Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Bongo ukiwa na PhD lazima uchukiwe

Hii imekaaje? Yaani ukimbie umande mwenyewe wakati mwenzako kakomaa mpaka kapata PhD halafu unanuna?

Tuache ghilba na chuki dhidi ya wasomi wetu. Kama hatukupata nafasi ya kusoma mpaka PhD tusiendekeze chuki itazidi kutuumiza sisi Kiwango Duni (KIWADU).
Na hasa kama huutendei haki huo usomi.
 
Wabongo wanataka mwenye PhD awe na mawazo kama yake wa darasa la saba.

Yaani wanataka wafanane mawazo, bila hivyo mara ni msaliti, mara PhD fake au elimu haija msaidia.

Mtu unalazimisha wa PhD awe na mtazamo kama wako wa darasa la 7.
Hii imemkost kaka yako huko Kyela kwa dharau zake... PHD haikufanyi uwe binadamu wa daraja la juu bali inakufanya uwe mwanazuoni mbobezi kwenye jambo fulani pekee.
 
Siku hizi Phd zipo kibao mbona. Waalimu wengi wa shule za Msingi na Sekondari ama wameshazipata au wako mbioni kuzipata. Masters ndio za kumwaga!!

Swali kubwa ni, Je, zinamchango wowote katika kuboresha ufanisi wa kazi na kuleta mapinduzi halisi ya elimu nchini au imekua ni fashion na kuongeza CV tu kwa wahusika?
 
Tanzania inahitaji watu wenye akili na maarifa mengi kwa ajili ya ujenzi wa Taifa lao na siyo hayo Ma PhD! Huwezi kumpima mtu uwezo wake wa akili eti kwa sababu ana digrii au la! Huko ni kukengeuka na kujitoa ufahamu.

Huenda ile sumu aliyowekewa Mheshimiwa wakati ule wa utawala wa awamu ya nne mpaka akanyonyoka nywele, haijawahi kumuacha salama. Tuendelee kumvumilia na kumsamehe.
Kwa sababu hatuna hizo PhD tafadhali tusilete chuki kwa walio nazo. Pengine, Lawama tuzipeleke kwa wazazi wetu kwa kutupa Elimu ya Kiwango Duni (EKIWADU).
 
Siku hizi Phd zipo kibao mbona. Waalimu wengi wa shule za Msingi na Sekondari ama wameshazipata au wako mbioni kuzipata. Masters ndio za kumwaga!!

Swali kubwa ni, Je, zinamchango wowote katika kuboresha ufanisi wa kazi na kuleta mapinduzi halisi ya elimu nchini au imekua ni fashion na kuongeza CV tu kwa wahusika?
Wabongo na ushamba wao wakiwa na Phd za chupi basi wanajifanya wanajua kila kitu.
 
Yaani huyu Mzee mwenye PhD alivyokuja tu kuandika Uzi huu nimegundua kwamba ni kilaza mkubwa kwa kushindwa tu kugundua kwamba so elimu yake inayochukiwa Bali pumba zenu nyie wenye PhD ndio sababu .

Na kiukweli nafikiri jf Kuna great thinkers kuliko huyu mwenye PhD ya kutolewa jalalani
 
PhD ni PhD tu kila fani inamtegemea mwenzake.Wewe lete dharau wenzako wanatengeneza Maisha
Kwamba huyu anadharau PhD coz ni ya food security? Huyu nae Hana tofauti na mtoa Uzi wote Hawa ni vilaza wenye viwang vidogo kabisa vya kifikra
 
Siku hizi Phd zipo kibao mbona. Waalimu wengi wa shule za Msingi na Sekondari ama wameshazipata au wako mbioni kuzipata. Masters ndio za kumwaga!!

Swali kubwa ni, Je, zinamchango wowote katika kuboresha ufanisi wa kazi na kuleta mapinduzi halisi ya elimu nchini au imekua ni fashion na kuongeza CV tu kwa wahusika?
Wewe mbona Huna hiyo PhD?
 
Wenye mamlaka wanakauli zaidi ya wenye utaalamu, kwetu sisi JPM ndiyo jaji, mganga mkuu, mtunga sharia, injinia mkuu , n.k kila kitu hata chenye kuitaji wataalam wenye mamlaka wanaingilia.. Hivyo hata uwe na PhD ukichangamana na siasa lazima jamii yetu ikuone kituko
 
Back
Top Bottom