Boss nisamehe mimi mtoto wa kike

Boss nisamehe mimi mtoto wa kike

Sawa fanya hivi,kubali kwenda,akupe heka za nauli na na marupurupu,ukifika Amsterdam shuka,,kula kuku kwa mrija hela ikiisha rudi kijijini kwenu ukalime
Anaweza kufika Amsterdam na madawa ya kulevya bila kukamatwa?!
 
Mungu aliyekusimamia kabla ya kupata hio kazi, ndo huyo huyo atakayekuwa nawewe baada ya kuachana na hio kazi.

Kuwa na msimamo na uthubutu najua utafanya maamumzi sahihi kwenye hichi kipindi kigumu.
 
Maisha haya asikwambie mtu ,baadaa ya kumaliza chuo na kujiajiri na baadae mtaji kukata,akatokea boss mmoja katika jiji moja kubwa hapa Tanzania ameniajiri kwenye kampuni yake

Nina miezi 6 tu kazini ila sasa boss ananilazimisha nikafuate mzigo HongKong tofauti na kazi niliyoajiriwa

Ananiambia bila kwenda HongKong ataniachisha kazi na anaweza kunifanyia kitu mbaya nikiwambia mamlaka

Ananitaka niende HongKong mara moja tu na nikirudi atanipa kazi special kwenye kampuni na pia atanipa kitita cha kutosha

Naombeni ushauri, nipo kwenye mawazo mazito,je nikikamatwa si ndo maisha yangu yatakuwa hivyo tena? Au niache kazi
Umetunga! Ingekuwa kweli wala usingekuja ku-post hapa. Uwekano wa mtu anayejihusisha na biashara kama hiyo kuona hii post ni mkubwa kabisa. Na akiiona atang'amua wewe siyo mtu wa kuaminika na uwezekano wa kutoa siri ni mkubwa..
 
Kama UMEAMUA kuishi na kuwa HAI basi ACHA KWENDA HUKO....

Kama UMEAMUA kuishi ukiwa mfu...kwa sababu ya sh.milioni 12 ATAKAZOKUPA basi nenda ukawe PUNDA....

DONT DO IT
DONT DO IT
DONT DO IT
DONT DO IT
 
Hapo kuna mawili kama unaenda na boss anataka ukawe kiburudisho chake huko ughaibuni au kama unaenda wewe mwenyewe kwa direction unabebeshwa sembe kwa maana nyingine unakua punda au yote kwa pamoja. Jinasue kwenye huo mtego.
 
Pole sana mpendwa. Hii Ni changamoto inayokutanika kwenye maisha na vijana wengi, na chanzo chake ni kukosa ajira baada ya kupoteza muda mrefu kusoma.

Hili jambo alilokutaka huyo boss kwa kweli naomba toka ndani ya moyo wangu usiende.
Pindi utakapoenda kuna mawili, unaweza ukaenda ukarudi salama na ukapewa kiasi kikubwa Cha hela.

Lakini hela siku zote huwa hazitoshi, wakati mwingine utatamani kwenda Tena na Tena, hapo ndipo kukamatwa kwako kutakapo kujia.

Pindi ukiisha kamatwa huyo boss hata kuwa upande wako kamwe.

Matokeo yake Mungu mwenyewe ndie ajuaye. Lakini litakuacha katika majuto makuu.



Japo maisha Ni magumu, hio kazi acha, japo unahitaji Leo uwe na uwezo wa kujikimu lakini kesho no bora kuliko Jana.

Ikibidi hama huo mji na mawasiliano badilisha Mungu akutangulie uvuke salama.
 
Dada...pole ila Kama mzigo Ni haramu..Acha TU kazi

Mwenyewe unaona uhujumu uchumi hauna dhamana...na huko wananyoga.

Usijitoe kafara.
 
Bora akiona hivyo..ataghairi mission Yake.
Su umesoma lakini?.... kwamba amemwambia akiwaambia mamlaka basi atamfanya kitu mbaya? Mimi mtu wa namna hii nashauri a-deal naye kwa kumfanyia kitu mbaya kabla yeye hajamfanyia.... of course kama ni kweli.
 
Mlamba asali haachi..Utanunua Ist..utaona mbaya utarudi hongkong...ili ununua Tako.la nyani...baadae utaona ndo lifestyle..baadae za mwizi arubaini zinakufika
 
Back
Top Bottom