Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Michewen

JF-Expert Member
Jun 27, 2012
24,551
32,175
Hii imekaaje? Yaani tukimbie umande wenyewe wakati wenzetu wamekakomaa mpaka kapata PhD halafu tunanuna?

Tuache ghilba na chuki dhidi ya wasomi wetu. Kama hatukupata nafasi ya kusoma mpaka PhD tusiendekeze chuki itazidi kutuumiza sisi Kiwango Duni (KIWADU).

1612626647968.jpeg
 

Attachments

  • 3026168_Facebook_media_-_3156867631263277__HD_.mp4
    6.2 MB
Unachokizungumzia sijawahi kukiona. Nilichokiona ni wenye hizo PhD wengi wao hawajui kutangamana na binadamu wenzao ndani ya jamii.

Mara nyingi kwa sehemu ya elimu waliyoipata huwa wanawadharau wale wengine ambao hawajapata sehemu ya elimu kama waliyopata wao. Wanakuwa na viburi na dharau.

Matokeo yake yanakuwa huo uzi uliyouleta wewe. Hawachukiwi kwa sababu ya elimu yao, wanachukiwa kwa sababu ya mienendo yao ya kutangamana na watu ndani ya jamii.
 
Kuna jamaa kasema hapo juu, tatizo la wabongo tunataka wa PhD wafikiri kama 'nyie' wa darasa la saba, wakifikiri kiPhD ndio comment kama yako mkuu zinakuja.
Kukimbia umande ni chaguo.
Bibie Nina masters ya aquatic Science kutoka uholanzi GPA ya 4.3, ningekuwa sipo kwenye kujiwekeza na kufanya mambo ya biashara zaidi sasa hivi ningekuwa na PhD na full scholarships zipo na nazipata daily. Kwahiyo nilichokiandika nakiamini na kukikubali. Mwakyembe ana PhD ya ujinga hawezi kukana somo thesis take kwasababu ya tumbo
 
Bibie Nina masters ya aquatic Science kutoka uholanzi GPA ya 4.3, ningekuwa sipo kwenye kujiwekeza na kufanya mambo ya biashara zaidi sasa hivi ningekuwa na PhD na full scholarships zipo na nazipata daily. Kwahiyo nilichokiandika nakiamini na kukikubali. Mwakyembe ana PhD ya ujinga hawezi kukana somo thesis take kwasababu ya tumbo
Nje ya mada kidogo! Kwa asilimia kubwa Bongo tunasomea mambo kwa kuiona fursa. Vipi kibongo bongo hiyo fani iko poa (aquatic science)?
 
Hii imekaaje? Yaani ukimbie umande mwenyewe wakati mwenzako kakomaa mpaka kapata PhD halafu unanuna?

Tuache ghilba na chuki dhidi ya wasomi wetu. Kama hatukupata nafasi ya kusoma mpaka PhD tusiendekeze chuki itazidi kutuumiza sisi Kiwango Duni (KIWADU).
Safi.Walitumwa na baba zao kuja kusoma wao wakawa daily Club na Ubishoo sasa hata vidigrii vyao vipo katika hali mbaya sana .Eti Leo wanalia hoo tunadharauriwa sasa kama inawauma Rudini shule.PHD ni Ulimwengu Mwingine ule.
 
Safi.Walitumwa na baba zao kuja kusoma wao wakawa daily Club na Ubishoo sasa hata vidigrii vyao vipo katika hali mbaya sana .Eti Leo wanalia hoo tunadharauriwa sasa kama inawauma Rudini shule.PHD ni Ulimwengu Mwingine ule.
Kuna mkuu wa mkoa wa Moro(PHD) ya mambo ya food security wkt Magu anaingia alitengua uteuzi wake jamaa likaanza kulia lia eti ooh eti hata yohana alimezwa kwny tumbo la samaki sijui nini nisamehe baba.Matunda ya PHD hayo

PHD-Permanent Head Damage
 
Tanzania inahitaji watu wenye akili na maarifa mengi kwa ajili ya ujenzi wa Taifa lao na siyo hayo Ma PhD! Huwezi kumpima mtu uwezo wake wa akili eti kwa sababu ana digrii au la! Huko ni kukengeuka na kujitoa ufahamu.

Huenda ile sumu aliyowekewa Mheshimiwa wakati ule wa utawala wa awamu ya nne mpaka akanyonyoka nywele, haijawahi kumuacha salama. Tuendelee kumvumilia na kumsamehe.
 
Back
Top Bottom