...............Mtizamo wangu ni kama ifuatavyo:-
Serikali ilitoa Standing Order kwa BOT kulipa madeni ya EPA kadri fedha za kigeni zinavyopatikana.Unatoa standing order inaamisha kuwa benki inatekeleza tu haina haja ya kuconsult serikali(Pay Master General wala Waziri).Kwahiyo sioni sababu ya kuwaingiza Mhe Mramba na Mgonja(in his capacity kama Paymaster General).Kama responsibility ilipewa BOT then the BOT Board of Directors(hapa Mgonja yupo na sio Balali peke yake),Director of Economic Policy na watu wa kitengo cha Debt Management Unit. Hawa ndio wako direct responsible.Kwa jinsi hii summary inaonyesha kilichotokea ni Clear Fraud kati ya BOT na waliolipwa.Mimi pia ningependa sana either Mramba au Megji wajiuzulu lakini sidhani kama wako directly responsible.
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ndio mwenye jukuma la ku audit BOT, je kwa nini hakufanya hivyo yeye mwenyewe?Kama hakuwa hana uwezo(Technical Competence) wa kufanya hivyo, je ni kwa nini alikubali Delloite(CAG Agent)akubali kufukuzwa(kukatokea kutoelewa!!!!!! na BOT. Kwani Delloitte walipewa kazi na Board ya BOT au CAG?
CAG naye yuko responsible kwa kushinda kualert of a possible serious Audit breach on time.
Haya yalikuwa ni madeni ya muda mrefu mno inakuwaje BOT na Serikali kukubali kulipa kwa idhini(through Notarized Deeds of Assigmment). Huitaji kwenda shule kujua hii ndio ilikuwa loophole ya kuzitoa hizi fedha maana zilishakuwa unclaimed kwa muda mrefu na hata hao genuine wadai waliisha yafutilia mbali hayo madeni.Toka 1970 hujalipwa, huwezi kuendelea kuweka kwenye vitabu vyako.Haya makampuni 22(nina huakika hizi kampuni zote zilisajiliwa after 2004), yalitoa records hizi za madeni yaliyokufa hapo hapo BOT, wakaingia Samora, wakatengeneza letter head na deed of assignement, malawyer of Malegesi Calibre waka notarised hela ikatoka.Simple kama kumsukuma mlevi.
Roho inauma sana jamani.