na Ukraine

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,785
46,503
Mwaka 1991 wakati USSR inavunjika mataifa kadhaa yaliyokuwa yanaunda umoja huo yalikuwa yanamiliki silaha za nyuklia na makombora ya masafa marefu. Ukraine lilikuwa ni taifa mojawapo lililokuwa likimiliki mzigo mkubwa wa silaha za nyuklia na nyinginezo nzito, ilikuwa taifa la tatu duniani kwa umiliki wa silaha za nyuklia baada ya Urusi na Marekani.

Kuvunjika kwa USSR ilikuwa ni furaha kubwa kwa Marekani na Uingereza na West yote kwa ujumla lakini pia kulikuja na hofu kubwa mno kwao kwamba kusambaratika huko kwa USSR kungeleta sintofahamu kubwa ya masuala ya kiusalama Ulaya kwa sababu mataifa mengi yaliyotoka USSR yalikuwa na silaha nyingi nzito zikiwemo nyuklia. Hapo ndipo Rais wa Marekani wa kipindi hicho George H.W Bush akabuni makubaliano ambayo aliwashirikisha Urusi, Uingereza na Ukraine kutatua sintofahamu hiyo. Baadaye makubaliano hayo yaliendelezwa kwa upana na ukubwa zaidi na Bill Clinton na yakaitwa Budapest Memorundum kwa sababu yalisainiwa rasmi katika mji wa Hungary wa Budapest mwaka 1994.

Makubaliano hayo ni marefu sana lakini katika kina chake hasa ilikuwa ni Ukraine kupeleka Urusi au kuharibu silaha zake zote za nyuklia pamoja na makombora yake masafa marefu kwa ahadi ya kwamba Urusi, Marekani na Uingereza hawataingilia uhuru nchi hiyo na wataheshimu mipaka ya Ukraine kama taifa huru. Pia Urusi kukazia ikaahidi msaada na mkopo wa gesi na mafuta wa zaidi ya $billion 2.5. Ukraine walitaka mkataba kamili kutoka kwa Marekani na Uingereza unao guarantee usalama wa mipaka yake lakini hadi mwisho wa makubaliano waliishia kupata ahadi tu kutoka kwa Wamarekani kwamba watapata ulinzi kamili kutoka kwao endapo taifa lolote litawaingilia au kuwavamia baada ya kukabidhi au kuharibu sila zao. Kulitokea mzozo, ubishani na upinzani mkali sana ndani ya Ukraine hadi kusababisha waziri wa ulinzi kujiuzulu lakini mwisho wa siku Ukraine ikaingia makubaliono hayo na kuyatekeleza yote mpaka kufikia mwaka 2008.

Matokeo yake baada ya muda mfupi baada ya Ukraine kutekeleza makubaliano yote Rais wa Urusi Putin akaanza kutoa kauli za ajabu ajabu kuhusu Ukraine kama "Urusi na Ukraine ni watu wamoja na mwisho wa siku lazima watarudi kuwa watu moja", "Ukraine kwanza ni taifa lisilio halisi la kutengenezwa tu lisilo na historia yake" n.k. Urusi ikaanza kuingilia siasa za ndani ya Ukraine kwa nguvu kubwa kipindi cha Rais Viktor Yanukovych wa Ukraine kuanzia 2010 baada ya kuona Ukraine ilikuwa inaelekea mueleko na kuzidisha ukaribu zaidi na West. Ikaanza kuzalisha vikundi vya uasi na kujitenga mipakani mwa Ukraine, ikavamia Ukraine mwaka 2014 na kuendelea kuivamia nchi nzima mwaka 2022. Urusi ikawa imevunja makubaliano yote ya Budapest memorandum na pia Ukraine ikiwa haina sila zake wala guarantee yoyote ya usalama kutoka Marekani au Uingereza. Wamarekani wengi hawataki kulikumbushia hili suala kwa sababu linaanika kiasi gani walivyo na deni kubwa kwa Ukraine.
 
Naomba lete madini zaidi kuhusu kuhusu Ukraine na Urusi. Maana kuna wanaosema tangu asili Ukraine ni sehemu ya Ufalme wa Russ yaani Urusi na kuna Wanaosema Russ ndo sehemu ya Utawala wa Ukraine ya asili makao makuu yakiwa ODESA.
Lete maneno@Yoda
 
Naomba lete madini zaidi kuhusu kuhusu Ukraine na Urusi. Maana kuna wanaosema tangu asili Ukraine ni sehemu ya Ufalme wa Russ yaani Urusi na kuna Wanaosema Russ ndo sehemu ya Utawala wa Ukraine ya asili makao makuu yakiwa ODESA.
Lete maneno@Yoda
Mkuu ni historia ndefu sana mkuu ila ufalme wenyewe ulikuwa unaitwa "Kievan Rus" na pia Ukraine upande mkubwa wa Historia yake imekuwa sehemu moja na Poland-Lithunia kuliko sehumu moja na Urusi.
 
Mwaka 1991 wakati USSR inavunjika mataifa kadhaa yaliyokuwa yanaunda umoja huo yalikuwa yanamiliki silaha za nyuklia na makombora ya masafa marefu. Ukraine lilikuwa ni taifa mojawapo lililokuwa likimiliki mzigo mkubwa wa silaha za nyuklia na nyinginezo nzito, ilikuwa taifa la tatu duniani kwa umiliki wa silaha za nyuklia baada ya Urusi na Marekani.

Kuvunjika kwa USSR ilikuwa ni furaha kubwa kwa Marekani na Uingereza na West yote kwa ujumla lakini pia kulikuja na hofu kubwa mno kwao kwamba kusambaratika huko kwa USSR kungeleta sintofahamu kubwa ya masuala ya kiusalama Ulaya kwa sababu mataifa mengi yaliyotoka USSR yalikuwa na silaha nyingi nzito zikiwemo nyuklia. Hapo ndipo Rais wa Marekani wa kipindi hicho George H.W Bush akabuni makubaliano ambayo aliwashirikisha Urusi, Uingereza na Ukraine kutatua sintofahamu hiyo. Baadaye makubaliano hayo yaliendelezwa kwa upana na ukubwa zaidi na Bill Clinton na yakaitwa Budapest Memorundum kwa sababu yalisainiwa rasmi katika mji wa Hungary wa Budapest mwaka 1994.

Makubaliano hayo ni marefu sana lakini katika kina chake hasa ilikuwa ni Ukraine kupeleka Urusi au kuharibu silaha zake zote za nyuklia pamoja na makombora yake masafa marefu kwa ahadi ya kwamba Urusi, Marekani na Uingereza hawataingilia uhuru nchi hiyo na wataheshimu mipaka ya Ukraine kama taifa huru. Pia Urusi kukazia ikaahidi msaada na mkopo wa gesi na mafuta wa zaidi ya $billion 2.5. Ukraine walitaka mkataba kamili kutoka kwa Marekani na Uingereza unao guarantee usalama wa mipaka yake lakini hadi mwisho wa makubaliano waliishia kupata ahadi tu kutoka kwa Wamarekani kwamba watapata ulinzi kamili kutoka kwao endapo taifa lolote litawaingilia au kuwavamia baada ya kukabidhi au kuharibu sila zao. Kulitokea mzozo, ubishani na upinzani mkali sana ndani ya Ukraine hadi kusababisha waziri wa ulinzi kujiuzulu lakini mwisho wa siku Ukraine ikaingia makubaliono hayo na kuyatekeleza yote mpaka kufikia mwaka 2008.

Matokeo yake baada ya muda mfupi baada ya Ukraine kutekeleza makubaliano yote Rais wa Urusi Putin akaanza kutoa kauli za ajabu ajabu kuhusu Ukraine kama "Urusi na Ukraine ni watu wamoja na mwisho wa siku lazima watarudi kuwa watu moja", "Ukraine kwanza ni taifa lisilio halisi la kutengenezwa tu lisilo na historia yake" n.k. Urusi ikaanza kuingilia siasa za ndani ya Ukraine kwa nguvu kubwa kipindi cha Rais Viktor Yanukovych wa Ukraine kuanzia 2010 baada ya kuona Ukraine ilikuwa inaelekea mueleko na kuzidisha ukaribu zaidi na West. Ikaanza kuzalisha vikundi vya uasi na kujitenga mipakani mwa Ukraine, ikavamia Ukraine mwaka 2014 na kuendelea kuivamia nchi nzima mwaka 2022. Urusi ikawa imevunja makubaliano yote ya Budapest memorandum na pia Ukraine ikiwa haina sila zake wala guarantee yoyote ya usalama kutoka Marekani au Uingereza. Wamarekani wengi hawataki kulikumbushia hili suala kwa sababu linaanika kiasi gani walivyo na deni kubwa kwa Ukraine.
Nimekuwa nawashangaa sana mafuasi wa Putin kulaumu Uingereza na Marekani kuisaidia Ukraine kiulinzi ilihali ilikuwa ni wajibu wa nchi zote tatu pamoja na Urusi kulinda Ukraine chini ya Makubaliano hayo. Kwa vile Putin aliamua kwa makusudi kuvunja makubaliano hayo haina maana kuwa Uingereza na USA nazo zitayavunja.

Putin ni kichaa wa ajabu alieyekuja kuvuruga amani ya ya dunia kwa nia ya kurudisha ule mfarakano wa zamani wa cold war ambao haukuwa mzuri kwa maisha ya binadamu wa kawaida. Sasa sijui yeye anategema kupata nini kutokana na mfarakano huo.
 
Mwaka 1991 wakati USSR inavunjika mataifa kadhaa yaliyokuwa yanaunda umoja huo yalikuwa yanamiliki silaha za nyuklia na makombora ya masafa marefu. Ukraine lilikuwa ni taifa mojawapo lililokuwa likimiliki mzigo mkubwa wa silaha za nyuklia na nyinginezo nzito, ilikuwa taifa la tatu duniani kwa umiliki wa silaha za nyuklia baada ya Urusi na Marekani.

Kuvunjika kwa USSR ilikuwa ni furaha kubwa kwa Marekani na Uingereza na West yote kwa ujumla lakini pia kulikuja na hofu kubwa mno kwao kwamba kusambaratika huko kwa USSR kungeleta sintofahamu kubwa ya masuala ya kiusalama Ulaya kwa sababu mataifa mengi yaliyotoka USSR yalikuwa na silaha nyingi nzito zikiwemo nyuklia. Hapo ndipo Rais wa Marekani wa kipindi hicho George H.W Bush akabuni makubaliano ambayo aliwashirikisha Urusi, Uingereza na Ukraine kutatua sintofahamu hiyo. Baadaye makubaliano hayo yaliendelezwa kwa upana na ukubwa zaidi na Bill Clinton na yakaitwa Budapest Memorundum kwa sababu yalisainiwa rasmi katika mji wa Hungary wa Budapest mwaka 1994.

Makubaliano hayo ni marefu sana lakini katika kina chake hasa ilikuwa ni Ukraine kupeleka Urusi au kuharibu silaha zake zote za nyuklia pamoja na makombora yake masafa marefu kwa ahadi ya kwamba Urusi, Marekani na Uingereza hawataingilia uhuru nchi hiyo na wataheshimu mipaka ya Ukraine kama taifa huru. Pia Urusi kukazia ikaahidi msaada na mkopo wa gesi na mafuta wa zaidi ya $billion 2.5. Ukraine walitaka mkataba kamili kutoka kwa Marekani na Uingereza unao guarantee usalama wa mipaka yake lakini hadi mwisho wa makubaliano waliishia kupata ahadi tu kutoka kwa Wamarekani kwamba watapata ulinzi kamili kutoka kwao endapo taifa lolote litawaingilia au kuwavamia baada ya kukabidhi au kuharibu sila zao. Kulitokea mzozo, ubishani na upinzani mkali sana ndani ya Ukraine hadi kusababisha waziri wa ulinzi kujiuzulu lakini mwisho wa siku Ukraine ikaingia makubaliono hayo na kuyatekeleza yote mpaka kufikia mwaka 2008.

Matokeo yake baada ya muda mfupi baada ya Ukraine kutekeleza makubaliano yote Rais wa Urusi Putin akaanza kutoa kauli za ajabu ajabu kuhusu Ukraine kama "Urusi na Ukraine ni watu wamoja na mwisho wa siku lazima watarudi kuwa watu moja", "Ukraine kwanza ni taifa lisilio halisi la kutengenezwa tu lisilo na historia yake" n.k. Urusi ikaanza kuingilia siasa za ndani ya Ukraine kwa nguvu kubwa kipindi cha Rais Viktor Yanukovych wa Ukraine kuanzia 2010 baada ya kuona Ukraine ilikuwa inaelekea mueleko na kuzidisha ukaribu zaidi na West. Ikaanza kuzalisha vikundi vya uasi na kujitenga mipakani mwa Ukraine, ikavamia Ukraine mwaka 2014 na kuendelea kuivamia nchi nzima mwaka 2022. Urusi ikawa imevunja makubaliano yote ya Budapest memorandum na pia Ukraine ikiwa haina sila zake wala guarantee yoyote ya usalama kutoka Marekani au Uingereza. Wamarekani wengi hawataki kulikumbushia hili suala kwa sababu linaanika kiasi gani walivyo na deni kubwa kwa Ukraine.
Ni kweli kulikuwa na makubaliano kati ya NATO na RUSSIA kwamba Russia haitojitanua tena kwenda west na NATO isijitanue kwenda EAST?
 
Ni kweli kulikuwa na makubaliano kati ya NATO na RUSSIA kwamba Russia haitojitanua tena kwenda west na NATO isijitanue kwenda EAST?
Hakujawahi kuwa na hayo makubaliono. Mahusiano ya NATO yako rasmi katika NATO-Russia founding Act, 1997 ambapo pamoja mambo mengine walikubaliana kuheshimu mipaka ya nchi zote na uhuru wa nchi kuchagua mafungamano inayotoka.
 
Hakujawahi kuwa na hayo makubaliono. Mahusiano ya NATO yako rasmi katika NATO-Russia founding Act, 1997 ambapo pamoja mambo mengine walikubaliana kuheshimu mipaka ya nchi zote na uhuru wa nchi kuchagua mafungamano inayotoka.
Screenshot_2024-04-24-14-50-33-77_96b26121e545231a3c569311a54cda96.jpg
 

Iulize makubaliano kati ya NATO na RUSSIA kwamba Russia haitojitanua tena kwenda magharabi na NATO isijitanue kwenda mashariki yanaitwaje, yalifanyikia wapi na viongozi gani wa Marais gani wa Marekani na Urusi waliohusika.

Pia iulize kiongozi wa zamani wa USSR, Mikhail Gorbachev alisema nini katika ya interview ya mwaka 2014 kuhusu NATO kujitanua.
 
Kwa kuongezea language iliyotumika kwenye budapest memorandum ilikuwa tricky kwasababu lilitumika neno "assurance" na sio "gurantee" ukiangalia tafsiri ya kawaida kwa maneno yote tofauti yake ni ndogo sana ila ukija in military terms Gurantee unakuwa na nafasi kubwa sana kama ikitokea tatizo basi moja kwa moja wataingia direclty kukusadia ila assurance ni kinyume.
 
Kwa kuongezea language iliyotumika kwenye budapest memorandum ilikuwa tricky kwasababu lilitumika neno "assurance" na sio "gurantee" ukiangalia tafsiri ya kawaida kwa maneno yote tofauti yake ni ndogo sana ila ukija in military terms Gurantee unakuwa na nafasi kubwa sana kama ikitokea tatizo basi moja kwa moja wataingia direclty kukusadia ila assurance ni kinyume.
Ukraine walipewa mkataba kama wa Mangungo
 
Nimekuwa nawashangaa sana mafuasi wa Putin kulaumu Uingereza na Marekani kuisaidia Ukraine kiulinzi ilihali ilikuwa ni wajibu wa nchi zote tatu pamoja na Urusi kulinda Ukraine chini ya Makubaliano hayo. Kwa vile Putin aliamua kwa makusudi kuvunja makubaliano hayo haina maana kuwa Uingereza na USA nazo zitayavunja.

Putin ni kichaa wa ajabu alieyekuja kuvuruga amani ya ya dunia kwa nia ya kurudisha ule mfarakano wa zamani wa cold war ambao haukuwa mzuri kwa maisha ya binadamu wa kawaida. Sasa sijui yeye anategema kupata nini kutokana na mfarakano huo.
Dunia ilikuwa na amani kabla ya Putin ?
 
Nimekuwa nawashangaa sana mafuasi wa Putin kulaumu Uingereza na Marekani kuisaidia Ukraine kiulinzi ilihali ilikuwa ni wajibu wa nchi zote tatu pamoja na Urusi kulinda Ukraine chini ya Makubaliano hayo. Kwa vile Putin aliamua kwa makusudi kuvunja makubaliano hayo haina maana kuwa Uingereza na USA nazo zitayavunja.

Putin ni kichaa wa ajabu alieyekuja kuvuruga amani ya ya dunia kwa nia ya kurudisha ule mfarakano wa zamani wa cold war ambao haukuwa mzuri kwa maisha ya binadamu wa kawaida. Sasa sijui yeye anategema kupata nini kutokana na mfarakano huo.
haya yote yasingetokea ikiwa Ukraine wasingeandika katiba inayotaja mission yao ya kujiunga nato.....

Putin angekua mtu mjinga na mpumbavu zaidi kuwahi kuwepo duniani kama angekaa kimya huku adui zake wakijiandaa kuweka makombora mlangoni mwake!

lengo na matajiri wanaotawala US ni kupora utajiri wa Urusi kama wanavyopora wa afrika, endapo Putin angekaa kimya basi miaka 10-20 ijayo Russia ingekua na vita vya wenyewe kwa wenyewe, ingevunjika vunjika au ingekuwa kama congo,
 
haya yote yasingetokea ikiwa Ukraine wasingeandika katiba inayotaja mission yao ya kujiunga nato.....

Putin angekua mtu mjinga na mpumbavu zaidi kuwahi kuwepo duniani kama angekaa kimya huku adui zake wakijiandaa kuweka makombora mlangoni mwake!

lengo na matajiri wanaotawala US ni kupora utajiri wa Urusi kama wanavyopora wa afrika, endapo Putin angekaa kimya basi miaka 10-20 ijayo Russia ingekua na vita vya wenyewe kwa wenyewe, ingevunjika vunjika au ingekuwa kama congo,
Na wewe ni mmoja wa victims walioathirika na hizo propaganda za Putin za kudai kuwa Marekani inataka kuiangusha Urusi. Iwapo Marekani ingekuwa inataka kufanya hivyo, kwanza isingesimamia hiyo Budapest memorandum kuhakikisha silaha zote za Nyuklia zinakwenda Urusi na kuiacha Ukraine haine Kitu. Pili, Marekani ilikuwa na takriban miaka kumi za kuingusha kabisa Urusi yote baada ya kuvunjika kwa USSR. Badala yake katika kipindi cha kuanzia 1994 hadi 2004 Marekani iliisaidia sana Urusi kuimarisha uchumi wake bila vikwazo vyovyote; Mpaka sasa hivi Urusi inadaiwa fedha nyingi sana na Marekani ilizokopeshwa kwa ajili ya kujenga uchumi wake. Elewa hapa kuwa inadaiwa pesa ilizokopa (kama Tanzania inavyokopa), siyo pesa za kuuza hati fungante kama ambazo Marekani inadaiwa.

Tatizo la Putin ni nia ya kung'ang'ania madaraka tu, kwani kosa kubwa la Ukraine na Georgia limekuwa lile la kufanya uchaguzi na kubadilisha viongozi. Huo unakuwa ni mfano mbaya sana mlangoni mwake ambaye haamini utamaduni wa kubadili viongozi; hawezi kuishambulia Belarus mpaka pale watakapobadilisha rais
 
Iulize makubaliano kati ya NATO na RUSSIA kwamba Russia haitojitanua tena kwenda magharabi na NATO isijitanue kwenda mashariki yanaitwaje, yalifanyikia wapi na viongozi gani wa Marais gani wa Marekani na Urusi waliohusika.

Pia iulize kiongozi wa zamani wa USSR, Mikhail Gorbachev alisema nini katika ya interview ya mwaka 2014 kuhusu NATO kujitanua.
Nakwambia hawa ni watu wa vijiweni tu bwana hawawezi kujua hayo kwani Gorbachev alisema wao waliongelea mambo ya upunguzaji wa silaha za hatari tu na wala hawakuongelea mambo ya Nato.
 
haya yote yasingetokea ikiwa Ukraine wasingeandika katiba inayotaja mission yao ya kujiunga nato.....

Putin angekua mtu mjinga na mpumbavu zaidi kuwahi kuwepo duniani kama angekaa kimya huku adui zake wakijiandaa kuweka makombora mlangoni mwake!

lengo na matajiri wanaotawala US ni kupora utajiri wa Urusi kama wanavyopora wa afrika, endapo Putin angekaa kimya basi miaka 10-20 ijayo Russia ingekua na vita vya wenyewe kwa wenyewe, ingevunjika vunjika au ingekuwa kama congo,
1. Utajiri wa Afrika unaporwaje wakati tunaona kila nchi ya Afrika ikiwa inatawaliwa na waafrika wenyewe. Unaweza ukatupa uthibitisho wowote wa madai yako..?

2. Mimi nafikiri Ukraine ni nchi huru tu kama vile Tanzania, Kenya, Zambia nk, sasa kuna nchi duniani yenye haki ya kuichagulia nchi yoyote maadui au marafiki.

3. Unafahamu chochote kuhusu Budapest Agreement iliyohusisha mataifa ya Ukraine, Marekani, Uingereza na Russia.
 
Mwaka 1991 wakati USSR inavunjika mataifa kadhaa yaliyokuwa yanaunda umoja huo yalikuwa yanamiliki silaha za nyuklia na makombora ya masafa marefu. Ukraine lilikuwa ni taifa mojawapo lililokuwa likimiliki mzigo mkubwa wa silaha za nyuklia na nyinginezo nzito, ilikuwa taifa la tatu duniani kwa umiliki wa silaha za nyuklia baada ya Urusi na Marekani.

Kuvunjika kwa USSR ilikuwa ni furaha kubwa kwa Marekani na Uingereza na West yote kwa ujumla lakini pia kulikuja na hofu kubwa mno kwao kwamba kusambaratika huko kwa USSR kungeleta sintofahamu kubwa ya masuala ya kiusalama Ulaya kwa sababu mataifa mengi yaliyotoka USSR yalikuwa na silaha nyingi nzito zikiwemo nyuklia. Hapo ndipo Rais wa Marekani wa kipindi hicho George H.W Bush akabuni makubaliano ambayo aliwashirikisha Urusi, Uingereza na Ukraine kutatua sintofahamu hiyo. Baadaye makubaliano hayo yaliendelezwa kwa upana na ukubwa zaidi na Bill Clinton na yakaitwa Budapest Memorundum kwa sababu yalisainiwa rasmi katika mji wa Hungary wa Budapest mwaka 1994.

Makubaliano hayo ni marefu sana lakini katika kina chake hasa ilikuwa ni Ukraine kupeleka Urusi au kuharibu silaha zake zote za nyuklia pamoja na makombora yake masafa marefu kwa ahadi ya kwamba Urusi, Marekani na Uingereza hawataingilia uhuru nchi hiyo na wataheshimu mipaka ya Ukraine kama taifa huru. Pia Urusi kukazia ikaahidi msaada na mkopo wa gesi na mafuta wa zaidi ya $billion 2.5. Ukraine walitaka mkataba kamili kutoka kwa Marekani na Uingereza unao guarantee usalama wa mipaka yake lakini hadi mwisho wa makubaliano waliishia kupata ahadi tu kutoka kwa Wamarekani kwamba watapata ulinzi kamili kutoka kwao endapo taifa lolote litawaingilia au kuwavamia baada ya kukabidhi au kuharibu sila zao. Kulitokea mzozo, ubishani na upinzani mkali sana ndani ya Ukraine hadi kusababisha waziri wa ulinzi kujiuzulu lakini mwisho wa siku Ukraine ikaingia makubaliono hayo na kuyatekeleza yote mpaka kufikia mwaka 2008.

Matokeo yake baada ya muda mfupi baada ya Ukraine kutekeleza makubaliano yote Rais wa Urusi Putin akaanza kutoa kauli za ajabu ajabu kuhusu Ukraine kama "Urusi na Ukraine ni watu wamoja na mwisho wa siku lazima watarudi kuwa watu moja", "Ukraine kwanza ni taifa lisilio halisi la kutengenezwa tu lisilo na historia yake" n.k. Urusi ikaanza kuingilia siasa za ndani ya Ukraine kwa nguvu kubwa kipindi cha Rais Viktor Yanukovych wa Ukraine kuanzia 2010 baada ya kuona Ukraine ilikuwa inaelekea mueleko na kuzidisha ukaribu zaidi na West. Ikaanza kuzalisha vikundi vya uasi na kujitenga mipakani mwa Ukraine, ikavamia Ukraine mwaka 2014 na kuendelea kuivamia nchi nzima mwaka 2022. Urusi ikawa imevunja makubaliano yote ya Budapest memorandum na pia Ukraine ikiwa haina sila zake wala guarantee yoyote ya usalama kutoka Marekani au Uingereza. Wamarekani wengi hawataki kulikumbushia hili suala kwa sababu linaanika kiasi gani walivyo na deni kubwa kwa Ukraine.

Asante sana kwa kulieleza hili. Pia tunaomba source ili tupate kujielimisha zaidi kuhusu hili.
 
Back
Top Bottom