Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Nimesoma Nigeria miaka minne (University of Lagos) hakuna PhD anaeombakazi ya udereva. Acha kutunga uongo ili kujifurahisha genge lako la NGUMBARU
wewe hujui kitu,sio udereva tu hata vibaka na matapeli pia ni wengi.
Niliwahi kuona kipindi kile cha uchaguzi wao kazi ya kusimamia wapiga kura ilikuwa inafanywa na maprofesa,ambayo huku hata form 4 failure anaweza kuifanya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PhD nyingi za Afrika ni sawa na Poverty,hunger & Diseases!
Hii imekaaje? Yaani ukimbie umande mwenyewe wakati mwenzako kakomaa mpaka kapata PhD halafu unanuna?

Tuache ghilba na chuki dhidi ya wasomi wetu. Kama hatukupata nafasi ya kusoma mpaka PhD tusiendekeze chuki itazidi kutuumiza sisi Kiwango Duni (KIWADU).
 
PhD ni kumiliki mpunga na mali za kutosha, sio vyeti ambavyo mtu anazunguka navyo miaka kibao kutafuta kazi.
 
Kwani Lipumba kafanya kitu gani cha maana zaidi ya kugombania ofisi ya buguruni.
Si bora Diamond tunaona anaisaidia jamii kwa pesa zake.
Halafu tumebuni faraja kuwa elimu sio kitu, kwamba waliofanikiwa kimaisha ni watu wasiosoma.... na tunayo mifano lukuki kujifariji.

Na kwa wingi wao wajinga watawin this trend, no wonder siku hizi watoto wote wanataka wakuwe dayamondi.... na sio Lipumba...vu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
cha sindano iwaingie
Cha ajabu,ngumbaru ina wafuasi wengi mno vyuo vikuu.Graduates wengi sasa hivi huwaambii kitu kuhusu Diamond.
Na nimesikia degree nne inaenda kukesha fiesta tarehe 8 Dec.
Hadi leo tunalazimishwa tuabudu vyeti.Ila niwaambie ukweli ninyi wenye PhD. Fanyeni vitu vya kipihedii!Tutawaheshimu sana.
Mnamuonaje Mesi?Mlushasikia anajitangaza yeye ni mchezaji bora?Si nyie wenyewe mnajipendekeza tu kwake?

Unadhani watu hawamheshimu Askofu Gwajima?Leo hata wewe PhD holder nikuulize,unamchukuliaje prorofesa Lipumba,ukimlinganisha na Millard Ayo?Ungeambiwa na Mungu uchague mmoja kati ya hao awe ndugu yako utamchagua nani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilipataga scholarship ya kusoma PhD sasa kuna mzee mmoja Professor nikaenda kumweleza hiyo habari na kumtaka ushauri. Alichoniambia ni kwamba kwa nafasi uliyonayo ambayo hata PhD holders wanaitamani usipoteze muda kwenda kusoma Zaidi, elimu uliyonayo inakutosha usiende kujaza maelimu halafu ukakutana na matarajio tofauti ukawa frustrated. Nilichukua ushauri wake sikwenda na sijutii .

Wengi wa PhD holders walitegemea kupata matokeo makubwa kimadaraka na kifedha na baada ya kukutana na utofauti wanaishia kudata tu. Kuna mmoja aliingia kujenga fensi mpk ndani ya eneo langu sehemu Fulani nilikuwa nimepanunua nimepaacha. Siku niliyoenda akaniletea nyodo wakati mpk huko kwenye hati halali kabisa. Nilichukua Tingatinga nikabomoa mchana kweupe baada ya kujiridhisha kuwa kavamia. Jamaa alipaniki kaenda polisi mie nikaenda kwa wakili wangu na watu wa Ardhi. Kufika pale anasema unajua mie ni Dokta, nikamwambie kajambe ukanye, kama ungekuwa na akili usingeshindwa kusoma Ramani ya kiwanja
Tulimshtaki na alitulipa Fidia
Saf sana mkuu.
ningekuwepo hiyo siku ya tukio ningekupa zawadi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Saf sana mkuu.
ningekuwepo hiyo siku ya tukio ningekupa zawadi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna moja hiyo kuna madogo walikuwa wameajiriwa benki moja ilishabadilishwa jina juzi kati hapa walikuwa wamefungua tawi moro sasa wakaenda kukaa sehemu kunywa jioni Bar moja maarufu moro town. Sasa madogo wamepiga gambe na wamevimba na funguo zao za magari ya mikopo wanajiona hawana shida hapa duniani.

Sasa pembeni yao kulikuwa na mdingi mmoja kapiga shati jeupe na tai nyekundu suruali nyeusi madogo wakajua meneja wa baa. Si wakamfuata wanalalamika muhudumu anawacheleweshea vinywaji basi yule dingi akajibu vijana kuweni na adabu mie sio meneja me ni lecturer tena PhD holder. Aisee madogo walimchana maana aliwajibu kwa dharau sana
Ukizingatia walikuwa wameshakolea pombe walimzingua wakamwambia PhD si ukanywee Nashera huko unatafuta nini kwenye Bar za mitaani. Nyie ndio mnajifanya mna PhD halafu mnavizia mabaamedi na wasukuma mikokoteni. Watu wacha tucheke, yule dingi akaacha vinywaji akajikataa. Wakati anaondoka jamaa mmoja akamrusha kama anaongelea puani " eti mie ni lecturer nina PhD" kwenda katafute bodaboda ikurudishe kwako mwanga wewe
 
Kuna moja hiyo kuna madogo walikuwa wameajiriwa benki moja ilishabadilishwa jina juzi kati hapa walikuwa wamefungua tawi moro sasa wakaenda kukaa sehemu kunywa jioni Bar moja maarufu moro town. Sasa madogo wamepiga gambe na wamevimba na funguo zao za magari ya mikopo wanajiona hawana shida hapa duniani.

Sasa pembeni yao kulikuwa na mdingi mmoja kapiga shati jeupe na tai nyekundu suruali nyeusi madogo wakajua meneja wa baa. Si wakamfuata wanalalamika muhudumu anawacheleweshea vinywaji basi yule dingi akajibu vijana kuweni na adabu mie sio meneja me ni lecturer tena PhD holder. Aisee madogo walimchana maana aliwajibu kwa dharau sana
Ukizingatia walikuwa wameshakolea pombe walimzingua wakamwambia PhD si ukanywee Nashera huko unatafuta nini kwenye Bar za mitaani. Nyie ndio mnajifanya mna PhD halafu mnavizia mabaamedi na wasukuma mikokoteni. Watu wacha tucheke, yule dingi akaacha vinywaji akajikataa. Wakati anaondoka jamaa mmoja akamrusha kama anaongelea puani " eti mie ni lecturer nina PhD" kwenda katafute bodaboda ikurudishe kwako mwanga wewe
Dah hatosahau maisha yake yote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama elimu hazithaminiwi utegemee kupata maendeleo, ukienda kufanya PhD huku nyuma watu wanajipanga waku-frustratrate wakitegemea kwamba utakaa kwenye position zao, hapo inabidi ufanye maombi sana ujinasue kwenye mitego yao ya hila waliyokuwekea au ufanye michakato ya kuomba kuhama hapo haraka sana.....ulozi, ushirikina, majungu, fitina vinaliangamiza sana hili taifa na tusitegemee kuendelea kwa mentality hizi....
 
Tatizo wenye PHD wakiongea utafikiri hiyi PHD walitunukiwa tu sio kwamba mnachukiwa ila mkiongea mnaongea utumbo


Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani wanaoongea mantiki ni level gani ya elimu mkuu, maana wenye PhD wamepita level zote huko chini hadi kufika hapo walipo, au ugonjwa wa kuongea utumbo umewapata walipoanza kusoma PhD...teh..
 
Kwani wanaoongea mantiki ni level gani ya elimu mkuu, maana wenye PhD wamepita level zote huko chini hadi kufika hapo walipo, au ugonjwa wa kuongea utumbo umewapata walipoanza kusoma PhD...teh..

tunategemea zaidi mtu alosoma awena upeo mzuri sasa unakuta mtu anaongea mpaka unajiuliza hivii huyu ana PHD kweli
 
Kilimo cha matikiti cha kwenye makaratasi.

Huo utumike kama mfano wa kufundishia,, Elimu dunia in matter sana hizi Masters tulizonazo at the end tunaishia kutumikishwa tu na wenye ofisi zao.
 
Utawaweza waswahili kwa wivu hawa.

Ukijionesha tu kwamba una elimu kubwa watakupopoa mpaka utajuta.

Mimi nimetumia robo tatu ya maisha yangu kukaa darasani, na sijuti kabisa.

Nimesoma taaluma zote zilizopo chini ya hili jua. Hii imenifanya nijiamini kuliko shetani.

Kwa kweli kusoma ni raha. Na ni kipaji pia.

Kuna mambo mengi sana ya kujifunza katika hii dunia. Kila siku najifunza kwa kadiri inavyowezekana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
tunategemea zaidi mtu alosoma awena upeo mzuri sasa unakuta mtu anaongea mpaka unajiuliza hivii huyu ana PHD kweli
Tatizo mtu mwenye PhD inahitaji akili kubwa kumwelewa, ndo maana wengi wanafikiri anaongea utumbo. Mfano, unafanya PhD tuseme miaka 3-4 na unaandika andiko lenye kurasa labda 200-400. Tuseme kwenye conference au mjadala unapewa dakika 8 uelezee utafiti wako, utoe matokeo na mapendekezo......yaani u-sammarize utafiti uliofanya kwa miaka 4 na kuandika andiko la kurasa 400 uelezee ndani ya dakika 8......ni lazima uwe na akili kubwa na huyo anayekusikiliza anatakiwa awe na akili kubwa kuweza kuelewa hata mantiki ya kile ulichokiwasilisha......kwa ma-layman inabidi uelezee katika lugha ambayo ni rahisi kwao kuelewa, nayo ni shughuli pevu, hahaha.....
 
Kuna moja hiyo kuna madogo walikuwa wameajiriwa benki moja ilishabadilishwa jina juzi kati hapa walikuwa wamefungua tawi moro sasa wakaenda kukaa sehemu kunywa jioni Bar moja maarufu moro town. Sasa madogo wamepiga gambe na wamevimba na funguo zao za magari ya mikopo wanajiona hawana shida hapa duniani.

Sasa pembeni yao kulikuwa na mdingi mmoja kapiga shati jeupe na tai nyekundu suruali nyeusi madogo wakajua meneja wa baa. Si wakamfuata wanalalamika muhudumu anawacheleweshea vinywaji basi yule dingi akajibu vijana kuweni na adabu mie sio meneja me ni lecturer tena PhD holder. Aisee madogo walimchana maana aliwajibu kwa dharau sana
Ukizingatia walikuwa wameshakolea pombe walimzingua wakamwambia PhD si ukanywee Nashera huko unatafuta nini kwenye Bar za mitaani. Nyie ndio mnajifanya mna PhD halafu mnavizia mabaamedi na wasukuma mikokoteni. Watu wacha tucheke, yule dingi akaacha vinywaji akajikataa. Wakati anaondoka jamaa mmoja akamrusha kama anaongelea puani " eti mie ni lecturer nina PhD" kwenda katafute bodaboda ikurudishe kwako mwanga wewe
Ukijichanganya na wajinga tarajia lolote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom