Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,194
- 10,929
Kufuatia shambulia kubwa kwenye ukumbi wa starehe jijini Moscow ambapo kundi la ISIS lilijitaja kupitia vyombo vya magharibi kuwa ndilo lililohusika.Urusi imeonekana kutoshawishika na uozo wa taarifa hizo.
Watu kadhaa walikamatwa mara tu baada ya shambulio hilo kutokea ambapo watu zaidi ya 130 wamefariki dunia.
Tangu taarifa hizo za tukio na tuhuma za washukiwa kutoka nchi marafiki wa Ukraine kwa upande wake Urusi haijaonekana kutaja chochote kuhusu kikundi chochote cha kiislamu. Badala yake jeshi la Urusi limeshambulia kwa nguvu kubwa maeneo mbali mbali ya Ukraine yote. Shambulio ambalo ni kubwa kufanyika kwa siku za karibuni.
Kwa upande mwengine Urusi imeitaka Marekani isaidie kupatikana kwa wahusika kufuatia kauli yake kwamba Ukraine sio waliotekeleza shambulia hilo.
Watu kadhaa walikamatwa mara tu baada ya shambulio hilo kutokea ambapo watu zaidi ya 130 wamefariki dunia.
Tangu taarifa hizo za tukio na tuhuma za washukiwa kutoka nchi marafiki wa Ukraine kwa upande wake Urusi haijaonekana kutaja chochote kuhusu kikundi chochote cha kiislamu. Badala yake jeshi la Urusi limeshambulia kwa nguvu kubwa maeneo mbali mbali ya Ukraine yote. Shambulio ambalo ni kubwa kufanyika kwa siku za karibuni.
Kwa upande mwengine Urusi imeitaka Marekani isaidie kupatikana kwa wahusika kufuatia kauli yake kwamba Ukraine sio waliotekeleza shambulia hilo.