BoT Saga Unfolding: Basil Mramba ajiuzulu - Wito

Mwanakijiji,

Hivyo ndivyo anavyotakiwa kufanya siku zote, ni sehemu ya majukumu yake. Sasa tumpongeze nini. Ila anapoboronga lazima kope zetu zinyanyuke.
 
Mama Zk, kilimponza kupingana na hoja ya Slaa kiwazi wazi! Yeye pale angesema kweli shida ipo na tunaishughulikia badala ya kuungana na Balali, Six and the compony kusema tuhuma ni za uongo wakati alijua ni za kweli!


This summarises it all!
 
Mwanakijiji,

Hivyo ndivyo anavyotakiwa kufanya siku zote, ni sehemu ya majukumu yake. Sasa tumpongeze nini. Ila anapoboronga lazima kope zetu zinyanyuke.

sijasema apongezwe kwani mambo ya kupongeza viongozi kwa wajibu wao mie simo. Ninachosema ni watu kurecognize and appreciate it. Kuna watu wameuliza "baada ya kugundua alifanya nini?" Jibu ni yeye ndiye aliyeagiza uchunguzi ufanyike, na ni yeye aliyesababisha Ernst and Young kupatikana mwezi Mei mwaka jana. tena kwa tukio moja hilo la EPA. Hiyo ilikuwa kabla ya Dr. Slaa kuja hadharani na hoja ya ufisadi Benki Kuu na kabla ya Buzwagi na Orodha ya mafisadi.

Kusema kuwa hakufanya kitu baada ya kuona tatizo ni kukejeli ukweli, na kutotaka kukiri kitu dhahiri. Mama Meghji hakukaa kimya kama walivyofanya kina Mramba, hakukaa kimya kama Mgonja au hata Rais mwenyewe.

Yeye alifanya kitu na matokeo yake ni hiyo ripoti ya Ernst and Young. Kwanini tunataka kumuangamiza mtu aliyeko upande wetu? Hilo ndio linanisumbua, kama ni suala la wapinzani kuumizwa kwa vile hakumtetea Dr. Slaa, I think they need to get over their emotions na kukubali ukweli. Meghji ni sehemu ya serikali, msimamo wake wa hadharani ni msimamo wa serikali na si wa mtu binafsi. Natumaini angekuwa upfront lakini alifanya alichofanya na matokeo yake watu wanakamatwa na polisi, wengine kesi zinaandaliwa, na visa zinafutwa.

Sisi kwa vile tuliumizwa na msimamo wake hadharani tunataka kumwajibisha kwa vile hakupigia makofi hoja ya Dr. Slaa! Tumwajibishe shahidi pekee aliyetokea hadharani kumnyoshea kidole Balali wakati wanaume wengine na mitumbo yao wanagwaya hata kuzungumzia EPA? tuwe wa kweli, Meghji mnataka kumtoa kafaya ya bure kwa sababu za kihisia na si za kihalisia.
 
Mzee Mwanakijiji,
Shukran kwa kunipa mwanga ktk hilo lakini nina maswali machache hapa:-
1. Kabla ya kuchukua hatua hiyo ya kuita wakaguzi, huyu mama Meghji alikuwa akijua kilichotokea Benki kuu?
2. Je, ni baada ya kugundua kwake kuwa kafungiwa kanya boya ndipo alipotoa maagizo ya uchunguzi kuhusiana na scandal hiyo... then why LIE to us kuwa hapakuwepo na ubadhilifu wowote. Kumbuka tu anapojibu hoja Bungeni hamjibu Dr. Slaa ila hujibu tuhuma kwa wananchi wote akiwakilisha serikali. Kifupi katudanganya UMMA wote mahala akijua ukweli ni upi. Yale yale ya Karamagi! -kulindana.
3. Nikinukuu maelezo yako yaonyesha wazi bado anazidi kutudanganya sisi ikiwa wahusika wakubwa ni Mramba na Mngoja inakuwaje yeye lawama zote kamshushia Balali hali picha nzima anaifahamu?.... Je, bado anazungumza kwa niaba ya serikali kwa hiyo kulindana ndio culture inayokubalika.
4. Navyoelewa mimi report bado wanayo mkononi na haijawekwa wazi huyu mama leo hii ni kulingana na report hiyo kiasi kwamba anajaribu kuficha madhambi yake kabla ya hiyo report haijawa released kwa wananchi?...
Why now, all of a sudden baada ya uchunguzi anakubali yote haya ya kudanganywa hali info nzima alikuwa nayo kabla hata hajawaita wachunguzi?
 
Watanzania, ni vizuri tukawa macho.Hichi anachofanya JK ni changa la macho kama mojawapo ya mbinu za kumpandisha chati,Tayari kwa uchaguzi wa 2010.
Hapa watu mkitaka jua ni kwanini walikataa kuwa hawajapokea barua ya kujiuzuru kwa Balali?Nia ni kuonyesha kuwa JK anafanya kazi,na aihitaji mambo makubwa kuwadanganya watanzania.Mojawapo ni kujifanya umelivalia njuga suala la wizi wa BOT.Lakini tunachofanyiwa ni kiini macho tu.
Ona wabongo walivyokwishaanza piga makofi!!!!
 
...............Mtizamo wangu ni kama ifuatavyo:-

Serikali ilitoa Standing Order kwa BOT kulipa madeni ya EPA kadri fedha za kigeni zinavyopatikana.Unatoa standing order inaamisha kuwa benki inatekeleza tu haina haja ya kuconsult serikali(Pay Master General wala Waziri).Kwahiyo sioni sababu ya kuwaingiza Mhe Mramba na Mgonja(in his capacity kama Paymaster General).Kama responsibility ilipewa BOT then the BOT Board of Directors(hapa Mgonja yupo na sio Balali peke yake),Director of Economic Policy na watu wa kitengo cha Debt Management Unit. Hawa ndio wako direct responsible.Kwa jinsi hii summary inaonyesha kilichotokea ni Clear Fraud kati ya BOT na waliolipwa.Mimi pia ningependa sana either Mramba au Megji wajiuzulu lakini sidhani kama wako directly responsible.

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ndio mwenye jukuma la ku audit BOT, je kwa nini hakufanya hivyo yeye mwenyewe?Kama hakuwa hana uwezo(Technical Competence) wa kufanya hivyo, je ni kwa nini alikubali Delloite(CAG Agent)akubali kufukuzwa(kukatokea kutoelewa!!!!!! na BOT. Kwani Delloitte walipewa kazi na Board ya BOT au CAG?
CAG naye yuko responsible kwa kushinda kualert of a possible serious Audit breach on time.

Haya yalikuwa ni madeni ya muda mrefu mno inakuwaje BOT na Serikali kukubali kulipa kwa idhini(through Notarized Deeds of Assigmment). Huitaji kwenda shule kujua hii ndio ilikuwa loophole ya kuzitoa hizi fedha maana zilishakuwa unclaimed kwa muda mrefu na hata hao genuine wadai waliisha yafutilia mbali hayo madeni.Toka 1970 hujalipwa, huwezi kuendelea kuweka kwenye vitabu vyako.Haya makampuni 22(nina huakika hizi kampuni zote zilisajiliwa after 2004), yalitoa records hizi za madeni yaliyokufa hapo hapo BOT, wakaingia Samora, wakatengeneza letter head na deed of assignement, malawyer of Malegesi Calibre waka notarised hela ikatoka.Simple kama kumsukuma mlevi.

Roho inauma sana jamani.

hebu jamani someni maoni ya mbangaizaji halafu tujiulize,

Waziri wa Fedha, CAG na BoT wanashirikiana vipi?

1. CAG ali-hire Delloit & Touche kufanya Audit....BoT etc....wakiwa bado kumaliza ukaguzi wao wakaondolewa.....tunaambiwa eti sababu ni BoT kutoelewana nao

2. Mama Meghji alimuagiza CAG ku-hire auditor mwingine E&Y.....na ripoti imetoka

Maswali

1.Ni nani mwenye mamlaka ya mwisho kusema Auditor atafutwe? Waziri/CAG?
2.Ni sababu zipi zilizofanya Delloit & Touche wasitishwe? na nini yalikuwa madhara (kwa serikali) ya kutatisha mkataba wao?
3. Je ni uongo wa barua ya Balali ndio iliyopelekea kufutwa kwa ukaguzi wa D&T au ni kutokana malalamiko ya BoT?
 
Vyombo vya habari vimebaini kuwa Mkurugenzi wa kampuni inayohakiki makampuni yanayochimba dhahabu Alex Stewarts Assayers ni mtoto wa Mhe. Basil Pesambili Mramba aliyekuwa Waziri wa Fedha wakati kampuni hiyo ilpopata mkataba huo Juni 2003. Katika miaka miwili ya mkataba huo, kampuni hii imekuwa inalipwa dola 751,267 sawa na sh. 939 millioni kila mwezi. Kwa muda wa miaka miwili imejikusanyia dola milioni 18 sawa na sh. 22.5 bilioni. Kampuni hii pia ilisamehewa kodi kwa notisi za serikali za Novemba 25 2005 iliyotiwa saini na aliyekuwa Waziri wa Fedha. Ni wazi kuna mgongano wa manufaa (conflict of interest) ya Waziri wa fedha kuipa mkataba kampuni ambayo mtoto wake ni mkurugenzi na pia kuisamehe kodi. Mpaka hivi sasa serikali haijatoa maelezo ya kina kufafanua utata huu ambao unaashiria matumizi mabaya ya madaraka kunufaisha familia yako ambayo ni rushwa. Rais anawajibika kulichunguza suala hili kwa kina na ikiwa taarifa ambazo zimeandikwa katika vyombo vya habari na vielelezo vyake zina chembe ya ukweli, basi waziri awajibishwe kwa kufukuzwa kazi na Tume ya Kuzuia Rushwa ichukue hatua za kisheria kuwafikisha wahusika mahakamani.

Kutoka: http://cuf-tz.com/666.html

Jamani watanzania, viko wapi asasi zisizo za kiserikali? Napenda tuonyeshe kuwa hatupendezwi na haya. Huku kuandika kwenye JF hakutoshi kwa sababu ni watu wachache sana wanaopata ujumbe huu. Ningependa tuone shinikizo toka kwa wananchi badala ya kuacha kila kitu kwa JK. JK hana uwezo zaidi ya kuchanganyikiwa. Alipita jeshi lakini si mjeshi. Hakika tunaitaji tuingie mitaani kushinikiza Mramba kujiuzuru na kuchukuliwa hatua. Pia lazima Meghji awajibike maana hana faida kwa Taifa hili. Alijua mambo mengi lakini hakudhubutu kuisaidia nchi hii na badala yake alishinikizwa na Dr. Slaa, vyama vya siasa na waisani. Inakuwaje waziri anakili adharani kuwa alidanganywa? Inakuwaje waziri kudhibitisha malipo yaliyofanyika wakati yeye hakuwa madarakani? Na huo usalama wa Taifa kufanywa na makampuni binafsi ni usalama upi huo. Hivi vyama vya siasa vilianzisha sakata hili linapaswa kulimaliza badala ya kutuacha wananchi njia panda. Ni wakati sasa wa mikutano ya jangwani na maandamano nchi nzima kufanyika kuona kuwa MRAMBA, MEGHJI, NA Mgonja wanajiuzuru na kuwajibishwa ipasavyo. Meghji mnafiki mkubwa na ndo maana alitamani kumwozesha binti yake kwa JK.
 
Ombi kwa mwanakijiji na wadau wote wa habari:
1.Tunaomba baadhi ya viongozi wanaotajwa ktk sakata hili watafutwe na wahojiwe na waeleze ni nini wanachojua kuhusu sakata hili na hili litakuwa fundisho kwa wengine.

2.Itafutwe list ya wabunge wote waliopinga hoja hii pale bungeni na kuulizwa kwanini walilidanganya bunge na hii itakuwa fundisho kwa wabunge wetu kutorukia hoja bila uchambuzi wowote.

3.wote kwa pamoja tupige kelele mpaka swala hili litakapo shughulikiwa kikamilifu kwani tusipokuwa makini tutadanganywa na ndio maana wanavuta muda.
 
EWA, unaweza kusaidia katika hilo la pili kwa kwenda kwenye Hansard za bunge, kila mmoja afanye anachoweza ndio ushirikiano huo. Haitoshi kusema "itafutwe", nani atafute?
 
Meghji mnafiki mkubwa na ndo maana alitamani kumwozesha binti yake kwa JK.

HAhahah ina maana mama alitaka muungwana ale kuku na kifaranga wake makubwa haya, mimi nashindwa kuelewa waziri ZM baada ya kugundua alidanganywa na Ballali naye akaandika barua siku nne baadaye zile pesa hazikupitishwa ie hazikwenda kwa mafisadi? Hivi longo longo zingine za kera kweli!!! Ningekuwa karibu na mama Zakia akielezea upuuzi huo walahi ninge mziba kofi!!
 
Ushirombo ukichukua muda kusoma kilichoandikwa sidhani kama utakuwa katika hali ya kushangaa tena.
 
Tuwapongeze mafisadi watuhumiwa kwa kuuchuna.

Pongezi kwa Mkapa unastahili pongezi!
Pongezi kwa Mramba
Pongezi kwa Yona
Pongezi kwa Jeetu Patel
Pongezi kwa Baba wa Richmonduli
Pongezi kwa Mastermind wa KAGODA
Pongezi kwa watuhumiwa mafisadi wengine.

Mmeonyesha uwezo wenu katika "KULA BATI"

Huyu mama aliyetupa ukweli (pamoja na kwamba hakuwepo kwenye mafisadi watuhumiwa) asipongezwe kwa kutupa habari za yaliyojiri.

Mramba! Mramba! Mramba! Mramba! Mramba!
 
Tuwapongeze mafisadi watuhumiwa kwa kuuchuna.

Pongezi kwa Mkapa unastahili pongezi!
Pongezi kwa Mramba
Pongezi kwa Yona
Pongezi kwa Jeetu Patel
Pongezi kwa Baba wa Richmonduli
Pongezi kwa Mastermind wa KAGODA
Pongezi kwa watuhumiwa mafisadi wengine.

Mmeonyesha uwezo wenu katika "KULA BATI"

Huyu mama aliyetupa ukweli (pamoja na kwamba hakuwepo kwenye mafisadi watuhumiwa) asipongezwe kwa kutupa habari za yaliyojiri.

Mramba! Mramba! Mramba! Mramba! Mramba!

Kwanza kabisa vizuri kuona umerudi tena jamvini baada ya kitambo.

Kwenye hilo Insurgent, wee acha 'wale bati' kwa sasa, tatizo walilo nalo ni kuwa mengi yaliyotendeka ni 'siri ya watu zaidi ya mmoja'..... si unajua ugumu wa hili?!


SteveD.
 
Waungwana, kuuliza si ujinga. Swali langu ni hili; kama Mgonja alimwambia waziri wa Fedha kuwa amedanganywa kuhusu fedha za "usalama", kwa nini mama Meghji hakupendekeza kwa Rais kusimamishwa kazi kwa Ballali? I mean, it does make sense to take some disciplinary actions kwa subordinates wako when they lie to you (badala ya kuunda tume ya uchunguzi).

Pamoja na kusema aliyoyasema kumshutumu Ballali, lakini mama Zakia atuambie kwanini hakufanya lolote mpaka baada ya mwaka? Katika kipindi hiki Ballali ameendelea kulipwa, kulipiwa hospitalini, etc na serikali imeendelea kuingia gharama ambazo zingeepukwa. For this, madam minister, you need to take responsibility!
 
Mhh huyu Basiri Mramba inaonekana anaogopwa sana na Kikwete. Yaani JK ameshindwa hata kutaja jina lake kwenye show yake ya kufukuza kazi mtu aliyejiuzulu!

Mramba watanzania wanaendelea kula nyasi kama ulivyotaka! swali ni je, nyasi zikiisha watakula nini? ...... nyama za watu I think

Mafisadi huwa wanahisi wanaogopeka lakini yakiwakuta wananywea.
 
Back
Top Bottom